Msaada wa kupata Pasi ya kusafiria

Msaada wa kupata Pasi ya kusafiria

Wakuu naombeni mwongozo wenu tafadhali, nilikua nafatilia pasi ya kusafiria (International Passport) kidogo nimekumbsna na vikwazo. Mimi niko mkoani huku (Chuganian)

Nimejaribu kuulizia uhamiaji wa hapa nimeelezwa niwe na..
  1. Cheti cha kuzaliwa (Ninacho)
  2. Namba za Nida (ninazo)
  3. Cheti cha kuzaliwa mzazi (Ninacho cha baba)
  4. Barua ya Serikali ya mtaa
  5. Barua mimi ya maombi ya Passport kwenda kwa afisa uhamiaji mkoa
Wamesema pia Nikishakamilisha vitu vitatumwa Dar ambapo itachukua kama mwezi hivi hadi kupata passport sasa naomba kuuliza kwq mliofuatilia passport kipindi cha hivi karibuni.
[emoji117]Barua ya Serikali za mtaa na baraua yangu ya kuomba passport ni Muhimu au ni huku tu wa mkoani ndio tunaambiwa hivo????
Kama ni lazima niandike barua ya kuomba he inakua katika lugha gani??? Na mfumo wa uandishi wake upoje????

Kwenye site ya uhamiaji wanasema uwe na ushahidi wa safari au ushahidi wa Shughuli anayofanya mwombaji. Je ushahidi huo ni upi?? Na unapatikanaje???

Kama kuna waliowahi kupata passport kutokea huku mkoani nilipo basi naombeni uzoefu wenu tafadhali.

Nawasilisha

Kwenye uzia penyeza rupia mkuu.
Wewe unasubiri mwezi mzima, funga safari njoo Dar ndani ya masaa 4 biashara imekwisha
 
Mkuu sasa hivi tunajaza kwenye mtandao jaza huko uki print ndio unapeleka hivyo vitu Uhamiaji kwani wana maswali ukishajaza na kulipia ni kusubiri passport yako hata wiki au wiki mbili mtu anakwambia nimetoa leo leo kwa laki tatu na safari sio ya leo maana yake nini sasa...
Ok Ahsante mkuu
Je mpaka barua ya mwaliko ndio nitapewa passport au Inawezekana bila barua ya mwaliko
 
Kwenye site ya uhamiaji wanasema uwe na ushahidi wa safari au ushahidi wa Shughuli anayofanya mwombaji. Je ushahidi huo ni upi?? Na unapatikanaje???
Kama HUNA haraka sana, na kama unayo shahada ya kwanza ya chuo kikuu, basi omba kusoma Masters Australia. Kama huna shahada ya kwanza, na umemaliza Form VI, basi omba kusoma shahada ya kwanza Australia. Tafuta vyuo vyenye majina kidogo.

Anyway, kuna baadhi unaweza kukumbana na changamoto ya kuambiwa utume maombi kupitia Wakala.

Australia hawana complocation sana za udahili, na kwahiyo within 2 weeks, na imezidi sana 3 weeks, watakutumia Letter of Offer au Admission Letter.

Ukipata hiyo, Uhamiaji wanakuweka kwenye priority list kama wangekuwa wanzingatia priority.

REMEMBER... Lengo lako sio kwenda kusoma Australia (or any country of your choice) bali lengo lako ni kupata admission letter utakayoitumia kama proof of trip! As a said, Australia hawana kabisa complication... nikiwa nimemaliza second year tu, nilipata admission ya kusoma masters kwenye one of the largest universities in Australia na duniani kwa ujumla!
 
Ok Ahsante mkuu
Je mpaka barua ya mwaliko ndio nitapewa passport au Inawezekana bila barua ya mwaliko
Soma post yangu hapo juu! Kama huna haraka sana, usitumie barua ya mwaliko kwa sababu hii haipo kwenye priority list!
 
Kama HUNA haraka sana, na kama unayo shahada ya kwanza ya chuo kikuu, basi omba kusoma Masters Australia. Kama huna shahada ya kwanza, na umemaliza Form VI, basi omba kusoma shahada ya kwanza Australia. Tafuta vyuo vyenye majina kidogo.

Anyway, kuna baadhi unaweza kukumbana na changamoto ya kuambiwa utume maombi kupitia Wakala.

Australia hawana complocation sana za udahili, na kwahiyo within 2 weeks, na imezidi sana 3 weeks, watakutumia Letter of Offer au Admission Letter.

Ukipata hiyo, Uhamiaji wanakuweka kwenye priority list kama wangekuwa wanzingatia priority.

REMEMBER... Lengo lako sio kwenda kusoma Australia (or any country of your choice) bali lengo lako ni kupata admission letter utakayoitumia kama proof of trip! As a said, Australia hawana kabisa complication... nikiwa nimemaliza second year tu, nilipata admission ya kusoma masters kwenye one of the largest universities in Australia na duniani kwa ujumla!
Utamu unakuja hapo sasa mm ni form four tu. Je hapo si itachukua hata miezi sasa kupata Passport, Nahitaji kwenda Asia sio Europe wala america.
Nimeplan hafi November niwe nimeipata passport
 
Utamu unakuja hapo sasa mm ni form four tu. Je hapo si itachukua hata miezi sasa kupata Passport, Nahitaji kwenda Asia sio Europe wala america.
Nimeplan hafi November niwe nimeipata passport
NO! Sijawahi kuangalia, lakini am sure vile vyuo hata Diploma watakuwa wanatoa!! Hofu yako hapo sio kuwa Form IV, hofu iwe uwezo wako wa kutuma maombi online! Kama unaweza kutafuta vyuo online na kutuma mombi, Form IV yako sio tatizo.
 
