Msaada: Huyu ni nyoka wa aina gani?

Msaada: Huyu ni nyoka wa aina gani?

Kama ni Morogoro basi atakuwa ni BROWN HOUSE SNAKE ambao wanapenda sana kukaa kwenye makazi ya watu wakila panya, mijusi. Ni nyoka wasio na sumu na ni completely harmless to humans.View attachment 2953250 wanapatikana kwa wingi sana Morogoro mjini.
Nadhani nimekusaidia mkuu
Kumbe naweza kumfuga kwa ajili ya panya kama paka
 
umejuaje ni black mamba na ili hali hujaangalia ndani ha mdomo wake ??
Unamuona tu kwa rangi yake ya juu..japo wapo wachache mnooo wanafanana na Black mamba...watu tumeishi mazingira ya nyoka
 
Watumie hiyo picha wale wa South Africa wa kipindi National Geographic Channel kinaitwa snake in the city kama sijakosea...ila watasikitika sana kuona umemuua maana wao huwa hawauii.
 
Kumbe naweza kumfuga kwa ajili ya panya kama paka
Yes inawezekana kabisa na akakua mkubwa kama 3m cha msingi asiwe anatoka tu nje maana watu wakimuona wataanza kukuhusisha na imani zingine au wakakuulia mifugo wako pendwa😀
 
Watumie hiyo picha wale wa South Africa wa kipindi National Geographic Channel kinaitwa snake in the city kama sijakosea...ila watasikitika sana kuona umemuua maana wao huwa hawauii.
Yeah yule jamaa na mke wake watapandwa na jazba na kujiuliza ni jamii gani hii haijali haki za kuishi kwa wanyama wengine?😀
 
Sio kweli kuna nyoka wengi sana wana rangi hiyo na sio black mamba
Black mamba anaweza kujulikana kwa rangi nyeusi ilyokolea ndani ya mdomo wake pale anapofoka au akisimama wima kwa 3/4 ya mwili wake vinginevyo ni rahisi kumchanganya na aina nyingine ya nyoka kwa rangi yake.
 
Nyoka hana shida kama hujamchokoza

Peace,

Wakuu jirani yangu amekua ananiambia hua anamwoma nyoka mkubwa nyakati za jioni akikatiza katika uzio wake. (Uzio unaotutenganisha) awali nilidhani ananitania maana manawake huwa waoga waoga tu akiona kijiti anaweza kusema nyoka au pia utani na masikhara

Lakini kwa umri wake sio mtu wa utani (mama mtu mzima) aliponiambia mara ya pili na ya tatu nikaanza kua makini. Sasa leo jioni hii upande wa pili na kule anakoniambia nimekutana na huyu nyoka nikamuua.

Nilipomuita aje kumtazama akasema nyoka anayemuonaga ni kama huyu kwa muonekano ila mkubwa zaidi, akasema ni kama mara 3 kwa unene na urefu hana uhakika maana hua hamuoni mwanzo mpaka mwisho wake.

Wakuu hapa naona sasa nahitaji kukaa mguu sawa maana ni kama kuna kambi ya hawa viumbe maeneo haya tuna share oxygen pamoja. Huyu niliyemuua anaweza kuwa mtoto wa huyo anaeonekana. Hapa kutakua na kiota.

Wakati najipanga kuwakabili hawa wajomba naomba aliye na ufahamu wa aina za nyoka anifahamishe huyu ni aina gani ya nyoka na tabia zake na je natakiwa kukabiliana nao katika mtindo upi.

(Najua utaratibu wa kuwataarifu mamlaka ya maliasiri lakini wote tunaifahamu nchi yetu kama ghorofa la Kishimba lilipoungua wakataarifiwa jeshi la zima moto sio tu walikuja siku iliyofuata yani walifika baada ya masaa 32 ila pia walikuja na gari halina maji, unaweza ukapata picha kuwategemea mamlaka za serikali ilivyo riskView attachment 2953224

Update: Nimelazimika kuihamisha familia (mke, watowo watatu na dada wa kazi) hapa nitabaki mwenyewe mpaka vita na hawa viumbe itakapofika tamati, maana kuna kila dalili huu mziki utakua bab kubwa. Hapa kutakua na kiota
Huyu nyoka hana shida kama hujamchokoza huonekana majira ya mchana pekee, nimepishana nao katika harakati za kilimo huko Kimashuku, kwa jina simjui.
 
Huyu nyoka hana shida kama hujamchokoza huonekana majira ya mchana pekee, nimepishana nao katika harakati za kilimo huko Kimashuku, kwa jina simjui.
Anaitwa brown house snake mkuu. She is completely harmless to humans
 
Yes inawezekana kabisa na akakua mkubwa kama 3m cha msingi asiwe anatoka tu nje maana watu wakimuona wataanza kukuhusisha na imani zingine au wakakuulia mifugo wako pendwa😀
Nyumbani wageni hawatakanyaga 🤣
 
Nyumbani wageni hawatakanyaga 🤣
Wakija unamwambja nyoka wako, ingia chini ya uvungu na usitoke🤣
Kimbembe wageni wanakula mezani alafu akajitokeza na kumpandia mmoja wapo mguuni maana kwa asili nyoka wanavutiwa na harufu nzuri nzuri kama za vyakula especially harufu ya wali. Sipati picha huyo mgeni atakavyoibwaga hiyo dinning table na vyakula vyote chini kwa kihoro🤣🤣🙌
 
Kuna dawa inauzwa katika maduka ya pembejeo za kilimo ni ya nyoka na wadudu unapulizia tu hiyo kwisha kazi
 
Daah wee jamaa nyama nyeupe io proten pure, uyoo mama nyokaa ukimuuaa wahi kumweka kwenye fridge Afu nifwate pm
 
Back
Top Bottom