Mrejesho: Safari yangu ya kwenda kulima mkoa wa Katavi - Wilaya ya Tanganyika, kijiji cha Mwese 4

Iyo ndio mbegu niliyolima wadau.
Kwakweli ni mbegu inafanya vizuri sana kama utahudumia, yani inabeba mahindi makubwa. View attachment 2854587View attachment 2854585View attachment 2854586
 

Attachments

  • 5-13.jpg
    67.6 KB · Views: 61
Mkuu vipi mavuno ya dk 9089 yalikuwa mazuri?
 
Mkuu vipi mavuno ya dk 9089 yalikuwa mazuri?
Mkuu Dk 90-89 yenyewe ilibeba vizuri sana tena sana, lakini Changamoto yake ni kwamba Yani inashambuliwa sana na wadudu waalibifu lakini ukithibiti mapema inafanya vizuri, lakini pia haitaki mvua nyingi maana inakomaa haraka sana.
Yenyewe nilichelewa kuipanda Ili iva vizuri.
Lakini ningeipanda pamoja na tembo ingeoza sana maana ingeivia kwenye mvua nyingi.
Kingine Dk punje zake ni ndogo ndogo sana, uwezi linganisha na mnyama Tembo 719 Yani punje zake ni kubwa sana. Pia inavumilia mvua nyingi. View attachment 2854743
 
Mkuu jifunafu..nikija huko na m6 nje na matumizi..
Nikataka kulima kama ifuatavyo
1.mahindi m3
2.maharage m2
3.karanga au choroko 1m

Naomba unieleweshe mchanganuo wa gharama za matumizi
Pia ikienda poa naeza pata gunia ngapi
Muda wa kukaa huko....soko ninalo ila bei ya kuuza
Je pia lazma niende kwa mtaalam?
Pls....
 
Hahahaha [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] hapo ngoja kwanza nchekeeee, kwamba Kwa mtaalamu.
Lakni ninachojua Kwa hesabu iyo ni kubwa sana Kwa mazingira ya uko najua Itafanya kazi kubwa sana maana ni kwamba gharama za mashamba na uendeshaji Bado upo chini, cost kubwa inakuja kwenye upande wa madawa. Na itapendeza zaidi uwe na vijana wa mkataba maana yake ni kwamba wao watafanya kazi Hadi mavuno.
Upande wa maharage wanaanza kuandaa mashamba mwezi wa pili. Kama Kuna mengine sijakujibu unaweza kuja PM tukaongea zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…