Mrisho Mpoto: 95% ya waliokataa mkataba wa DP World tuko nao hapa tunaposaini na baadaye tutakula nao Ubwabwa

Mrisho Mpoto: 95% ya waliokataa mkataba wa DP World tuko nao hapa tunaposaini na baadaye tutakula nao Ubwabwa

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Ni Kauli ya Msanii lakini imebeba ujumbe mzito sana.

Yawezekana hao 5% waliopelea kwa mujibu wa takwimu za Mpoto ni wale Chadema na akina Mwabukusi.

Sijajua Mrisho Mpoto alitaka kumaanisha nini hasa lakini Ujumbe wake kwa tafsiri yoyote ile ni mzito.

Mungu wa Mbinguni awabariki 😀
 
Ni kauli za kijinga Sana, yeye anaona mkataba Ni mzuri kwa akili ndogo alizonazo, hivi Tanzania mtu kuonekana kwenye TV anaona ana akili Sana na ujanja kuliko watu wengine wasomi na waelewa wa mambo kumbe hajui wengine wapo hapo kulinda vibarua vyao umri umeshawatupa mkono ya nini kulumbana, tasania ya maigizo kwa nini hakuna walioenda shule wengi Ni waganga njaa wapiga majungu etc
 
Ni Kauli ya Msanii lakini imebeba ujumbe mzito sana

Yawezekana hao 5% waliopelea kwa mujibu wa takwimu za Mpoto ni wale Chadema na akina Mwabukusi

Sijajua Dr Mrisho Mpoto alitaka kumaanisha nini hasa lakini Ujumbe wake kwa tafsiri yoyote ile ni mzito

Mungu wa Mbinguni awabariki 😀
MAONI YA WAKILI BONIFACE MWABUKUSI

Maoni na hoja zangu za Awali kuhusu kusainiwa kwa mikataba mitatu ya uwekezaji wa Bandari. Na Boniface Mwabukusi

1.Mikataba hiyo imefichwa na haijawekwa wazi kwa wananchi wala kuwasilishwa Bungeni kama sheria inavyotaka.kwa hiyo ni muendelezo wa vurugu na ukiukwaji wa sheria.

2.Mikataba hii(HGA) haina nguvu dhidi ya IGA mkataba mama ambapo licha ya mikataba hii (HGA) kusema kuwa itatumia sheria za Tanzania haielezi iwapo sasa zitatumika mahakama na mabaraza ya ndani ya Tanzania katika utatuzi wa migogoro.

3.Rais anasema mkataba huu ni matokeo ya IGA ,Mwingine anasema mikataba hii ni matokeo ya Public Private Partnership.Kama mikataba hii ni matokeo ya PPA kwanini mulipeleka Azimio na Mkataba wa IGA kuridhiwa na Bunge? Kama ni PPA kwanini muweke exclusive clause? Kwanini mgeni amiliki asilimia 40? Je sheria Na.5 na No 6 za mwaka 2017 zinasemaje kuhusu umiliki wa Raslimali za Asili ?

4.Wametuambia kwamba eti tutamiliki kwa ubia wa asilimia 60 kwa Serikali na Asilimia 40 kwa DPW...Hiyo Asilimia 60 ni yaserikali ipi ya Muungano au Tanganyika?

5. Je Zanzibar itapata mgawo kwenye mapato ya bandari ya Tanganyika? Je katika hiyo asilimia 60 kuna viongozi wa Zanzibar wataingizwa kwenye usimamizi wa Bandari za Tanganyika ambazo siyo za muungano?

6. Je hawa wenzetu wametuambia na kutufafanulia ili kupata hiyo asilimia 40 DPW kawekeza kiasi gani na katika maeneo yepi? Kwanini hamjaweka feasibility study wazi kwa Umma ili umma ujue badala yake mkafanya siri na kuitana kwa faragha kana kwamba nchi hii ni shamba lenu binafsi?

