Msaada: Nyoka Mkali anazunguka Mazingira ya Nyumbani

Msaada: Nyoka Mkali anazunguka Mazingira ya Nyumbani

Msaada, kuna jirani yangu Kaingiliwa na nyoka mazingira ya nyumbani kwake, huyu nyoka ana week tangu aonekane mara ya kwanza, ila upo uwezekano ni zaidi ya week maana kabla ya hapo ilikua inatokea tu kuku kapotea, kelele za kuku bandani, usumbufu dirishani akiwa amelala n.k n.k.

Baada ya muda ndio akaonekana live. Kumtafuta imekua changamoto kwanza ni kwa mashaka maana yaweza kua naye anakutafuta au mshtukiziane akuwahi.

Na inaonesha ni mkali na ana sumu mbaya, Juzi paka wake alikua naye ndani, ile anatoka tuu nje paka akapiga kelele kutoka anamkuta paka ndio anakaukia, chini ya dk akawa tayari kafa.

Japo inaonekana alimjeruhi, maana mdomoni alikua na damu na ngozi.

Imebidi ahamishe watoto huku, hawakai tena pale. Mwenyewe anaenda kwa machale.

Nyumbani kwake kuna maua mengi sanaa yale yanayotanda mpaka ukutani, bustani ya mboga, kama mita 50 hivi kuna kijimto na nyasi nyingi, tumepatana leo tupulize ile dawa ya kuua mimea.

Kuna uwezekano anakuja na kuondoka, na si mara ya kwanza kuonekana maeneo ya nje, wanafunzi washamuona sana Kwa maelezo yao ashawahi mgonga mmoja wao kwenye kiatu.

Huyu ndugu tunamsaidiaje?
Jana kakutana na michirizi nje, akaishia nje.
Juzi katika kumsaka tukaambulia gamba tukasepa.
Mara anoe maua yanacheza au kuanguka.

Hakuna njia yoyote zaidi ya kumuua, ila njia gani sasa?

Naomba imani za kishirikina uwe ushauri wa mwisho.
Achome miba ya samaki ataibuka tu
 
Nyoka kamuuma paka anakukufa. [emoji849]

Then kamuuma mwanafunzi na hajakufa.[emoji56]

Ebu nyorosha maelezo mkuu, otherwise mnaweza mwagia mafuta ya taa ama diesel kuzunguka maeneo ambayo mnahisi huyo mgeni anaonekana.

Ama, nashauri mchome moto eneo linalo zunguka hiyo nyumba na hata ikiwezekana hayo maua mengi myateketeze kwa moto.
Hofu ni kitu mbaya sana
Aliuma kiatu cha mwanafunzi ina maana hakuifikia ngozi ya mwanafunzi
 
Pia amwage mbolea ya chumvichumvi.

Ila wawe makini, wasije wakamuua halafu wakaonekana kuwa wamemuua, maana nyoka ni nyara ya serikali kwa mujibu wa Kigwangara, au kama watamuua basi wasiwe na itikadi ya upinzani.
Achana na kigwangala mpuuzi yule 😃
 
Ajikaze achukue jiko lenye moto aweke ndani achome pilipili ya unga kama wanavyochoma ubani au achome mataili moshi uweze kuingia ndani au kama kina uwezekano amwage mafuta ya diesel au petrol lazima atahama huyo nyoka.
 
Mkuu unataka kumfukuza au kumuua kabisa?
Kama unataka kumfukuza njia zilizo shauriwa na wengi zitiumike yaani kumwaga oil chafu na mafuta ya taa kuzunguka eneo lote la nyumba. Ndani choma viwanda vya mpira pamoja na pilipili ila njia hii haitkupa amani kwakuwa anaweza kutoka akakimbia usimuone alafu ukawa unaendelea kuhofia kuwa yupo.

Toa taarifa idara ya wanyamapori waje wamsake nyoka wao huko kuna wataalamu wa nyoka hata wakiona mchirizi wanajua aina ya nyoka.

Kama unaweza ukapata wadudu wadogo kama panya wanaitwa nguchiro hawa watamsaka mpaka wamkate kichwa ndio wanaridhika, walipo hawa nyoka hawezi kuishi.

Tafuta sangara wapandikize hapo kwako, sangara ni wadudu wadogo kama siafu. Hawa walipo ni usumbufu tosha kwa nyoka lazima akimbie.
Hii njia ya sangara alituma mkoloni mmoja aliekuwa anamiliki mashamba makubwa ya karanga huko wilayani Nachingwea. Huyu mkoloni aliitwa John Mollam, aliamua kwenda Kwenye misitu huko Australia kutafuta nyoka ili akawapandikize kwenye mashamba ya karanga kwalengo la kudhibiti panya, baada ya nyoka kustawi na kuwa tishio wakamshinda akaenda kutafuta hawa siafu sangara ili kudhibiti nyoka na alifanikiwa kwani nyoka walikimbilia maeneo ya misitu na mlimani kukwepa sangara.
 
Mkuu Kwanza tulia,chukua lita ya petroli,changanya na disel lita moja na mafuta taa ya jero,spray vyumbani Kwanza,kaa siku mbili au tatu ili Kama yuko ndani atoke afu pulizia nje kwenye majani. Hii ikishindikana jua ni mkono wa mtu ambao ni lazima uondolewe kwa maombi au mtu vilevile. UKIFANYA HIVI,NIAMBIE
 
Back
Top Bottom