Msaada mwenye connection ya ajira nchi za Kiarabu

kazi gani unataka uarabuni?njoo inbox nikupe mchongo wa kazi Dubai International Airport ni semi skilled job(Airport cleaner,na Airport porter
 
Niunganishe kaka...kama kuna mtu unamjua...ata na uyo ndugu yako...nizungumze nae...pengine nipata pa kuanzia...sikufichi ata hapa tz nafanya kazi ya ulinzi...sasa nimesikia kidogo huko kwenye nchi za kiarabu kidogo mshahala upo juu...
Upo kampuni gani hapa nyumbani?wanapolipa huo mshahara
 
Unachosema kuhusu hao Agents kuwepo Kenya ná Uganda ni kweli kabisa. Wakenya wako wengi sana Qatar na Dubai. Nilishangaa sana sikupata nafasi ya kukutana na mbongo hata mmoja. Basi nikawauliza inakuwaje wako wengi sana kule wanapataje kazi? Ndiyo wakanijibu kwamba nchini mwao kuna maagents ambao wameingia mikataba na waajiri au maagents wa huko kwa hiyo wao wanafanya taratibu zote za ajira na wakiridhika na mtu kwa ajira zilizotangzwa kule na waajiri au maagents basi wanafuata taratibu zote za kuingia nchi hizo kihalali ili mhusika akishafika kule na kukamilisha taratibu zote za kuingia anaanza kazi mara moja. Sidhani kama hao maagents wa Kenya na Uganda watakubali kumsaidia Mtanzania.
 
awawezi kabisa...kwasababu watanzania walio wahi kwenda huko wale wa mwanzo hawakuwa na moyo wa uvumilivu tofauti na wakenya ama waganda ama kutoka mataifa mengine...kwakifupi watanzania atuaminiki...nimefanya mawasiliano na maagent wote hao na bila kupepesa maneno wamenijibu majibu yanayo fanana...hadi nguvu ziliniisha ivi sasa nia yangu ni kupambana kupata njia ili nitengeneze njia kwa wengine wenye nia ya dhati ya kufanya kazi
 
napambana nifike huko
boss nisaidie kama unao uwezo maji yamezidi unga kiongozi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…