7.Je kama HGA ni ya miaka 30 Inter Governmental Agreement (IGA) ni ya miaka mingapi?

Muhimu kujua:

1 .Mbuzi hawezi kuzaa Tembo.IGA ni haramu inapoka Mali asili za watanganyika na kuziweka kwenye mikono ya watu wa chache kwa njia ya ujanja ujanja.

2.Hitaji letu ni IGA ifutwe na kama kuna uwekezaji unafanyika lazima uzingatie maslahi ya Umma na siyo ya viongozi wa ccm na familia zao kwa kuhakikisha

@ Bandari za Tanganyika zinamilikiwa na Umma kama sheria zinavyotaka

@. Kama ni uwekezaji lazima uwe wa mfumo unaotoa nafasi na fursa kwa watanganyika na kampuni za kitanzania kumiliki sehemu kupitia hisa badala ya Kampuni moja ya kigeni kupewa asilimia 40?

WEKENI HUO MKATABA WA HGA WAZI ILI TUUONE NI MATAKWA YA KISHERIA.

BAK MWABUKUSI
SHAMBANI BUSOKELO.
 
Alimaanisha kuwa hiyo 5% ya wasiokuwepo ni wale wale wapingaji wa maendeleo wa siku zote, ambao kazi yao ni kupinga tu.

Mkataba uwe wa manufaa au hasara wanapinga tu.

Makonda akiteuliwa ili kutumikia chama ambacho sio cha kwao wanapinga tu.

Ujenzi wa barabara ya njia nane kutoka Kimara hadi Kibaha wanapinga tu.

Raisi Samia kuendeleza miradi iliyoachwa na mtangulizi wake na pia kuanzisha ya kwake wanapinga tu.

I mean ujumbe wake ulikuwa clear mno. Nashangaa mwana Kawe mwenzangu haujauelewa.
 
Ni Kauli ya Msanii lakini imebeba ujumbe mzito sana.

Yawezekana hao 5% waliopelea kwa mujibu wa takwimu za Mpoto ni wale Chadema na akina Mwabukusi.

Sijajua Dr Mrisho Mpoto alitaka kumaanisha nini hasa lakini Ujumbe wake kwa tafsiri yoyote ile ni mzito.

Mungu wa Mbinguni awabariki 😀
Amepiga kanisa takatifu la mitume
 
Alimaanisha kuwa hiyo 5% ya wasiokuwepo ni wale wale wapingaji wa maendeleo wa siku zote, ambao kazi yao ni kupinga tu.

Mkataba uwe wa manufaa au hasara wanapinga tu.

Makonda akiteuliwa ili kutumikia chama ambacho sio cha kwao wanapinga tu.

Ujenzi wa barabara ya njia nane kutoka Kimara hadi Kibaha wanapinga tu.

Raisi Samia kuendeleza miradi iliyoachwa na mtangulizi wake na pia kuanzisha ya kwake wanapinga tu.

I mean ujumbe wake ulikuwa clear mno. Nashangaa mwana Kawe mwenzangu haujauelewa.
Waliopinga wapo ikulu wanasubiri ubwabwa, TEC njaa zitawaua
 
MAONI YA WAKILI BONIFACE MWABUKUSI

Maoni na hoja zangu za Awali kuhusu kusainiwa kwa mikataba mitatu ya uwekezaji wa Bandari. Na Boniface Mwabukusi

1.Mikataba hiyo imefichwa na haijawekwa wazi kwa wananchi wala kuwasilishwa Bungeni kama sheria inavyotaka.kwa hiyo ni muendelezo wa vurugu na ukiukwaji wa sheria.

2.Mikataba hii(HGA) haina nguvu dhidi ya IGA mkataba mama ambapo licha ya mikataba hii (HGA) kusema kuwa itatumia sheria za Tanzania haielezi iwapo sasa zitatumika mahakama na mabaraza ya ndani ya Tanzania katika utatuzi wa migogoro.

