Msaada wa kupata Pasi ya kusafiria

Msaada wa kupata Pasi ya kusafiria

Namora

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2020
Posts
410
Reaction score
1,014
Wakuu naombeni mwongozo wenu tafadhali, nilikua nafatilia pasi ya kusafiria (International Passport) kidogo nimekumbsna na vikwazo. Mimi niko mkoani huku (Chuganian)

Nimejaribu kuulizia uhamiaji wa hapa nimeelezwa niwe na:
  1. Cheti cha kuzaliwa (Ninacho)
  2. Namba za Nida (ninazo)
  3. Cheti cha kuzaliwa mzazi (Ninacho cha baba)
  4. Barua ya Serikali ya mtaa
  5. Barua mimi ya maombi ya Passport kwenda kwa afisa uhamiaji mkoa
Wamesema pia Nikishakamilisha vitu vitatumwa Dar ambapo itachukua kama mwezi hivi hadi kupata passport. Sasa naomba kuuliza kwa mliofuatilia passport kipindi cha hivi karibuni.

Barua ya Serikali za mtaa na barua yangu ya kuomba passport ni Muhimu au ni huku tu wa mkoani ndio tunaambiwa hivyo??

Kama ni lazima niandike barua ya kuomba, je inakuwa katika lugha gani??? Na mfumo wa uandishi wake upoje??

Kwenye site ya uhamiaji wanasema uwe na ushahidi wa safari au ushahidi wa Shughuli anayofanya mwombaji. Je ushahidi huo ni upi?? Na unapatikanaje?

Kama kuna waliowahi kupata passport kutokea huku mkoani nilipo basi naombeni uzoefu wenu tafadhali.

Nawasilisha
...

UPDATE


Nimefanikiwa kuipata nikiwa huku huku mkoani kwa muda wa siku 21. Mungu mwema

Maelezo haya ya mkuu Mosha yapo sahihi kwa 99%

Ili kupata passport, unatakiwa uwe na.
1. Cheti cha kuzaliwa.
2. Cheti cha kuzaliwa cha mzazi mojawapo.
3. Kitambulisho cha Taifa.
4. Kitambulisho cha Kazi Kwa watumishi wa umma au barua ya utambulisho KUTOKA Serikali za mitaa Kama hujaajiriwa.
5. Barua ya maombi ya passport kama uko mkoani anapitisha kwa kamishna WA mkoa kwenda Kwa kamishna mkuu, anwani zao za posta unaweza kuzipata ofisini kwao.
6. Uthibitisho wa safari ukionyesha nchi unayokwenda.
7. Baada ya kuwa na vielelezo vyote utaanza kujaza form ya maombi online kupitia uhamiaji portal, kuna sehemu uta upload barua ya utambulisho na Cheti cha kuzaliwa.
Kama ombi limekamilika utapewa contral namba ya kulipia 20,000 ili uweze Ku print form.
Ukishaprint form utatafuta mashaidi waijaze na pia mwanasheria.
8. Baada ya hapo utaenda ofisi za uhamiaji ukiwa na hiyo form na vielelezo nilivyotaja hapo juu,
9. Ombi litapitiwa kama hakuna dosari, litapitishwa, utalipia 130,000 Kwa kutumia control namba, halafu utakamilisha ombi Kwa kupiga picha pamoja na kuchukuliwa alama za vidole.
10. Baada ya hapo utasubiri Kwa mwezi mmoja passport kuwa tayari.
11. Kama unahihitaji Kwa haraka na hauna baadhi ya vielelezo unaweza watumia vishoka, Ila utawalipa gharama za ziada almost 100-200k.
 
Acha tu mkuu Afrika tuna laana walahi, kitu ni haki yako lakini utakavyozungushwa. Yaani unalazimishwa kutenda dhambi bila kupenda
Hii Laana Kweli Yaani Vigezo Unavyo Vyote Kupewa Inakuwa Nogwa Hao Wanaotaka Pesa Ya Brush Bado Serikali IInawalipa Salary Kupitia Kodi Ambayo Wewe Unaitoa
 
Usitoe kitu wewe ni Mtanzania passport yako utapata sasa hivi unajaza Online harafu unapeleka viambatanisho vyako uhamiaji baada ya kulipia huko 30,000 kwa Control Number kiasi kingine utalipia baada ya ofisa uhamiaji kuzipitisha mimi sijawahi kufikiri kutoa Rushwa kwa mkwaju wa Nchi yangu na mkwaju napata tuu hapa nina fomu za watoto ntazipeleka wiki ijayo.
 
Back
Top Bottom