Msaada: Nyumba kuwa na matumizi makubwa ya umeme!!!

Msaada: Nyumba kuwa na matumizi makubwa ya umeme!!!

Mimi nipo kwenye nyumba ya kupanga yenye wapangaji 8 kati ya hao wapangaji saba wapo single na mmoja ndo mwenye mke na anamtoto mdogo muda wa mchana anabaki mkewe na mtoto sisi wengine tunaenda kusaka pesa na huwa tunatoka asubuhi sana kurudi usiku ratiba huwa hazitofautiani sana

Lakini cha kushangaza unit 40 zinaisha ndani ya siku 5 au 6 na kwa mwezi tunatumia unit 200 sijui tatizo ni nini kodi yangu ikiisha nataraji kuhama kwa hii nyumba bili ya umeme inanimalizia pesa
Mm mwenyewe nilipatwa na tatizo km lako. Ikibidi niweke sub meter, kwa mwezi nalipa elfu 5-6 kwa mwezi.
 
Hujasema ukubwa wa nyumba. Ni chumba kimoja au nyumba kubwa ya familia? Lakini hata hivyo ulitegemea units 28 zimalize mwezi?
Tatizo kwa wengi, sio matumizi makubwa, bali bei ya umeme. Mimi kwangu, nimejiwekea utaratibu wa kununua umeme unit 60 kila mwezi. Lakini matumizi yangu ni unit 45-55 kwa mwezi. Nipo kwenye watumiaji wa ile punguzo. Hivyo, hizo unit 60 huwa nanunua kwa 7,380/=. Kwa hiyo bei nyingine, ningenunua kwa zaidi ya 20,000/=.
 
Kaka hapo hua kuna issue kubwa mbili, kwanza ni ile earth rod hua inachoka au hakuiweka vzr, hii ilinilia sana unit kabla haijabadilishwa
Pili ni size ya waya za wiring, ita fundi aangalie vitu hivyo viwili na vingine atakavyoshauri yeye
Shukran!!

Hizi ni fix
 
Kitu cha umeme kilichochoka. TV hasa zile za plasma na mafriji ya kizamani.

Hata tv za LED zinatafuna moto. mm nina OLED TV ya LG ina watt 300. hiyo ikifanya kazi masaa ma 3 lazima unit moja ilike. sasa kwa 24 hrs inapiga kazi kuanzia 6 - 9 hours ni unit ngapi hizo?
 
Hata tv za LED zinatafuna moto. mm nina OLED TV ya LG ina watt 300. hiyo ikifanya kazi masaa ma 3 lazima unit moja ilike. sasa kwa 24 hrs inapiga kazi kuanzia 6 - 9 hours ni unit ngapi hizo?
Duh hii itabidi nihakiki maanake huwa nakaa weekend kama jumapili naangalia TV hata masaa 10 na overall usage haizidi 3 units.
 
3bedroom house mkuu. Sio kumaliza mwezi lakini angalau hata wiki mbili nisingelalamika mkuu

Ngoja nikushauri mkuu.
that is an area of career

asikudanganye mtu mambo ya kuchimba erthrod sijui mkaa sijui chumvi.

issue ya umeme ni matumizi yako mwenyewe hakunaga uchawi.

watakuja watu hapa na fix sijui za leakage lakini ni uongo tuu.
Mambo ya leakage yalikuwaka zamani kabla ya ELCB/ RCD/ RCCB

hivi vifaa vya kukinga circuit AKA circuit braker haviwezi vumilia kitu inaitwa leakage, so kwenye assumption yako ondoa hiyo. unless circuit braker yako iwe mbovu haitrip so unaweza itest kwa kubonyeza T button.

Njoo na hesabu hapa, una taa ngapi za nje zinawaka kwa muda gani na ni za watts ngapi

una taa ngapi za ndani zina watts ngapi zinawaka kwa muda gani

Vipi kuhusu Rice cooker ipo? au hita za maji moto au kuota moto?

