Habarini za mchana,
Wakuu mimi huwa situmii pombe, ni juice na soda tu na soda yangu pendwa ni Pepsi.
Kila siku huwa nakunywa Pepsi tena napenda ikiwa baridi sana. Nilianza kunywa moja kwa siku, ikaja mbili ikaja 3 now nakunywa nne kwa siku; mbili mchana na mbili usiku. Hizo mbili nakunywa kwa mpigo.
Nifanyeje ili kuacha? Pia Mimi sio mpenz wa chai asubuhi, niko radhi nile vitafunwa vikavu au na maji au soda, na usiku siwezi kulala bila kunywa maji baridi-huwa nalala na jug la maji pembeni.
Nikinywa maji baridi akili huwa inarelax, nalala kwa haraka tofaut na nisipokunywa maji. Nifanyeje?