Utoehela, kuna jamaa alipata paspot ndani ya siku moja tu lakin alitoa 300k. Kuongeza nguvu utoe hela uwape hao wahusika ufañyiwe haraka bila ya kuzungushwa.

Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app
Lakitatu parefu asee nitavumilia hizo wiki 2
 
Mdoa mada naona analilia lia tu yaani kama upo serious kweli kutoa laki 3 unaona nyingi?mimi hata milioni nikiambiwa natoa endapo safari yangu inaenda kubadilisha maisha yangu!
N:B mtoto wa kiume usipende kuonewa huruma utapoteza marinda
 
Tanzania Ni Ngumu Sana Hii
Yaani Aongeze Nguvu Ya Nini Wakati Kila Kitu Anacho
Kama kila kitu anacho,basi aende nacho hicho hicho huko nje.

Hii nchi sio wewe. Sasa hivi hata polisi wamerudisha mageti barabarani ya kuombea rushwa. Utafikiri wao ndio wenye nchi.
 
Kama kila kitu anacho,basi aende nacho hicho hicho huko nje.

Hii nchi sio wewe. Sasa hivi hata polisi wamerudisha mageti barabarani ya kuombea rushwa. Utafikiri wao ndio wenye nchi.
Mama Anaupiga Nje
 
Ili kupata passport,unatakiwa uwe na.
1.cheti cha kuzaliwa.
2.cheti cha kuzaliwa cha mzazi mojawapo.
3.Kitambulisho cha Taifa.
4.kitambulisho cha Kazi Kwa watumishi wa umma.au barua ya utambulisho KUTOKA serekali za mitaa Kama hujaajiriwa.
5.barua ya maombi ya passport kama uko mkoani anapitisha kwa kamishna WA mkoa kwenda Kwa kamishna mkuu,anwani zao za posta unaweza kuzipata ofisini kwao.
6.uthibitisho wa safari ukionyesha nchi unauokwenda.
7.baada ya kuwa na vielelezo vyote utaanza kujaza form ya maombi online kupitia uhamiaji portal.kuna sehemu uta upload barua ya utambulisho na Cheti cha kuzaliwa.
Kama ombi limekamilika utapewa contral namba ya kulipia 20,000 ili uweze Ku print form.
Ukishaprint form utatafuta mashaidi waijaze na pia mwanasheria.
8.baada ya hapo utaenda ofisi za uhamiaji ukiwa na hiyo form na vielelezo nilivyotaja hapo juu,
9.Ombi litapitiwa kama hakuna dosari,litapitishwa,utalipia 130,000 Kwa kutumia control namba,alafu utakamilisha ombi Kwa kupiga picha pamoja na kuchukuliwa alama za vidole.
10.Baada ya hapo utasubiri Kwa mwezi mmoja passport kuwa tayari.
11.kama unaihitaji Kwa haraka na hauna baadhi ya vielelezo unaweza watumia vishoka,Ila utawalipa gharama za ziada.almost 100-200k.
Mlolongo mrefu sana kama unaomba kuingia peponi qyunamamayake walai
 
Kama HUNA haraka sana, na kama unayo shahada ya kwanza ya chuo kikuu, basi omba kusoma Masters Australia. Kama huna shahada ya kwanza, na umemaliza Form VI, basi omba kusoma shahada ya kwanza Australia. Tafuta vyuo vyenye majina kidogo.

Anyway, kuna baadhi unaweza kukumbana na changamoto ya kuambiwa utume maombi kupitia Wakala.

Australia hawana complocation sana za udahili, na kwahiyo within 2 weeks, na imezidi sana 3 weeks, watakutumia Letter of Offer au Admission Letter.

Ukipata hiyo, Uhamiaji wanakuweka kwenye priority list kama wangekuwa wanzingatia priority.

REMEMBER... Lengo lako sio kwenda kusoma Australia (or any country of your choice) bali lengo lako ni kupata admission letter utakayoitumia kama proof of trip! As a said, Australia hawana kabisa complication... nikiwa nimemaliza second year tu, nilipata admission ya kusoma masters kwenye one of the largest universities in Australia na duniani kwa ujumla!
Wa fom foo mkuu tunafanyaje hapo?
 
Mdoa mada naona analilia lia tu yaani kama upo serious kweli kutoa laki 3 unaona nyingi?mimi hata milioni nikiambiwa natoa endapo safari yangu inaenda kubadilisha maisha yangu!
N:B mtoto wa kiume usipende kuonewa huruma utapoteza marinda
Naona unahalalisha rushwa. Wewe unaona ni sahihi kulipia kitu ambacho ni halali yako kukipata baada ya kutoa ghalama zake??
 
Wa fom foo mkuu tunafanyaje hapo?
Tafuta chuo chochote nje ya nchi kinachoweza kuku-admin kwa kozi ya diploma au hata certificates. Hivyo vyuo, vipo. Jitahidi kutafuta vyuo vyenye majina kidogo! REMEMBER, mbele hawana complications kama za Bongo!
 
Back
Top Bottom