Mrejesho: Nimesafiri na BAJA 250 XLR kupitia mbuga ya Mikumi, kwa niliyoyaona sipiti tena

Mrejesho: Nimesafiri na BAJA 250 XLR kupitia mbuga ya Mikumi, kwa niliyoyaona sipiti tena

Yaani unapita speed 150 na unaweza kuona simba ana damu mdomoni!!

Halafu ni nadra sana kuona wanyama hao wote ukiwa unapita Mikumi.

Ila poa tu ngoja tumeze!!

Mkuu afu alipowapita tu wale Simba wenye damu midomoni mbele yake akakutana na kundi la nyati,hakusimama bali aligeuza pikipiki hadi kwa wale simba afu akarudi tena.
Inabidi tukubali tu maana hamna namna tena
 
Wewe jamaaa acha uongoo.....izo adithiii....sema nimecheka kuona jinsi gani uko idle kutunga adithii ya kitoto kama hiii
 
Ingekuwa ni kweli ungekuta wewe ni marehemu sasa
 
Huyu jamaa ni muongo sijapata ona. Mikumi mchana simba wapi na wapi? Almost kila mwezi napita ile njia mara mbili. Nyati, twiga tembo Sawa. Simba labda usiku B-)B-)
 
Hahahah we jamaa umetunywesha chai walahi.....

Mikumi hii hii???
 
Hii story ungesema hata serengeti ungeeleweka, mikumi!!? No way.
 
Jamaa, umejitahidi kutunga hii hadithi , ila hamna shida coz nimecheka sana
 
Hujui hata kutunga hadithi inayofanana na ukweli
 
Yaani unapita speed 150 na unaweza kuona simba ana damu mdomoni!!

Halafu ni nadra sana kuona wanyama hao wote ukiwa unapita Mikumi.

Ila poa tu ngoja tumeze!!

Mkuu umeniwahi hii kauli😂😂😂
 
Mdau umetupa story nzuri. Lakini story yako ni kamba tu....... Anyway tunga nyingine.
 
Mtoa uzi unamiaka mingapi na umeishia darasa la ngapi labda tuanzie hapo...? Maana mie nakupita kwangu mikumi mara zote simba nshamuona mara mbili tena night kali, chui bado.....sasa wewe na pikipiki fasta umewaona, tena na kichaka kimetingishika
 
Wewe ni mwongo kupindukia maana habari ilivyonioongo mtupu.
Hata mimi nina doubt ukweli wa habari hii!
Kwanza barabara hii ina magari mengi sana, kwa hiyo haiwezi kupita dakika tatu hajakutana na gari toka pande zote mbili.
Pili kukutana na makundi ya simba kando ya barabara ni nadra sana mama si uongo
Tatu, chui kumwona Mikumi ni almost impossible barabarani, na uongo wa dhahiri ni ati chui ana swala juu ya mti!

Nne kumwona simba Mikumi tena barabarani ni nadra, ingawaje unaweza kubahatika.
Sasa huyu ndugu kaona almost simba 11 in a singke day!!!!
Haya bwana, halafu nyati ati unawatoka spidi!

Hizi hadithi za kutunga.
 
Mmehabarikaje Wandugu ,
nimerud niliandika uzi kuomba uzoefu kwa waliozoea kusafiri kupitia Mbuga ya mikumi na mm nilikuwa natska kupita na Mwanandama wangu ,
niliondoka Moro saa 8 kwa speed ya MOTOCHINI 150 nilifika saa 9:30
safar inaendelea nimefika Mwanzo wa mbuga naona amani tu ,nimepata kujionea swala makundi kwa makundi,pundamilia na twiga kwa mbali huku tembo nao wakiendelea kutembea kwa kujigamba
safari inaendeleaa....,. wakati bado nipo katikati ya mbuga ghafla kwenye kichaka nasikia kinatikisika ghafla simba kama watano wanatoka wakiwa wa damu mdomoni wakawa wananitizama watatu wakaunguruma huku wanafata usawa wangu nilichofanya nikuongeza speed 180 kwan BAJA haina kujali BAMPS,wakatrot kidogo wakarud zao,mbele kidogo mita 200 kwenye mti mkubwa namuona chui akiwa na swala kwenye mti,
viumbe walionitisha ni Nyati waliopita kwa makundi kuvuka barabara ilibid nisisimame bali nirud nilipotoka hadi nilipoona wamepita wote ndio nikapita speed 120 lakin walirud baadhi kunifukuzia lkn kwa kua wote mnamwelewa ndama alivyo ,nilitaka kuzimia nimekutana na simba wawili mbele kulia na kushoto wawili katikati wameacha nafas nilichofanya nikuwapita kama mwewe au kipanga hao nduli kwan wote mnajua mziki wao ulivyo
USHAURI:Jaman ndugu zangun hapo mbugani sio pa kupita jion wala usiku,mm nimepita jioni mengi niliyoyaona sipiti tena bora nipakie pikipiki kwenye lori ,mnaotaka picha ni ngumu kupata labda ningekua nipo na wewe ukashuka kunipiga picha zingetokea vizuri
HEBU TUAMBIE NA WEWE YALIYOKUKUTA MM NILIPATA PRESSURE SIKU 3
Mkuu pikipiki kama hiyo na mimi ninayo.
Ulipo nunua hawakukuonyesha kitufe pale chini ukibonyeza una paa angani?
Usingepata adha yote hiyo.
 
Umesahau ulivyoona mamba wakingonoka.
 
Braza we ni muongo sana,kwa mikumi ni vigumu sana kuwaona simba na chui kando ya barabara mara nyingi ukipita utaambulia kuwaona swala,twiga,zebra,tembo na nyati kwa mbaaaaliiiiii.

siku nyingine usirudie kutudanganya kitoto tutakunasa vibao!
 
Back
Top Bottom