TV inafanya kazi masaa mangpi na ni ya inches ngapi ila ukijua watts ni vizuri zaidi.

fridge ni ya watts ngapi? ina energy rating ipi ?

wala hakuna uchawi hapo unahitaji kueleweshwa tuu. haakuna technica fault in most cases
 
Anza na earth rod..tafuta copper original... ukienda dukani wakikwambia original ipo tafuta sumaku iguse...ikinasa ujue hiyo sio original...funga earth rod original...uone

kitu ambacho watu mnachanganya ni kwamba. kama nyumba ina leakage, na wew ukaongeza kwa kweka earthrod nzuri na kuweka mkaa sijui chumvi nk. kwa kifupi ukaimpruv earthing ndio umeme utalika kuliko mwanzo ilivyokuwa.

Boss leakage haitatuliwi kwa kuboresha earthing/ grounding

sijui kwa nini concept ndogo hii huwa inachanganya watu
 
unit 40 zinaisha ndani ya siku 5 au 6 na kwa mwezi tunatumia unit 200 sijui tatizo ni nini kodi yangu ikiisha nataraji kuhama kwa hii nyumba bili ya umeme inanimalizia pesa
Issue ya umeme kwenye nyumba za kukodi ni majanga sana, yaani unaweza kukuta garama ya umeme inazidi ya pango!.
 
Ngoja nikushauri mkuu.
that is an area of career

asikudanganye mtu mambo ya kuchimba erthrod sijui mkaa sijui chumvi.

issue ya umeme ni matumizi yako mwenyewe hakunaga uchawi.

watakuja watu hapa na fix sijui za leakage lakini ni uongo tuu.
Mambo ya leakage yalikuwaka zamani kabla ya ELCB/ RCD/ RCCB

hivi vifaa vya kukinga circuit AKA circuit braker haviwezi vumilia kitu inaitwa leakage, so kwenye assumption yako ondoa hiyo. unless circuit braker yako iwe mbovu haitrip so unaweza itest kwa kubonyeza T button.

Njoo na hesabu hapa, una taa ngapi za nje zinawaka kwa muda gani na ni za watts ngapi

una taa ngapi za ndani zina watts ngapi zinawaka kwa muda gani

Vipi kuhusu Rice cooker ipo? au hita za maji moto au kuota moto?

TV inafanya kazi masaa mangpi na ni ya inches ngapi ila ukijua watts ni vizuri zaidi.

fridge ni ya watts ngapi? ina energy rating ipi ?

wala hakuna uchawi hapo unahitaji kueleweshwa tuu. haakuna technica fault in most cases
Nashukuru mkuu, ngoja nifanye majaribio ya kuzima taa za nje kwa Leo usiku tuone matokeo yake itakuaje. Nina taa kama 7 hivi
 
Nashukuru mkuu, ngoja nifanye majaribio ya kuzima taa za nje kwa Leo usiku tuone matokeo yake itakuaje. Nina taa kama 7 hivi

ukifanikiwa kuaanda jedwali

Column ya kwanza weka kifaa jina lake pili weka watts zake, tatu weka idadi yake nne weka masaa kinayofanya kazi kwa siku/ 24 hrs ntakupa majibu.

au tuwasiliane DM tufix
 
Asubuhi Zima vitu vyote vinatumia umeme na wakati huo soma idadi ya unit zinasoma kwenye mita ,baadaye mpaka jioni ukiona idadi ya units zimeongezeka ujue Kuna leakage ya umeme,
 
Kuna comment za kijinga humu😂😂😂.
eti mimi umeme unalika kweli kweli, zaidi naosha sufuria tu ndio nyingi ndani😂😂😂😂.
sasa kuosha sufuria na umeme wapi na wapi?
 
Fridge ndogo ukijisahau ikawa hujaweka auto ijizime yenyewe kila baada ya muda ni vinakula umeme balaa… Kingine ni Feni, Radio kama ni ya Mtumba au subwoofer yenye watts nyingi kama inatumika muda mwingi
 
ukifanikiwa kuaanda jedwali

Column ya kwanza weka kifaa jina lake pili weka watts zake, tatu weka idadi yake nne weka masaa kinayofanya kazi kwa siku/ 24 hrs ntakupa majibu.

au tuwasiliane DM tufix
Taa watt 15 ziko 7 masaa almost 13
Friji watt 500 (auto) masaa 24
Hisense Tv 55" 4k maa 9
Pasi, watts 1000 nusu saa
Redio (sub ufa za kichina) na Azam decoder 9hrs
Blender (inatumika almost mara 5 kwa mwezi chini ya dakika 15)
 
Back
Top Bottom