Msaada: Mwanamke anataka kuachwa, ana mimba na ashatolewa mahari

Msaada: Mwanamke anataka kuachwa, ana mimba na ashatolewa mahari

SuperHb

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2016
Posts
911
Reaction score
751
Rejea hapo juu....naomba niende kwenye mada husika..

Nina mdogo wangu alimtambulisha binti nyumbani kwa wazazi wetu, wazazi wakambariki baada ya hapo binti aliendelea kuishi kwao

Kwa bahati mbaya au nzuri binti alipata Ujauzito ,ikabidi binti atoroke aje kwa mwanaume ili Nyumbani wasigundue kama kapata mimba

Basi mwanamke alihamia kwa mwanaume na taratibu za kwenda kuongea nyumbani kwa binti zikafuata. Nyumbani kwa binti wakasema wasubiri watapewa majibu, kwa ngoja wawasiliane na wazazi wao husika walioko mkoa mwingine, maana binti alilelewa na Bibi yake.

SASA TATIZO LILIPO...
Sasa Baada ya mwanaume ambaye ni mdogo wangu baada ya kukaa na binti kwa miezi miwili anataka amfukuze Hamtaki tena, na isitoshe binti mwenyewe ana mimba, anasema hana mapenzi nae, yupo anayempenda rohoni kwamba huyu ilikuwa bahati mbaya...

Kwahyo huyu mdogo wangu ameenda kwa wazazi akawaambia hamtaki anataka amfukuze binti hana mapenzi nae tena. Sasa kesho nimeitwa kwenye kikao Mimi, mdogo wangu ambaye ni mhusika pamoja na Wazazi kwa ajili ya kulijadili hili.

KWA KUKUMBUSHIA...
Huyu dogo anaye binti ambaye yuko naye katika mahusiano tangu nyuma sema wametengana kama miaka miwili hivi binti alienda kimasomo, ila bado wanawasiliana vizuri mpaka sasa hivi. HUYO NDO ANAYEMPENDA KUTOKA MOYONI MWAKE NDO ANATAKA AMUOE

NAOMBENI USHAURI NINI CHA KUFANYA NDUGU ZANGU
 
Ndoa ni mapatano, mapenzi hayalazimishwi. Hapo cha kufanya ni hichi.
1. Maamuzi ya dogo lazima yaheshimiwe.
2. Ndugu ombeni radhi kwa kuwasumbua wazee wa binti.
3. Kijana aachwe akapambane na hali yake, iwe kuoa mwingine, kutunza mimba aliyompachika binti wa watu nk.
 
SuperHb Hakuna solution hapo, familia yenu ichukue jukumu la kumlea huyo Mtoto na Mdogo wako asilazimishwe kumuoa!

Wameshaishi na kaona madhaifu yake au karazaa zake, haya ndo madhara ya kulana kabla ya ndoa, angekuwa Ana ndoa asingethubutu kusema hayo ma ujinga!

Mwambie Dogo tu ni ngumu yeye kuishi kwa Furaha Kama ataamua kuyafanya hayo, maana atakuwa atendi haki kabisa! Sio uungwana, anajiletea Lana!
 
Ndoa ni mapatano, mapenzi hayalazimishwi. Hapo cha kufanya ni hichi.
1. Maamuzi ya dogo lazima yaheshimiwe.
2. Ndugu ombeni radhi kwa kuwasumbua wazee wa binti.
3. Kijana aachwe akapambane na hali yake, iwe kuoa mwingine, kutunza mimba aliyompachika binti wa watu nk.
Kijana alipe faini ya kudyeha Mabele yaani kuangusha chuchu za binti wa wenyewe kwa kumtia Mimba.

Kijana aweke wazi mpango wake wa kuendelea kuhudumia ujauzito.

Kijana aweke wazi mpango wake kuhusu kijacho.

Mkiridhika na haya itapendeza mkiheshimu mapendekezo yake na mumpe Uhuru apambane na Hali yake.
 
dogo anayetaka mwenyew kuoa ndo alianza naye mahusiano....ila binti alienda mkoa mwingine kwa ajili ya masomo,,,sasa huyu anayeishi nae mwenye mimba ni wa after,,,ambaye anasema hamtaki,hana hisia nae japo ashajitambulisha kwa wazazi wa binti
 
Kijana alipe faini ya kudyeha Mabele yaani kuangusha chuchu za binti wa wenyewe kwa kumtia Mimba.

Kijana aweke wazi mpango wake wa kuendelea kuhudumia ujauzito.

Kijana aweke wazi mpango wake kuhusu kijacho.

Mkiridhika na haya itapendeza mkiheshimu mapendekezo yake na mumpe Uhuru apambane na Hali yake.
anataka mimba itolewe....Lakini yule binti wa Aliyenzisha ne mahusiano wa mwanzo...alisema yuko tyari waoelewe wote wawili...na ikitokea haiwezekani basi yuk tihari yule binti wa pili akishajifungua amfukuze...mtoto atamlea kwa roho nyeupe,kwa niaba yake
 
SuperHb Simple sana, chukua fimbo charaza viboko vya maana! Niliwahi kuambiwa kule Upareni unapokua na vitabia vya kishetani hivi wazee waanakupitisha kwenye Tanuru lina wazeee wamejipanga na bakora za kutosha.

Huu ni ujinga, uwendawazimu na kukosa dira ya maisha kama Kijana, tatizo katakua kametahiriwa hospital kwa ganzi. Pumbavu zake
 
Back
Top Bottom