Msaada wa jinsi ya kusamehe na kuachilia

wewe inaonyesha kuna mazingira hujawaii kuishi mimi naweza pishana na mtuu mwaka mzima na tuko sehemu moja huwa na tabia ya kutokujali hasa pale napo ona niko sahihi kwa upande wangu.

kwa maelezo yako kwanza una huruma sana na pia kuna maisha ambayo huja wai kuyaishi no maana unakuwa unapata matatizo madogo madogo ya msongo wa mawazo. japo una onekana uko vizuri kazini lakini bado una kasoro moja, kuishi wewe kama wewe.

mke wako aliogea ukweli usimpe hiyo deal wewe umetoa na pia kazini unajua yeye sio mfanisi juu na mzoefu kama wewe kwanini una nyenyekea kuna mda unakuwa mkaksi na kukataa kazi mfano kama ambazo hazina malipo.

kazini mwenye tatizo sio wewe bali ni yeye japo ukiingia ofisini unaona kama tatizo kubwa ni wewe cha msingi jenga uhusiano mzuri na wafanyakazi wengine kwa ukaribu zaidi na anza kumchukulia kama boss na sio rafiki tena maana sio kwa tabia anazo onyesha kuwa huru pale kwenye ukweli itakuwia vigumu kama huja zoea ni hayo tu... rafiki wa kweli ni muwazi na mkwelii

(sijaeleza kiundani ila nime jaribu)
 
Kama umeshindwa kumsamehe na muhusika haonekani kujutia kosa lake unatakiwa umchukulie hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kumueleza jinsi ulivyochukia/kuathirika na vitendo vyake viovu kwako (hii itasaidia kukuletea afueni ndani ya roho yako)
Mhusika haonekani kujutia kosa lake kabisa...amefikia.hatua anataFut vibaka waje waniibie kwenye kaz zangu nilost..! Aliwah mwambia dada wa kazi wang aweke chumv kwa engine atamlipa🤨...yaan kosa halipo..
 


Wanaume wengi hawawezi kuishi hvyo...mm hata 5yrs napishana tu na ww kiroho safi..
 
Pole sana mkuu. Ni kweli hypertension inaweza kuchangiwa sana na hiyo stress ulitopitia kwa kipindi kirefu. Una alternatives 2:
1_ imani zote zinasisitiza juu ya msamaha. Unaweza kwenda kwa kiongozi wako wa dini kwa ushauri nasaha. Baada ya hapo akuombee. Ningekuwa wewe ningetoa na sadaka ya kumuachilia. Sadaka ina nguvu kubwa sana katika imani yako na nina hakika ingekusaidia (binafsi nilishawahi kumtolea sadaka mtu alienitesa sana kazini. Mungu alivyo muaminifu yule ndugu aliondolewa)

2_ Counseling. Kuna washauri nasaha ambao wanaweza kukusaidia kupambana na hii hali. Japo ina gharama kiasi lakini unahitaji kupona.

Kila la kheri. Kusamehe ni muhimu sana kwako. Usijiadhibu kwa makosa uliyotendewa, unajionea.

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
 
Na kwa kusema hivyo anayefaidika zaidi na msamaha ni yule anayekosewa. Si yule anayekosea! Faida ya kusamehe toka moyoni ni kuondokana na maumivu yatokanayo na aliyekukosea au kukuumiza. Ukiijua siri hiyo hutabaki na wabaya wako na maumivu yao moyoni mwako.

Hata Mungu hutusamehe kwa faida yake Mwenyewe - kwa ajili ya utukufu wa jina lake. Hapendi aendelee kuumia kwa makosa na viburi vyetu kwake.

Achilia au yatupilie mbali makosa ya watu kwako ili upate amani moyoni. Kaa nao mbali moyoni na hata kimwili ikiwezekana!
 
Sahihi kabisa!
 
Ushauri murua kabisa
 
Nimewahi andika juu ya kinyongo changu kwa Marehemu Sr. Mary Antony. Yaani toka primary mpaaka ule mwaka nilioleta kisa changu hapa. Hiyo ilikua ni early 2000s. Yaan kinyongo kiliendelea hata alipokufa. Lakini siku niliposimulia humu ndo siku niliachilia rasmi. Yaan sijawahi kuumia tena nikisia jina lake. Kuongea kunasaidia sana. Yaan hata kwenda kumuaga nilikataa kabisa nikiwa nimefika chuo hapo Luguruni hapo. Mpaka kesho sijisikii tena kumchukia. Natafuta siku niende convent kwao makaburini kuweka maua kbs. Nafurahi mno maana imenitesa sana zaidi ya 15 years. Kuongea kuna faida. Umefanya jambo jema sana. Utanambia after some time...

May you heal from this brother
 
Ndugu yangu nilisha samehe! ila nakumbuka na kuhisi tena maumivu.
Hakuna msamaha wa kweli pasipo kuweka wazi tatizo. Ulipaswa umwambie ukweli boss wako ndipo usamehe, lakini wewe mwenyewe uliamua ukae nalo and that's what has been eating you mpaka kuwa na hypertension.
Kwa boss wako ushachelewa Sana coz yaonekana mambo sasa ni shwari kwasababu ulichagua njia hiyo, ila ingekuwa shwari zaidi Kama boss wako angejua kuwa unajua kila kitu na majungu aliyokuwa akikupiga.
Kwasasa ongeza maombi na tafuta rehema za Mungu mwenyewe, vinginevyo utaingia kwenye Imani nyingine itakayokugarimu zaidi.
 
Nak
Nakumbuka kisa chako. Hopeful now you're ok
 
Nak

Nakumbuka kisa chako. Hopeful now you're ok
I am very good aisee. Yaan siku hizi hata umtaje je.. siumii zaidi naona kama nammiss. Yule sista ilibidi akasomee jeshi. Halaf enzi hizo walikua wanapitia jeshini. Maana amepanda hewani balaa halaf ana mkono wa kutosha. Wanawake wa kibosho ni wakorofi in general. Nilipoelewa hili ilikua rahisi zaidi kusamehe
 


Hahaa umenikumbusha luguruni..lol
 
Kama bado anaendelea kukupiga majungu,kaa nae chini,ongea nae Kama rafiki wa mwanzo,ongea nae kwa upendo na hekima,yeye ni binadamu naamini atakuelewa ,unamwambia ukweli.kukaa kimya itamfanya aone unajipanga kulipiza kisasi juu yake,kwa kuwa anajua aliyokufanyia.rafiki yako alishindwa kukabiliana na mazingira ya hapo kazini kwenu,na inavyoonekana ni ofisi imejaa watu wa manenomaneno,wewe ndo ulipaswa uwe mwalimu na ndg kwake.labda nikuulize je Kama angelikuwa ni Kama,au mdogo wako,ungelikaa kimya!?? jibu ni hapana ,Basi hapo ndipo ulipokosea ndg yangu mleta mada.kukaa na kitu moyoni kinachokuumiza ni dhambi ,sawa na dhambi nyingine,pia ni unafiki sawa na unafiki mwingine.sorry kwa kutumia lugha Kali kidogo bt my hope u get me.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…