Msaada: Naomba kupewa gharama za hatua hizi za ujenzi

Nimechelewa kuuona uzi, pia ungeweza kuichana 2*6 ukapata 2*2 tatu. Mfano kama ulikua unahitaji 2*2 30, basi kwa 2*6 kumi tu zingetosha hitaji lako

Sent using Jamii Forums mobile app
Thanks sana boss nitafanya hivyo ujenzi mwingine maisha ni nyumba nimejenga hii so nina uzoefu wa vitu vingi sana, nimejaribu kupiga hatua japo, ila nimefurahi kwa mawazo yako nitakucheki PM tuzidi kuwasiliana kwaajili ya ushauri wa hapa na pale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hebu njoo boss unipe makadirio ya kupiga skimming
 
May mwaka jana nilifanya vitu vichache vikabaki vitu kama skimming, tiles na Rangi,... Hebu nipe makadirio gharama za fundi za kufanya skimming
 
May mwaka jana nilifanya vitu vichache vikabaki vitu kama skimming, tiles na Rangi,... Hebu nipe makadirio gharama za fundi za kufanya skimming
mdogo mdogo siyo tutumie picha
 
Nipo kibaha
 
May mwaka jana nilifanya vitu vichache vikabaki vitu kama skimming, tiles na Rangi,... Hebu nipe makadirio gharama za fundi za kufanya skimming
mkoani skimming kuna fundi alifanya nyumba ya vyumba vitatu 150,000
 
Hebu njoo boss unipe makadirio ya kupiga skimming
nyumba ya vyumba vinne

mifuko 5 ya gypsum powder@25,000
white enamel ndoo 3-4@35,000
white cement mfuko 1-2 @35,000

ufundi
skimming 200,000

Rangi nje
white enamel ndoo 1 na nusu@35,000
binder ndoo 1@90,000
weatherguard ndoo 1 na nusu@140,000 +75,000
rangi ya fishabodi kopo2 za lita4@16,000
rangi ya grill kopo 2 za lita4@16,000

Rangi ndani
white enamel ndoo 3@35,000
primer ndoo 2 @ sikumbuki bei
silk ndoo 2 @140,000

Ufundi laki 350,000

N.b: Huyo ni fundi wa mkoani mkuu ndio alinifanyia mimi nyumba vyumba 4
na hizo bei za rangi ni huku mkoani mkuu nyie wa dar mna bei zenu
 
Jina lako linakusadifu maana sio kwa kumkatisha tamaa mwenzio duh....
Mm yangu nliiwekea mil9 nihamie kumbe nlikuwa nawaza kitoto. Saiz ina mil30 haijaisha na nlihamia ikiwa na 15mil, ikiwa haina lipu, sakafu,blandaring, wala umeme nliweka solar but akat naingia hata solar sikuwa nayo
 
Kuna jamaa yangu mi nilimuona boya eti alikuwa ananipiga majungu kwa wana sababu nimenunua gari tena kwa kuagiza badala ya kufanya finishing kwanza!!! Nilimjibu tu kiustaarabu nimejenga nyumba yangu mpaka kupaua bila kupumzika so finishing ntaifanya bila pressure mdogo mdogo tu na sait navisit na mkoko wangu. Shubaamit
 
Ushauri wangu mimi No Escape....Usiamini fundi yeyote,Mwite fundi elewana nae kazi moja akimaliza mpe pesa yake angalia kama amekuridhisha mpe kazi nyingine. Kwa hapo unaweza kuanza na;
Blundering
Wiring
Plasta
Alluminium,kama pesa inatosha unamalizia Tiles..Sikiliza ushauri wa mafundi ila changanya na akili zako mara nyingi huwa wanashauri sehemu ambazo wanaweza kupata pesa nyingi wanaweza kukushauri uanze na Tiles kabla kuwa makini.Nakutakia ujenzi mwema

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…