Ahsante sana mkuu ,hapa umenipa jibu sahihi mkuu, vipi kwa wale wenye mzunguko wa randomly wanahesabu vipi siku zao za hatari?
Hahaa, iko hivi mkuu,,,,, mzunguko ule wa kawaida huwa ni siku 28. Mzunguko huu ni rahisi kutabirika siku zake za hatari kwa maana ya kuwa unajua ktkt yake (siku ya 14) ni ya hatari au ya kupachika mimba.
Tofauti na hapo ujue hyo ni randomly menstrual cycle. Unajuaje kuwa ni random? Fanya uchunguzi kwa miezi isiyopungua mitatu. Kama ambavyo umetoa mfano wa wife wako ambao mzunguko wake ulikuwa 20/10/10/8/18 ukianzia mwezi wa 5-9. Kujua km ni random mzunguko unakuwa haufanani kabisa yaani unaweza ukawa labda 10/2/20. Hapo ujue huo ni random menstrual cycle.
Random menstrual cycle maana yake ni kuwa either ovulation haitokei kabisa au inatokea lakini kwa bahati sana. Hii mara nyingi huwa ni kiashiria cha kuwa na tatizo fulani kiafya (ingawa pia kuna visababishi vingine nitavitaja mwishoni). Hivyo ukiona mwanamke ana mzunguko wa aina hii ni vyema kwenda hospital kupata ushauri wa daktari na kujua km ni tatizo la kiafya ama la.
Kugundua siku za hatari kwa mwanamke ambaye ana mzunguko usio wa kawaida huwa ni ngumu kwasababu huwa haitabiriki. Kugundua kama mwanamke yuko kwenye siku za hatari labda afanye uchunguzi wa viashiria vya yai kuwa tayari limetoka kwenye mirija ya fallopia (ovulation).
Viashiria vyenyewe ni kama:-
*Kuangalia ute ute unaotoka kwenye K
kama ni mzito na una rangi ya maziwa maziwa hii huashiria siku ya hatari.
*Joto la mwili kuzidi sana
*Ongezeko la hamu ya kufanya mapenzi n. k
Hivi ni baadhi ya viashiria tu kwahyo akiona dalili hizi ajue kuwa yupo kwenye siku za hatari.
Baadhi ya sababu zinazopelekea kubadilika kwa siku za hedhi ni kama vile :-
*Kuwa na msongo wa mawazo/Stress
*Kuugua
*Kubadilisha mazingira au vyakula au ratiba ya kula
*Matumizi ya dawa za Uzazi wa mpango au Uvutaji wa sigara n. k
*Kufanya mazoezi kwa wingi kupita kiasi
n. k