Msaada wa Kisheria kuhusu mahusiano na Mwanafunzi

Msaada wa Kisheria kuhusu mahusiano na Mwanafunzi

Sitaongelea nani aletwe shahidi sababu hiyo ni kazi ya Mwendesha mashtaka wa serikali, na jibu la wazi juu ya hilo mtendaji hana huo uwezo wala mamlaka ya kusema nani awe shahidi hivyo kama kweli anafanya hivyo anafanya kazi ya watu sio yake.

Turudi kwenye hicho mnachoita ushahidi wa picha na video.

Hivyo havitoshi kumkuta na hatia huyo kijana. (Sitasema zaidi sababu mnataka kumfunga tu sio kutenda haki).
Mtendaji ndiye anayetaka kumfunga na sio wazazi
 
Shahidi anayeharibu ushahidi kwa makusudi ni kweli anaweza kukutwa na hatia na huyo shahidi ni pamoja na huyo mtendaji.

Kwani kesi ipo polisi au Mahakamani maana ni kama kuna stori mbili tofauti hapa.
Kesi ilianzia Polisi wazazi waliitwa maana ni karibu waliweza kufika, na ni tarehe 16 mwezi uliopita, Jana ndo amewatumia summons ambayo imeandikwa kwa lugha ya Kiingereza. Akawasomea na kuondoka akiwataka leo wafike mahakamani. Leo asubuhi kafika nyumbani kuwachukua na pikipiki kwenda mahakamani hajawakuta ila kaenda shuleni kamchukua binti kaenda naye mahakamani.

Binafsi nikiangalia hii kesi sioni wazazi wakihusika ndiyo maana nikaja hapa kuomba kwenu mnaoijua sheria.
 
Ndugu wa JF hapa kuna Mvulana ( Sio Mwanafunzi) alikamatwa na Msichana (Mwanafunzi).

Alipokamatwa akaitwa mtendaji wa kata pamoja na baba mzazi wa binti. Kesi ikapelekwa Polisi then mahakamani. Mahakama inataka ushahidi (Ambao tayari upo maana walipigwa picha na video wakiwa pamoja)

Mtendaji amekuwa akiwalazimisha wazazi wa binti hususani mwanamke (ambaye hakuwepo kwenye tukio) kufika mahakamani kutoa ushaidi na mama amegoma kwa madai ya kuwa hakuwepo kwenye tukio hivyo hana ushaidi wa kuiambia mahakama lakini pia na ugumu wa maisha hana nauli za kumpeleka mahakamani.

Swali langu: Je huo ushaidi wa picha hautoshi kumfunga huyo kijana?. Na je anayehitajika kutoa ushaidi ni upande wa wazazi au wale waliowakamata na kupeleka taarifa kwa mtendaji.

Naomba kuwasilisha.
Kosa liko wapi?
 
Mkuu kosa la ubakaji ni lazma LITHIBITISHWE PASIPO KUACHA SHAKA YOYOTE.
Unadai kuwa mliwapiga picha je hizo picha mliwapiga wakiwa mazingira gani? Isijekua mmewakuta watu wamekaa chumbani nyie mnawapiga picha.
Halafu mnapolazmisha wazazi wakatoe ushahidi ni ushahidi gani mnaoutaka kama mzazi hauwepo eneo la tukio?
Waende mtendaji na waliokuwepo eneo la tukio pamoja na huyo mwanafunzi ndio wakatoe ushahidi kama ukiwa na mashiko mahakama itamkuta jamaa na hatia na kama hautakua na mashiko basi jamaa ataachiwa
 
Mkuu kosa la ubakaji ni lazma LITHIBITISHWE PASIPO KUACHA SHAKA YOYOTE.
Unadai kuwa mliwapiga picha je hizo picha mliwapiga wakiwa mazingira gani? Isijekua mmewakuta watu wamekaa chumbani nyie mnawapiga picha.
Halafu mnapolazmisha wazazi wakatoe ushahidi ni ushahidi gani mnaoutaka kama mzazi hauwepo eneo la tukio?
Waende mtendaji na waliokuwepo eneo la tukio pamoja na huyo mwanafunzi ndio wakatoe ushahidi kama ukiwa na mashiko mahakama itamkuta jamaa na hatia na kama hautakua na mashiko basi jamaa ataachiwa
Naam, kwanza mimi sikuwa eneo la tukio, Binti hajabakwa na hawakuwakuta wanafanya tendo na picha zilizopigwa wapo kitandani wamekaa. Ndiyo maana nikajaribu kuhusisha hii kesi na wazazi wake ambao hawakuusika kabisa mpaka taarifa zimepelekwa polisi, na baadae Mahakamani ni Mtendaji wa kata ndo anaratibu na kusimamia mpango mzima. Shida imekuja baada ya kuwalazimisha wazazi wakatoe ushaidi na hawajui chochote kilichotokea na wenyewe walihadithiwa.
 
Kesi ilianzia Polisi wazazi waliitwa maana ni karibu waliweza kufika, na ni tarehe 16 mwezi uliopita, Jana ndo amewatumia summons ambayo imeandikwa kwa lugha ya Kiingereza. Akawasomea na kuondoka akiwataka leo wafike mahakamani. Leo asubuhi kafika nyumbani kuwachukua na pikipiki kwenda mahakamani hajawakuta ila kaenda shuleni kamchukua binti kaenda naye mahakamani.