3.Rais anasema mkataba huu ni matokeo ya IGA ,Mwingine anasema mikataba hii ni matokeo ya Public Private Partnership.Kama mikataba hii ni matokeo ya PPA kwanini mulipeleka Azimio na Mkataba wa IGA kuridhiwa na Bunge? Kama ni PPA kwanini muweke exclusive clause? Kwanini mgeni amiliki asilimia 40? Je sheria Na.5 na No 6 za mwaka 2017 zinasemaje kuhusu umiliki wa Raslimali za Asili ?

4.Wametuambia kwamba eti tutamiliki kwa ubia wa asilimia 60 kwa Serikali na Asilimia 40 kwa DPW...Hiyo Asilimia 60 ni yaserikali ipi ya Muungano au Tanganyika?

5. Je Zanzibar itapata mgawo kwenye mapato ya bandari ya Tanganyika? Je katika hiyo asilimia 60 kuna viongozi wa Zanzibar wataingizwa kwenye usimamizi wa Bandari za Tanganyika ambazo siyo za muungano?

6. Je hawa wenzetu wametuambia na kutufafanulia ili kupata hiyo asilimia 40 DPW kawekeza kiasi gani na katika maeneo yepi? Kwanini hamjaweka feasibility study wazi kwa Umma ili umma ujue badala yake mkafanya siri na kuitana kwa faragha kana kwamba nchi hii ni shamba lenu binafsi?

7.Je kama HGA ni ya miaka 30 Inter Governmental Agreement (IGA) ni ya miaka mingapi?

Muhimu kujua:

1 .Mbuzi hawezi kuzaa Tembo.IGA ni haramu inapoka Mali asili za watanganyika na kuziweka kwenye mikono ya watu wa chache kwa njia ya ujanja ujanja.

2.Hitaji letu ni IGA ifutwe na kama kuna uwekezaji unafanyika lazima uzingatie maslahi ya Umma na siyo ya viongozi wa ccm na familia zao kwa kuhakikisha

@ Bandari za Tanganyika zinamilikiwa na Umma kama sheria zinavyotaka

@. Kama ni uwekezaji lazima uwe wa mfumo unaotoa nafasi na fursa kwa watanganyika na kampuni za kitanzania kumiliki sehemu kupitia hisa badala ya Kampuni moja ya kigeni kupewa asilimia 40?

WEKENI HUO MKATABA WA HGA WAZI ILI TUUONE NI MATAKWA YA KISHERIA.

BAK MWABUKUSI
SHAMBANI BUSOKELO.
BAK Mwabukusi 😂😂
 
Ni kauli za kijinga Sana, yeye anaona mkataba Ni mzuri kwa akili ndogo alizonazo, hivi Tanzania mtu kuonekana kwenye TV anaona ana akili Sana na ujanja kuliko watu wengine wasomi na waelewa wa mambo kumbe hajui wengine wapo hapo kulinda vibarua vyao umri umeshawatupa mkono ya nini kulumbana, tasania ya maigizo kwa nini hakuna walioenda shule wengi Ni waganga njaa wapiga majungu etc
Wakati mwingine wasomi tunafanya blunders kiasi cha kutaka hata kuidhalilisha Nchi, yetu na hata nchi zza wawekezaji, the same thing you are doing it here right now
Subiri bajeti ya 2024/2025 uone kitakachoptaikana kutoka Bandarini. Haipo nchi duniani ambayo Bunge na Serikali viliwahi kushirikiana kuuza nchi, hajiajwahi kutokea
 
Wanajinasibu kuwa na mikataba mizuri ya utekelezaji wakati IGA ya kikanjanja inayolinda hiyo mikataba ya utekelezaji ipo palepale, tutaishia kupigwa na kitu kizito kama ile bil. 75 tuliyopigwa hapa majuzi....
 
Back
Top Bottom