JITU LA MIRABA MINNE
JF-Expert Member
- Mar 28, 2015
- 726
- 476
Mmehabarikaje Wandugu,
Nimerudi niliandika uzi kuomba uzoefu kwa waliozoea kusafiri kupitia Mbuga ya mikumi na mimi nilikuwa nataka kupita na Mwanandama wangu.
Niliondoka Moro saa 8 kwa speed ya MOTOCHINI 150 nilifika saa 9:30.Safari inaendelea nimefika Mwanzo wa mbuga naona amani tu, nimepata kujionea swala makundi kwa makundi, pundamilia na twiga kwa mbali huku tembo nao wakiendelea kutembea kwa kujigamba.
Safari inaendeleaa...., wakati bado nipo katikati ya mbuga ghafla kwenye kichaka nasikia kinatikisika ghafla simba kama watano wanatoka wakiwa wa damu mdomoni wakawa wananitizama watatu wakaunguruma huku wanafata usawa wangu nilichofanya ni kuongeza speed 180 kwani BAJA haina kujali BAMPS, wakatrot kidogo wakarudi zao, mbele kidogo mita 200 kwenye mti mkubwa namuona chui akiwa na swala kwenye mti.
Viumbe walionitisha ni Nyati waliopita kwa makundi kuvuka barabara, ilibidi nisisimame bali nirudi nilipotoka hadi nilipoona wamepita wote ndio nikapita speed 120, walirudi baadhi kunifukuzia lakini kwa kuwa wote mnamwelewa ndama alivyo.
Nilitaka kuzimia nimekutana na simba wawili mbele kulia na kushoto wawili katikati wameacha nafasi, nilichofanya ni kuwapita kama mwewe au kipanga hao nduli kwani wote mnajua mziki wao ulivyo.
USHAURI: Jamani ndugu zanguni, hapo mbugani sio pa kupita jioni wala usiku, mimi nimepita jioni mengi niliyoyaona sipiti tena, bora nipakie pikipiki kwenye lori, mnaotaka picha ni ngumu kupata labda ningekuwa nipo na wewe ukashuka kunipiga picha zingetokea vizuri.
HEBU TUAMBIE NA WEWE YALIYOKUKUTA, MIMI NILIPATA PRESSURE SIKU 3
Nimerudi niliandika uzi kuomba uzoefu kwa waliozoea kusafiri kupitia Mbuga ya mikumi na mimi nilikuwa nataka kupita na Mwanandama wangu.
Niliondoka Moro saa 8 kwa speed ya MOTOCHINI 150 nilifika saa 9:30.Safari inaendelea nimefika Mwanzo wa mbuga naona amani tu, nimepata kujionea swala makundi kwa makundi, pundamilia na twiga kwa mbali huku tembo nao wakiendelea kutembea kwa kujigamba.
Safari inaendeleaa...., wakati bado nipo katikati ya mbuga ghafla kwenye kichaka nasikia kinatikisika ghafla simba kama watano wanatoka wakiwa wa damu mdomoni wakawa wananitizama watatu wakaunguruma huku wanafata usawa wangu nilichofanya ni kuongeza speed 180 kwani BAJA haina kujali BAMPS, wakatrot kidogo wakarudi zao, mbele kidogo mita 200 kwenye mti mkubwa namuona chui akiwa na swala kwenye mti.
Viumbe walionitisha ni Nyati waliopita kwa makundi kuvuka barabara, ilibidi nisisimame bali nirudi nilipotoka hadi nilipoona wamepita wote ndio nikapita speed 120, walirudi baadhi kunifukuzia lakini kwa kuwa wote mnamwelewa ndama alivyo.
Nilitaka kuzimia nimekutana na simba wawili mbele kulia na kushoto wawili katikati wameacha nafasi, nilichofanya ni kuwapita kama mwewe au kipanga hao nduli kwani wote mnajua mziki wao ulivyo.
USHAURI: Jamani ndugu zanguni, hapo mbugani sio pa kupita jioni wala usiku, mimi nimepita jioni mengi niliyoyaona sipiti tena, bora nipakie pikipiki kwenye lori, mnaotaka picha ni ngumu kupata labda ningekuwa nipo na wewe ukashuka kunipiga picha zingetokea vizuri.
HEBU TUAMBIE NA WEWE YALIYOKUKUTA, MIMI NILIPATA PRESSURE SIKU 3