Msaada: Nimefikia hatua ya kunywa Pepsi 4 kwa siku, nifanyeje kuacha?

Ila twende mbele turud nyuma kapeps nikatam aah Tena iwe ya barid wee burudan sana

Ila sijawah zidisha hata mbil Kwa siku na kunywa ni mara chache sana Mzee wangu kimemkuta jambo magoti yalianza kugoma kufanya kazi
 
Hamna namna zaidi ya kuamua kuacha maana madhara ni mengi kuliko faida.

Ila sikulaumu maaana Dec nilikunywa Pepsi mbeya Ina ladha tofauti na hizi za daslam sijui ww unakunywa ukiwa wapi
 
Pole kwa kuwa mhanga wa kunywa soda nyingi ndani ya siku moja hata mimi nimetoea huko,nakupa ufumbuzi wa Hilo tatizo kwenye DM yako.
Nipe dakika ishirini.
 
Tafadhali punguza sana la sivyo utakaribisha kisukari.
 
Pepsi nne kwa siku ni afadhali unywe bia 5
 
Pepsi nayo ina ulevii flaniii.. Coka wanaisingizia tuu.
 
Kwani unakoishi hakuna maji na hujui faida ya kunywa maji na hasara za kujitutika misukari feki? Uamuzi ni wako. Endelea ufe au acha uishi mwanangu. Simpo.
 
Pepsi nne kwa siku siyo nying, usiogope; wenzio wanakunywa Safari Lager zaidi ya 15 kwa masaa matano tu ya usiku.
 

Soda za Pepsi na Coca kwa sasa zinawekwa kahawa. Kahawa ina nafasi ya kwenda kusisimua ubongo kupitia sehemu ya furaha kwenye ubongo.

Kwa kadri unavyoendelea kutumia kwa wingi ndivyo unavyofanya sehemu husika kuitegemea kahawa ili mwili kuwa wenye uwezo kutimiza majukumu yake.

Pia, kwa upande mwingime, matumizi haya yanaweza kuwana matokeo ya ukosefu wa madini au vitamini mwilini. Kama inavyotokea kwa watu kula mkaa, udongo au barafu. Hivyo tathmini nzuri inahitajika kufanyika pia kwa upande huo.

Kumbuka:
Kahawa : Huweza kukufanya uwe macho mda mrefu na mwenye nguvu, ila inaweza kukufanya pia kuwa mtu mwenye wasiwasi, usingizi usiotosheleza/mang'amung'amu au usipate kabisa nk.

Matokeo yake ni:
1: Utegemezi kwenye chanzo cha kahawa.

2: Mapigo ya moyo kwenda mbio. Kunakuwa na hatari ya kupata mapigo ya moyo yasiyoendana na hali yake ya kawaida. Ugonjwa wa moyo unaweza kuanzia hapo.

3: Kuwa na kiasi kikubwa cha sukari mwilini, na pale kongosho litakapochoka/litakaposhindwa kutoa kiasi hitajika cha homoni ya insulini utakuwa na tatizo la kisukari.

4: Kuongezeka uzito.

5: Kuongezeka mafuta kwa wingi mwilini.

6: Tatizo la mishipa ya fahamu.

7: Tatizo la figo.

8: Tatizo la macho.

9: Unaweza kujikuta kuwa mtu mwenye wasiwasi uliopitiliza au hata msongo wa mawazo kwa mambo yako kubadilika au kutokwenda vyema.

Nini kifanyike?
1: Jitambue kuwa hali hii si njema kwa mustakabali wa afya yako na maisja kwa ujumla.

2: Fika kituo cha afya kupata vipimo na ushauri.

3: Anza zoezi la kupunguza kiasi na si kuacha mara moja. Unaweza kujipa muda wa kupunguza kiasi cha soda 2 kwa wiki na baada ya hapo unapunguza tena na mwisho kuacha mazoea ya matumizi husika.

4: Tafuta kitu mbadala ya soda ambacho hakitakuwa na athari ya moja kwa moja kama: kupata matunda na maji ya kutosha au mlo kamili.
 
Endapo utaongeza zaidi kiwanda chetu kitakuzawadia.
 

Tumia tu akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…