60,000×30×3= 5,400,000/= net profit(minimum) na bado unalalamika...
Hiyo corrolla yako ulinunua bei gan?
Typical hesabu za Mtanzania ambae hajawahi fanya biashara. Ingekuwa hivyo kila mtu angeendesha Uber!
13 mega pixel said:Typical hesabu za Mtanzania ambae hajawahi fanya biashara. Ingekuwa hivyo kila mtu angeendesha Uber!
Haha kaniduwaza sana aise . Mbona kwa maelezo yake biashara inaonekana inalipa sana hiyoKwa hiyo baada ya kuacha kazi inayokuingizia 60k per day kwa kuona ni ujinga na kujizeesha sasa hivi umepata inayokuingizia milioni kwa siku ili uendelee kubaki kijana!?
Wakuu habari.
Kama kichwa kinavyojieleza hapo naomba nilete experience yangu ya kua Uber/Taxify Driver kwa kutumia gari binafsi.
Gari ni cc1500 Corolla, na niliifanya kama part-time job sio full time. Mara nyingi nilikua naendesha Kuanzia Ijumaa to Jumapili, saa 2 usiku hadi saa 12 Asubuhi. Ingawa sio kila weekends but Most of them. Na nimefanya kwa muda wa kama miezi mitatu, Tokea mwaka jana November /December. Na nilikua na Apps zote mbili, Uber na Taxify.
Kwa siku faida nikitoa mafuta na kula mimi, nilikua na save kati ya 60,000 hadi 100,000 mambo yakiwa mazuri. Hapo ikiwemo ile hela ya kamisheni (25% kwa Uber) nnayotakiwa ipeleka kwa Uber. Mi sijawahi kuwapa kusema kweli.
Guys hii biashara ni kuzeesha gari, kujichosha, stress za kuwaza ratings na faida ni kwaajili ya kupata hela ya kuspend tu siku 2 au 3 .
Kwamaana hako ka faida ulikokapata kesho utataka ukasafishe gari (20,000 Car Wash), ununue marashi mazuri ya kwenye gari kuwavutia wateja wakupe high ratings, ununue MB za kutosha maana muda wote laziwa uwe online so unakuta unabakiwa na hela ya chakula tu.
Kwa muda huo wa masaa 10 niliopo online muda mwingi, karibia masaa 7, nakua gari inatembea tu. Hapo milage zinaongezeka sana na gari inachakaa sana ukichukulia Watanzania wengi hatukai sehemu rafiki, ila mabondeni sana ambako ukipeleka gari lolote linaweza kutokea. Mfano, nimeshachana Bumper na kusababisha gharama kulitengeneza na kupaka rangi ya Tsh 180,000.
Usiku unakuta wateja ni madogo walevi, miguu juu ya viti na maviatu yao machafu, gari inanuka pombe, hafu wanakutreat cheap sana, yaani kisa wanatoa hela basi ni Kero.
Pia Uber maximum ni watu wanne, sasa unakuta kila trip wewe unapakiza watu 3 to wa 4. Gari inakula sana mzigo. Unaichosha sana na wanakaa maporini huko Kimara mabondeni.
Kwa hitimisho, sio biashara mbaya ila ukiwa na gari dedicated kwa hii biashara na sio gari binafsi. Pia, mitaa yako iwe Posta, na uzunguni ambapo pings zinakua nyingi so muda wa kuzurura bila abiria unakua mdogo na kazi iwe full time (uwe na dereva wako), na gari zuri liwe na cc ndogo 1300 IST na vitz, PASSO na nyingine za cc990 ni nzuri.
Ila kwa upande wangu, hii kitu sio kwaajili ya barabara za Tanzania. Inakula sana kwa dereva.
60,000×30×3= 5,400,000/= net profit(minimum) na bado unalalamika...
Hiyo corrolla yako ulinunua bei gan?
Huyu anatupiga Changa la macho huyuUliwezaje Kuacha Kuwalipa fedha zao Uber?
Madereva Uber Dar wanaburuzwa tu hawajui haki zao haiqezekani utoke Airport (JNIA) mpaka Kempinski kwa 6,000 Tsh na bado unakenua meno tu.
Hope ulim-rate vizurii (5 star)upo sahihi.. mimi nina gari yangu.. ila kuna siku nilipanda uber kutoka muhimbili hadi banana airport na ikasoma 8000 na tulikaa kwenye foleni mbaya. mpaka nikamuonea huruma dereva nikamuongeza 2000
Mueleweni kasema kuwa ni ijumaa kwa jpiliTufanye ka save 60,000/= kwa siku X siku 28 = 1,680,000/=
Hapo UBER alishalipwa 25%...
Au?
Ni kweli siyo biashara nzuri, ila siyo mbaya, kwamba wewe na familia mnakula na watoto wanasoma, hata kodi waweza kulipa, jaribu kuacha kusafisha gari kwa 20,000/=, kwanini usisafishe mwenyewe, mazoezi mazuri mno, tena wewe ndio utalisafisha vizuri zaidi..
Alfu nimegundua wew syo dereva mzuri ...unalalamika bampa kwani ni kila wkt unaharibu bampa au once kwa muda mrefu?Brother. Sifanyi siku zote za wiki. Nafanya siku 3 tu weekends,. Na sio kila weekends. Nilikua nafanya katika mwezi kama weekends 2 au 3.
Ishu inakuja kwenye service mzee. Leo bampa limechanika, kesho muda wa kuchange oil, keshokutwa lingine tena. Hela haiji kubwa kama hesabu ulizoandika hapo.
Nikweli hayuko serious huyu jamaaa alfu analalamika kaaribu bamba lake ndio hapo inamuuma kwani c yey ndio karibu kwa uzembe wake huyu atayumbisha watu wasifanye biashra hii wabaki wao tu huku wakileta changamoto nyingi ili kusudi vijana wakwamee wakose kaz za kufanya13 mega pixel said:
60,000×30×3= 5,400,000/= net profit(minimum) na bado unalalamika...
Hiyo corrolla yako ulinunua bei gan?
Cha kushangaza huyo bwana kaweka 30 (yaani siku 30 badala ya 20 au 24 sababu ya mapumziko)..
Na hesabu ya 60,000/- kwa siku hapana, 30,000/- kwa siku tutakubali...
Kwa hiyo basi...
24 x 30,000/= ni sawa na 720,000/= kwa mwezi...
Sielewi hesabu yake ya siku 30 gari kufanya kazi bila ya dereva au gari kupumzika!
Kweli huyo mbumbumbu wa hii biashara...