Msaada kwa wenye kufahamu kuhusu malipo ya Serikali

Msaada kwa wenye kufahamu kuhusu malipo ya Serikali

Hili lina ugumu wake na nina uhakika kama ni kulipa moja kwa moja itachukua muda kuliko hata ilivyo sasa. Tafuta watumishi wanaolipwa malimbikizo ya mishahara ndipo utaelewa.

Kwa uzoefu wangu kwenye suala la kuwalipa waajiriwa wapya hasa wanaolipwa kwa pesa kutoka serikali kuu hakuna ukiritimba kwenye halmashauri isipokuwa ni taratibu za zilizowekwa na serikali yenyewe ambapo halmashauri haiwezi zikwepa wala kuzipindisha. Akipindisha ndiyo utasikia amekiuka taratibu, n.k.

Wanaolipwa kwa makusanyo ya halmashauri hapo ndipo kuna changamoto na mara nyingi makusanyo kama hayako sawa na si mfuatiliaji utasumbuka sana. Hata huko kwenye mashirika na mamlaka taratibu ni hizo hizo isipokuwa wao chain yao ni fupi sana na uhakika wa fedha upo kwa 100% kama siyo 99%.
Nimekuelewa sana mkuu kwenye michango yako ya huko juu. Japo hapa kwetu wamefikia hapo BOT ndo ikaleta zengwe. So na imani zitaingia tu ngoja tuwapange tu hawa wadeni wetu.
 
Inawezekana kweli kuna shida BOT Kwa wiki au zaidi kuwa mvumilivu
 
Kwa maoni ya wadau suala hili nimelielewa...ngoja tuvumilie
 
Inawezekana wewe ndiye mtu wa hovyo sana kwa kushindwa kuelewa maelezo!
Maelezo nimeyaelewa sana ila hapa ileje ndugu njoo ujionee...wenyeji wakishakujua wewe ni mgeni hakuna rangi utaacha kuona. Vitu na mahitaji bei inapanda Mara dufu. Niko chilemba humu ndani ndani. Labda huko itumba na isongole kuna kauafadhali.
 
Maelezo nimeyaelewa sana ila hapa ileje ndugu njoo ujionee...wenyeji wakishakujua wewe ni mgeni hakuna rangi utaacha kuona. Vitu na mahitaji bei inapanda Mara dufu. Niko chilemba humu ndani ndani. Labda huko itumba na isongole kuna kauafadhali.
Hali hiyo si Ileje peke yake, ni po pote Tanzania! Watanzania tumekuwa watu wa kupenda utapeli na kuvuna usichopanda.
 
Ila mbona halmashauri kama ya tunduma wameshapewa. Hii huwa imekaaje? Sisi walikuwa wanatwambia tutapewa then wakaanza kuleta habari kuwa malipo yetu yako tayari shida sasa iko BOT.
Wewe bado mgeni sana halmashauri aisee! Ngoja nikuongezee mfano mwingine..

Kuna ziara ya rais au waziri anakuja kitembelea kituo cha afya, na ujenzi hauja kamilika kwasababu pesa hakuna ila ded anaona kuna kifungu cha malipo yenu kina 10milion na zinatakiwa 10mil ili kukamilisha ujenzi!

Je wewe ungekua ded ungelipa watumishi posho alafu rais akija utumbuliwe au utapeleka kwenye kituo cha afya ili usitumbuliwe?

NB: jiweke nafasi ya ded ndio ujibu.
 
Nimeajiriwa 2012
Mpaka leo huwa nadai hela yangu ya kujimu na nauli.
Juzi nikandika barua ya kukumbushia juu ya deni langu wakaniambia "Kwa madai ya nauli leta tiketi" nikaona isiwe tabu nika comment "Lipeni tu ya kujikimu" ila mpaka leo sijapata.

#YNWA
🥲Haki za wanyonge haziendi bure kwa hakika kuna haja ya kuwa na siku ya hukumu ili kila mtu apate haki yake


Viongozi mnaopewa madaraka msidhulumu haki za watu hii ni mbaya inatengeza jamii yenye chuki na viongozi
 
Ni kweli mfumo unasumbua wa BOT , Pia ujue hamna hela itakayopitishwa zaidi mshahara kwa tarehe hizi, Kila Hela inapigwa zuio kuelekea tarehe za mishahara....hii ni kawaida sana.

Mimi ni Internal Auditor wa halmashauri Fulani Kenya...au Tanzania.Uliza chochote nikujibu,

Malipo ya kielektroniki ni changamoto, mfumo umeshatengemaa sasa kuruhusu malipo ya hawa watu?
 
Malipo ya kielektroniki ni changamoto, mfumo umeshatengemaa sasa kuruhusu malipo ya hawa watu?
Kwa kuwa mishahara imeanza kutoka naamin wakifuatilia within two weeks watakuwa wamelipwa specifically watu wa afya!
 
Back
Top Bottom