Msaada unahitajika maana naona kichwa kinaelekea kupasuka

Msaada unahitajika maana naona kichwa kinaelekea kupasuka

Hakuna jambo lisilokuwa na sababu mpaka mkeo anakukimbia na mtoto anamtelekeza na wewe unataka kumtelekeza inaonekana your the kind of Man ambaye hauko responsible kusimamia majukumu yako kama baba wa familia.

Ushauli wangu pambana umrudishe mkeo nyumbani na uanze kusimamia majukumu yako kama baba haya mambo ya kumpeleka mtoto sijui kwa sister sijui kwa mama achana nayo wee pambana na hali yako simamia majukumu yako.
 
Nimepata uchungu sana! Yani baba umgawe mtoto? Kweli mwanaume unathubutu kufanya hivyo? Mkeo alikusanya kila kitu baada ya kukuta msg za yule mchepuko wako ukimdanganya huna mke!

Ataachaje kuondoka? Kwani kwako alikuja na huyo mtoto? Lea mwanaoooo Tena pambana, unaishi Dar halafu unakuwa mzembe?

Umenisikitisha, pole kwa changamoto Ila jitahidi kumlea na uishi naye, tafuta mdada.
 
Msaada unaitajika ndugu zangu maana hata sijielewi kabisa kwa mambo yanayoendelea. Nilikuwa na mke wangu ila tukaamua kuachana baada ya yeye kuchukua vitu na kuondoka. Baada ya muda kaona haitoshi kamtelekeza mtoto wetu mdogo mwenye umri wa mwaka 1 na nusu kwa sister wangu.

Hilo wazo la kumgawa mtoto linanitafakarisha sana hadi naona huyo mama aliye kuachia mtoto anastaili maana angeondoka naye usingemsaidia kwa chochote
Hadi kuondoka na vitu ni halali yake maana kwa maelezo yako inaonyesha vitu ni vyake
N.k
Kaka wewe ni mwanaume simama kiume
Umeachiwa mtoto ni mdogo lakini kwa uwezo wa Mungu utaweza kumlea

Si kushauri umgawe mtoto kama tunavyogawa vitu ambavyo hatuviitaji mf. Nguo, simu, vyombo n.k

Tafuta mbinu za kutatua hiyo changamoto maana mazingira uliyo nayo unayajua

ILA
Acha uvivu, fanya kazi yoyote alali kama ukienda kwenye ujenzi omba kuwa saidia fundi baada ya muda ikija swala la umeme unasema wewe ndio fundi kidogo kidogo unapata conection

Acha utoto tambua wewe ni mkubwa na
Akili yako iwe ya kikubwa siyo ya kitoto

Acha woga wa maisha wa kutokudhubutu
Acha mawazo mgando
Simama kama baba na mtoto wako
Naamini ukiamua unaweza Kujiudumia wewe na mwanao

Mwisho tambua ulipo kosea mmalize tofauti zenu wewe na mama mtoto KAMA ITAWEZEKANA maana huyo mama ni mzuri toka mwanzo sema tu ulimbadilisha mpaka ikatokea kilichotokea

Kama haiwezekani endelea na maisha
 
Msaada unaitajika ndugu zangu maana hata sijielewi kabisa kwa mambo yanayoendelea. Nilikuwa na mke wangu ila tukaamua kuachana baada ya yeye kuchukua vitu na kuondoka. Baada ya muda kaona haitoshi kamtelekeza mtoto wetu mdogo mwenye umri wa mwaka 1 na nusu kwa sister wangu.
Utakuwa na roho ya ajabu sana kumgawa mtoto wako halafu bado ukaendelea kujiita mwanaume nimejikuta nashikwa na hasira za ghafla tu yani mkuu kiukweli ningekuwa karibu na wewe ningekutia makofi heavy .

Nimeshapata na picha kwanini huyo uliyemuita mke alikukimbia yaani unashindwa kabisa kulea mtoto hadi umgawe? 😠😠😠
 
Msaada unaitajika ndugu zangu maana hata sijielewi kabisa kwa mambo yanayoendelea. Nilikuwa na mke wangu ila tukaamua kuachana baada ya yeye kuchukua vitu na kuondoka. Baada ya muda kaona haitoshi kamtelekeza mtoto wetu mdogo mwenye umri wa mwaka 1 na nusu kwa sister wangu.
ULIOAJE NA KUZAA BILA KUWA NA UWEZO WA KUTUNZA MTOTO? Ndio maana mke kakukimbia sababu hauna mipango ya maisha. Na mtoto ni wajibu wa baba na mama. Kama yeye amemtelekeza, ungekuwa ni mtu wa mipango usingeshindwa. Mimi sipendi kabisa watu mnazaa halafu mnataka wengine wawasaidie kulea. Kwendaaa!!!
 
Unataka kugawa mtoto wako akalelewe na kuchukuliwa na mtu mwingine. Huyo mtoto masikini amezaliwa kwenye shida na ni mtoto wa kike, mama kamtelekeza na baba anataka amgawe. Ningekuwa na uwezo ningemchukua nimlee kwa miaka hata mitatu maana naona kwa hapo lazima taifa lipate hasara.
Wapumbavuu sana. Wanazaa tu bila mipango. Pambaf kabisa huyu jamaa.
 
Pole na majanga papaa.

1. Kwasababu ya uwezo wako wa kifedha kuwa mdogo. Mm nashauri umtafute huyo mzazi mwenzio. Umuombe msamaha ili arud mkae wote kama mwanzo.

Na Mlee mtoto wenu. Nina uhakika ww ndio ulizingua. Bas omba radhi ili mtoto alelewe vyema.

Fanya namna yoyote mwanamke arud nyumban.

2. Na uahidi kwa kuandikishana ni kias gan utatoa cha matunzo ya mama na mtoto.

Kwa namna hii. Mwanamke atakuona unajali familia na unajutia uliyoyafanya.
 
Braza unataka kugawa mtoto yani kumtoa mazima kisa hali ni ngumu?

Hebu imagine umemgawa halafu soon mambo yako yakawa poa je utaenda kumdai?

Hebu fikiri mtoto akikuwa akaja kujua kuwa mama yake alimtelekeza na kisha baba yake akaamua kumgawa huyo mtoto atapata trauma kiaisi gani?

Bro pambana sana asee yani ikiwezekana usilale piga mishe huku na huko upate hata khaki daily hutashindwa kumlea huyo mtoto asee.

Kikubwa usimgawe huyo mtoto kwasababu utakuja kusababisha shida kubwa siku za mbele.
 
Usigawe mtoto we komaa na binti yako tu chamuhim jitaidi kutafta ela ya kumtunza
 
Back
Top Bottom