Mrejesho: Ufugaji wa nguruwe, kilimo cha matikiti maji na ufugaji ng'ombe wa maziwa

Mrejesho: Ufugaji wa nguruwe, kilimo cha matikiti maji na ufugaji ng'ombe wa maziwa

Pole sana mkuu,yaliyokukuta kwenye nguruwe
yaliwahi kunikuta.Ila kuna mfugaji ameniambia
kuwa nilikosea,nguruwe mmoja anatakiwa kula kilo moja
ya pumba kwa siku.muda wote uliobakia anatakiwa apewe maji ya kutosha.

Na ikitokea akawa mzembe wa kula,jitahidi uondoe hayo masalia
ili asizoee kula kila wakati.Hayo mabaki kama unafuga bata au kuku wawekee hayo mabaki
na nguruwe mpe maji tu mpaka kesho yake utakapompa haki yaki ya kilo moja ya pumba.
Hii inasaidia kwamba kesho yake ukimuwekea hiyo kilo moja atakula na kumaliza
maana atakuwa na njaa ya jana.
pia epuka mtindo wa kuwawekea nguruwe vitu mbalimbali kama vile mabaki ya vyakula
au makabichi n.k.ukifanya hivyo unamzoesha kula kila mara bila mpangilio
ambao utakughalimu,maana wakihisi njaa watakupigia kelele na kukukosesha amani.

Natarajia kufuga tena kwa kufuata maelekezo hayo,nione kama nitaweza
kupata faida.Hayo maelezo hapo juu nilipewa na mdau anayefuga
ambaye nilimtembelea nikaona mabanda yake ndo akanipa siri hiyo.
Chakula kilo moja kwa siku?
Hii umeifanya au umeitoa kwa wale ma spika?
 
Yaani kwa mwezi nguruwe wanakula laki 3! God forbid!!! Nikagundua nimekuwa mzalishaji mkubwa wa mbolea badala ya nguruwe!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Elimu sahihi na taarifa sahihi , tembelea mabanda ya hao watu, alie post au hao walio like post , ujifunze.. hiyo ni miez minne

huyu ndani yuko mdau anaitwa Malafyale .. ni baba lao kwenye huu ufugaji , miez sita hadi 120 kg anafika , anafugia morogoro hapo
Screenshot_20200406-080341.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole na hongera sana kwa kulifanyia jambo kazi, maana wengi tunaongea sana kutekeleza hakuna....

Mi ninachoweza kusema ni kuwa, Ukifocus ktk kitu kimoja ni rahisi kutoka kuliko kubadilibadili biashara, utaconcentrate Sana na utajua utatue vipi changamoto zitakazokukabili kwa kusoma zaidi, kuulizia waliokwishanya, kuona nk nk..ninachoona hapa Katika mradi wako wa nguruwe cha kwanza hukufanyia utafiti wa kutosha ni kuhusiana na mbegu bora ya kufuga, eneo ulipo mjini VS Kijinini nk, njia za jinsi ya kupunguza gharama za ulishaji.

Aina ya ujenzi WA banda pia ni factor muhimu mno no mno..Kuna vitu ulimiss, baba yangu huu ni mwaka WA 35 anafuga nguruwe na anauza Sana tu na kupata pesa za kumtosha, zamani ilikua kama wewe six months kg 30, sasa hivi kaimprove Sana tu! Hadi Kuna kipindi alikua anauzia wachina laki 3 nguruwe WA miezi mi2, alikua anawaambia siuzi nguruwe mtoto wakawa wanambembeleza akasema bila Laki 3 siuzi, aliuza Sana hicho kipindi...

MOTIVATIONAL SPEAKERS hukupa mwanga sasa wewe kama wewe inapasa kuingia chimbo zaidi, unajiongeza na wewe mwenyewe pia kuona kama kuna ukweli ama lah, all in all Mi nawapenda coz wanahamasisha...

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimeyafurahia sana maneno yako yooote hasa ushauri uliompa muanzisha mada na mfano wa baba yako. Bila shaka tunahitaji kautafiti ka vitendo kabla ya kuyaendea yasemwayo. Kwa mfano, kama mdau angepata fursa ya kujitolea wiki mbili tatu kumsaidia kazi baba yako, angeondoka pale na elimu kubwa kuliko maneno ya matapeli.

Sehemu uliyoniacha kidogo ni kuhusu hawa motivational speaker. Kiufupi, hawakupi mwanga bali wanakupa sababu za kujigeuza fursa kwao. Hawana wanachojua zaidi ya maongezi na uongo.

Mtu mwenye kukupa mwanga hasiti kukuonya juu ya changamoto utakazokutana nazo na masuluhisho ya ukweli. Wao watakwambia changamoto zipo lakini watakupa vile vile suluhisho jepeeesi la kimaandishi halafu...kafie mbele, wao washachukua 20,000 yao.
 
Plz nisaidie formula ya hiz kitu..unawachanganyia pumba na mashudu alone? Au unachanganya na maji pia?
Mimi si mfugaji nguruwe lakini pumba laini ya mpunga,pumba ya mahindi,mashudu ya alizeti,pig boost ni miongoni mwa viambata kwenye mchanganyiko wa chakula cha nguruwe.
Naamini wajuzi wapo humu watakusaidia mkuu
 
Mimi si mfugaji nguruwe lakini pumba laini ya mpunga,pumba ya mahindi,mashudu ya alizeti,pig boost ni miongoni mwa viambata kwenye mchanganyiko wa chakula cha nguruwe.
Naamini wajuzi wapo humu watakusaidia mkuu
Mkuu hii pig boost ungeielezea kidogo kwa faida ya wengi, ni nini hasa na upatikanaji wake.
 
Back
Top Bottom