MSAADA: Nimepata kazi Serikalini dereva ila mshahara mdogo kuliko wa Mwendokasi ninakofanya kazi sasa. Nimechanganyikiwa!


Kuna madaraja matatu kiongozi ikijumuishwa secretaries, drivers sina uhakika kwa office attendants hao wapo ngazi ya 80k kwa night moja, then kuna officers kama wahasibu, IT Technicians, Communication officers etc, hao wapo ngazi ya 100 then kuna senior officers wanakula 120k kwa night moja. Sasa sijajua unaposema per diem inatokana na ngazi ya mshahara unamaanisha vipi labda, ila kama inatokana na cheo cha mtu, basis hizo rates ndizo nnazozifahamu mimi chief.

Suala la mikopo kwa watumishi was serikali nnavyofahamu ni liko wazi sijajua kwa upande wako unaposema ni mtumishi halafu hujawahi kupata mkopo tatizo ni nini walikukatalia kukupa...? Kwa kigezo kipi...? Au hukuwahi kuomba tu kiongozi...?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwahiyo hapo nikujua kuubwabwaja, tena kwa majungu kama memory card haa haa haa
 

[emoji23][emoji23][emoji23]kwako mwalimu kashasha
 
Kuna taasisi mambo yao hayaendani na taaisis zingine..ni muhimu kufuatilia badala ya kugeneralise..
 
Serikalini ukiumwa unahakika na mwisho wa mwezi kwa muda usiopungua miezi sita! na pia hakika ya matibabu toka bima ya afya kwa gharama ndogo na huduma nzuri. Per diem nyingi za bosi nawe umo
 
Mkuu,tatizo watanzania wengi tunapenda kutengenezewa fursa,yaani mtu atengeneze Jambo la faida halafu akunufaishe wewe kirahisi ...

800k per month yaan Ni zaidi ya mwalimu mwenye digrii
 
Mwendo kasi ni kudumu au part time. Kama ni part time acha mwendo kasi. Nenda serikali. Ukiwa serikalini posho kadiri unavyo pata uzoefu utapata zaidi ya hiyo na utakuja juta kwanini ulichelewa
 
Kuna taasisi mambo yao hayaendani na taaisis zingine..ni muhimu kufuatilia badala ya kugeneralise..

Okay kwa watu wa WMA kwani rate zao zipo chini kiasi gani kumzuia jamaa asiende kupiga mzigo serikalini chief...?

Cha msingi akomae na Transport Officer ahakikishe kila anapopata safari asimsahau T.O coz wanaingia wengi hapo kwa hiyo lazma ajiongeze asubuhi na mapema tu sio.
 
Mkuu nnavyofahamu mimi even if mwendokasi sio kama serikal lakini hauna budi kuiacha
Kwasababu! Mwendokasi ipo na itaendelea kuwepo
Sio project ya wiki au mwez n ya muda wooote
Kwahyo fanya kazi kwa uaminifu hapo hapo mwendokasi
Usitibuane na watu wala kufanya magendo
Nnaamin utadumu tu
Huko kwa 300000 Mwanangu sio deal kabisaaaa
 
Ndio tutambue wawekezaji ni muhimu kwetu, serikali haina uwezo wa kulipa mishahara mikubwa kwa wafanyakazi wote...wawekezaji/wageni waondolewe masharti na wapewe msamaha wa kulipa permit/visa free. Sisi kama wazawa tutapata ajira na mishahara mikubwa, na serikali itanufaika mno kupitia wawekezaji na hata sisi walipa kodi.
 
Hayo maisha ya kumtegemea transport officer ni maisha ya ufala uliozidi kipimo..wewe unafikiri huko anapoenda wapo madereva wangapi..wote wamfuate huyo officer unategemea nn...ndo yale mambo ya nipe changu nikuweke kwenye list
 
Ngazi za mshahara
Afya mfano
TGHS A hadi C wanapata 80,000
TGHS D hadi F 100000
TGHS G nakuendelea 120000

Hapa wakiwa manispaa na mjiji. Inapungua kulingana na kushuka miji
 
... inategemea majukumu atakayopewa. Kuna taasisi kama UDSM zina hadi matrekta ya kupeleka takataka dampo na wengine wana bodaboda za kufuata barua posta. Ajiandae kisakolojia sio lazima akakabidhiwe V8 maana ndio dream za madereva huko sirkalini hadi wanalogana. Na 300 series muda wowote itaingia serkalini tegmeeni vifo vya ghafla vya madereva!
 
Mkuu,tatizo watanzania wengi tunapenda kutengenezewa fursa,yaani mtu atengeneze Jambo la faida halafu akunufaishe wewe kirahisi ...

800k per month yaan Ni zaidi ya mwalimu mwenye digrii

Inategemea na taasisi uliyopo kiongozi kama hapa nilipo mimi ni driver na nalamba 1.2m kiongozi...!

Kuna sehemu driver anakula mpaka 3m acha kabisa chief...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…