Msaada: Nilipata ajali mkono wa kulia haufanyi kazi japo nafeel

Mnyakyusa Ipinda

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2020
Posts
439
Reaction score
1,526
Wakuu habari, kama mmeona sikuwa active hapa online, hata kwenye simu kwa wale mliokuwa na my contacts since March.

Nitaelezea one day ilikuaje but kwa wale mnaofatilia habari mtakuwa mliona this year March ilitokea ajali mbaya sana ya treni ya Tazara, mtu aliyegongwa it was me, na nilikuwa nimeshuka tu kwenye bajaji niongee na simu kumbe niko relini.

Anyway tuyaache hayo nitaelezea next time. Sasa kuna jambo nataka mnisaidie ushauri au tiba, najua humu kuna madr bingwa pia, mkono wangu wa kulia, nilipopona mwezi wa 6 nimerudi home nikagundua mkono mmoja haufunction, nikajua maybe cas naumwa utakaa, sawa after sometime, but haukukaa sawa na ukanikunja, siwezi hata kushika kitu cas hata vidole havifanyi kazi, hospital wamecheki nmefanyiwa MRI, wameona tatizo ni moja tu, mishipa ya fahamu kwenye mikono ndio inashida, niko hospital nmechoka wacha nilale tamalizia kesho, i need help.

Namalizia sasa

Wanecheck MRI report mifupa yote iko sawa na mazoezi tu takaa sawa, but wameona tatizo ni mishipa ya fahamu inayopita mkononi ndio inashida haipeleki taarifa kwenye ubongo that why vidole havifunction, na tatizo ni kwenye shingo mifupa ya shingo imeibana hiyo mishipa ya fahamu ya right hand ndo mana taarifa hazifiki kichwani na wanakutena leo jopp la madaktari wadiscuss hiyo report na wadecide kana ni operation au wafanye niu cas wanasema issue zinazohusisha nerves za fahamu ni delicate kidogo, huitaji umakini mkubwa.

Kwenu wana JF, najua madoctor mmo humu, tatizo hili linaweza tibika? Sababu nimechoka wakuu, nimekaa hospital since March seriously.

Pia kama kuna tiba hata huko mitaani za mifupa cas haina shida mifupa nahitaji tu mazoezi but jana naweza pata hata dawa nzuri na kuchua na mazoezi tafarijika sana, najua kuna watu nnje huko wanaweza kusolve hata hili la mishipa ya mkononi na mkono uanze kufunctiion, nisaidieni wakuu, ushauri wowote napokea, yani mda huu mi wakuogeshwa kweli? Dah help me.

Ngoja nione madr watasmua nini tawapa mrejesho, please maombi yenu ni muhimu, sijawahi dhani naweza fkia hali hii one day, its so sad😥
 
After sometime utarudi kuwa sawa. Kuna huduma ya kuupiga shots za umeme ila siyo ule wa tanesco. Na ukipata nafasi unaufanyisha mazoezi baada ya miezi kadhaa utakua poa
Asante mkuu, naomba Mungu nirudi kuwa sawa, mazoezi nafanyiwa isipokuwa huu mkono wa kulia haufanyi chochote hata vidole havifanyi kitu, hivyo ni kazi sana, imagine naogeshwa cas siwezi jiogesha, dah is painful kiukweli, nipone tu
 



1. Eka fikra sawa kwamba utapona.
2. Kuwa active kuusumbua.
3. Do not rekax na kukubali umelemaa
4. Pata ushauri wa wataalam.

Naamini utakua sawa.
 
Pole sana nashauri tafuta bingwa wa mishipa atakushauri vema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…