Msaada: Jirani yangu ni mbabe na msumbufu

Msaada: Jirani yangu ni mbabe na msumbufu

Ushawahi kusikia story mpaka unajiuliza huyu anayesemwa ni mimi au ni mwingine?😂🤸 Leo nimecheka sanaa

Ipi sweetheart?

Ya mleta mada au ya hawa wanaochombeza na stori ya kuchinja kuku?

Au wewe ndio aina ya jirani mtata 😁?
 
Kama mjuavyo, viwanja ambavyo havijapimwa huwa havina barabara, hivyo ili kupata njia, inabidi busara zitumike. Mimi, kwa kiherehere changu, nikamega sehemu kidogo ya kiwanja changu kwa mbele ili kupata barabara ya kupita gari na watu wa nyuma yangu waweze kuitumia.

Jirani niliyepakana naye upande wa pili wa hiyo barabara niliyotoa ndiye pasua kichwa. Kwa sasa anasema yeye ndiye aliyetoa barabara na ni sehemu ya eneo lake, hivyo ninapaswa kurudi nyuma hatua moja na nusu.

Nikaamua kuweka ukuta kuepusha mgogoro naye, lakini bado anataka ukuta wangu uvunjwe. Anadai nimejenga barabarani. Wenyeviti wote wapo upande wake, wakidai nimejenga barabarani. Ninapowaambia kuwa barabara ni sehemu ya eneo langu na jirani ndiye anayepaswa kurudi hatua kadhaa nyuma ili barabara iwe pana, hawanielewi na wamenikomalia. Jirani ana lugha isiyofaa, si mstaarabu, anatumia nguvu na mabavu ili nivunje ukuta.

Nimewaza kufunga kabisa hiyo barabara, ila nawaza majirani wa nyuma yangu watapita wapi. Naomba mnisaidie namna ya kushughulika na mtu wa namna hii maana wenyeviti wote wapo upande wake, nahisi wamepewa mlungula ili waikandamize haki yangu. Nimewaambia sitaki usumbufu na sijajenga ukuta kwenye eneo la mtu.
Wakati unatoa hiyo barabara nani alikuona?? Inawezekanaje jamii nzima isikuelewe ww imsikilize yeye?? Acha janjajanja
 
Kama mjuavyo, viwanja ambavyo havijapimwa huwa havina barabara, hivyo ili kupata njia, inabidi busara zitumike. Mimi, kwa kiherehere changu, nikamega sehemu kidogo ya kiwanja changu kwa mbele ili kupata barabara ya kupita gari na watu wa nyuma yangu waweze kuitumia.

Jirani niliyepakana naye upande wa pili wa hiyo barabara niliyotoa ndiye pasua kichwa. Kwa sasa anasema yeye ndiye aliyetoa barabara na ni sehemu ya eneo lake, hivyo ninapaswa kurudi nyuma hatua moja na nusu.

Nikaamua kuweka ukuta kuepusha mgogoro naye, lakini bado anataka ukuta wangu uvunjwe. Anadai nimejenga barabarani. Wenyeviti wote wapo upande wake, wakidai nimejenga barabarani. Ninapowaambia kuwa barabara ni sehemu ya eneo langu na jirani ndiye anayepaswa kurudi hatua kadhaa nyuma ili barabara iwe pana, hawanielewi na wamenikomalia. Jirani ana lugha isiyofaa, si mstaarabu, anatumia nguvu na mabavu ili nivunje ukuta.

Nimewaza kufunga kabisa hiyo barabara, ila nawaza majirani wa nyuma yangu watapita wapi. Naomba mnisaidie namna ya kushughulika na mtu wa namna hii maana wenyeviti wote wapo upande wake, nahisi wamepewa mlungula ili waikandamize haki yangu. Nimewaambia sitaki usumbufu na sijajenga ukuta kwenye eneo la mtu.
Ishi na majirani zako vizuri. Acheni ugomvi, Duniani tunapita tu, kila kitu tutakiacha.


JESUS IS LORD&SAVIOR
 
Unadhani ni jambo rahisi sana hvyo ee
kupata tu sahini ili wakala waARDHI akupimie nakukuwekea JIWE ni mbinde
Watanzania haswa watu wa bara ni watu wa hovyo sana
Kipind unatafuta kiwanja hapo kabla ya kununua lazima ujuane na majirani kwanza.
 
Rudi nyuma tu mimi nilikuta jamaa wa nyumba za mbele wana tatizo kama hilo uzuri wa karibu yangu ni muelewa tukarudi hatua za kutosha kwenye bara bara na kwenye ukuta hata gari kupaki hatusumbuki wao wamebana na nafasi wanayo wanasumbuka kuingiza gari kubwa mpaka unashangaa Ardhi hii watu wanasumbuka nayo sijui kwa kitu gani?labda uwe na eneo dogo kama una eneo la kutosha Ardhi isiwe sehemu ya migogoro kabisaa na wengine kutokana na kuhangaika kupata pesa ya Ardhi kwa muda mrefu anaweza kukuroga mkigombea Udongo...
 
Kiwanja ulinunua? basi aliyekuuzia ndo shahidi yako namba moja.....nenda kata
 
😂🤣

Basi wacha uteseke, umeamua kuwa swala lazima uishi kwa tabu na hofu ya kukamatwa kila saa.
🤣🤣🤣🤣🤣acha tu niwe swala
Unajua nitakapofanya hivyo hatokubali kuendelea kuona hivyo vimbwanga kwenye eneo lake lazima atakimbilia kwa sangoma🤣🤣🤣🤣
 
Inakuaje watu mnakuwa wapole wapole hivi!! Kuna mambo hayahitaji diplomasia nguvu lazima itumike, kuna jirani yangu alimega hatua 5 za kiwanja changu akajenga ukuta,mimi nilichofanya nikavuja ukuta nikaweka waya mchezo ukaisha
Huyo hakuwa mkorofi alikujaribu tu lasivyo angekupandisha kizimbani kwa kuvunja ukuta wake
 
Huyo hakuwa mkorofi alikujaribu tu lasivyo angekupandisha kizimbani kwa kuvunja ukuta wake
Ukuta ukiwa ndani ya eneo lako sio wake tena.
Kuna wajinga walijenga eneo lao lote halafu hamna barabara nikamega kiwanja changu ikawa barabara nzuri. Eti wakaanza kujenga fremu nikawaambia marufuku kujenga fremu hilo ni eneo langu mkijenga tu nazungushia ukuta. Hadi leo hakuna aliethubutu.
 
Back
Top Bottom