Binafsi nikiangalia hii kesi sioni wazazi wakihusika ndiyo maana nikaja hapa kuomba kwenu mnaoijua sheria.
Kwanza kabisa ni kesi ya aina gani imefunguliwa?, sababu hapo inapaswa kuwa kesi ya jinai. Na ikishakuwa hivyo kuna ofisi ya muendesha mashtaka wa serikali (NPS) hawa ndio wanaosema nani awe shahidi kwenye hizo kesi dhidi ya Jamhuri.

Polisi wao ni kukusanya ushahidi na kuandikisha maelezo na kupeleka faili NPS na kumpeleka mtuhumiwa Mahakamani siku ya kwanza baada ya hapo kazi yao imeisha.

Kesi za hivi zinazohusu makosa ya mahusiano na wanafunzi plus ubakaji yanaenda Mahakama ya wilaya au hakimu mkazi sasa nikuulize hiyo kesi ipo Mahakama gani?. Kama ipo Mahakama ya mwanzo jua ni magumashi hayo hapo wahuni wanatafuta kuwatoa hela.

Swali lingine muhimu, mtuhumiwa yupo wapi na ni nani mtuhumiwa kwenye hiyo kesi?.

Kuna jambo halijakaa sawa Mkuu.
 
Kesi ilianzia Polisi wazazi waliitwa maana ni karibu waliweza kufika, na ni tarehe 16 mwezi uliopita, Jana ndo amewatumia summons ambayo imeandikwa kwa lugha ya Kiingereza. Akawasomea na kuondoka akiwataka leo wafike mahakamani. Leo asubuhi kafika nyumbani kuwachukua na pikipiki kwenda mahakamani hajawakuta ila kaenda shuleni kamchukua binti kaenda naye mahakamani.

Binafsi nikiangalia hii kesi sioni wazazi wakihusika ndiyo maana nikaja hapa kuomba kwenu mnaoijua sheria.

Sio sawa kumpeleka uyo kijana jela uyo mtendaji mpuuzi tuu, apo mnapaswa kumdefend uyo kijana kupitia uyo binti maana binti akisema uyo mvulana ni alikua ni mtu wake wakaribu kwajil ya masomo tu na sivinginevyo sizani kama mahakama itapinga.
 
Kwanza kabisa ni kesi ya aina gani imefunguliwa?, sababu hapo inapaswa kuwa kesi ya jinai. Na ikishakuwa hivyo kuna ofisi ya muendesha mashtaka wa serikali (NPS) hawa ndio wanaosema nani awe shahidi kwenye hizo kesi dhidi ya Jamhuri.

Polisi wao ni kukusanya ushahidi na kuandikisha maelezo na kupeleka faili NPS na kumpeleka mtuhumiwa Mahakamani siku ya kwanza baada ya hapo kazi yao imeisha.

Kesi za hivi zinazohusu makosa ya mahusiano na wanafunzi plus ubakaji yanaenda Mahakama ya wilaya au hakimu mkazi sasa nikuulize hiyo kesi ipo Mahakama gani?. Kama ipo Mahakama ya mwanzo jua ni magumashi hayo hapo wahuni wanatafuta kuwatoa hela.

Swali lingine muhimu, mtuhumiwa yupo wapi na ni nani mtuhumiwa kwenye hiyo kesi?.

Kuna jambo halijakaa sawa Mkuu.
Kesipo mahakama ya Wilaya na kijana amewekwa mahabusu kwa mujibu wa taarifa ya mtendaji
 
Sio sawa kumpeleka uyo kijana jela uyo mtendaji mpuuzi tuu, apo mnapaswa kumdefend uyo kijana kupitia uyo binti maana binti akisema uyo mvulana ni alikua ni mtu wake wakaribu kwajil ya masomo tu na sivinginevyo sizani kama mahakama itapinga.
Huyu binti alitishiwa na kupangiwa maneno ya kuongea kipindi maelezo yannachukuliwa polisi na inasemekana kijana naye leo amekiri kwamba ni kweli alikamatwa kweli.

Binafsi kijana sijihusishi naye sana afungwe asifungwe ni sawa ila kulazimisha wazazi kutoa ushaidi na hawakuwa kwenye tukio ndo kinachonipa wasiwasi
 
Ndugu wa JF hapa kuna Mvulana ( Sio Mwanafunzi) alikamatwa na Msichana (Mwanafunzi).

Alipokamatwa akaitwa mtendaji wa kata pamoja na baba mzazi wa binti. Kesi ikapelekwa Polisi then mahakamani. Mahakama inataka ushahidi (Ambao tayari upo maana walipigwa picha na video wakiwa pamoja)

Mtendaji amekuwa akiwalazimisha wazazi wa binti hususani mwanamke (ambaye hakuwepo kwenye tukio) kufika mahakamani kutoa ushaidi na mama amegoma kwa madai ya kuwa hakuwepo kwenye tukio hivyo hana ushaidi wa kuiambia mahakama lakini pia na ugumu wa maisha hana nauli za kumpeleka mahakamani.

Swali langu: Je huo ushaidi wa picha hautoshi kumfunga huyo kijana?. Na je anayehitajika kutoa ushaidi ni upande wa wazazi au wale waliowakamata na kupeleka taarifa kwa mtendaji.

Naomba kuwasilisha.


  • Kuna Mimba?
  • Mmemfumania wakilalana?

Kama hakuna hayo hapo muachen kijana wa watu.
 
Back
Top Bottom