Msaada wa Mawazo: Hapa panafaa kujenga?

Kwa muonekano wa ujumla wa picha, hilo eneo linaonekana liko poa sana, tambarare fulani hivi iliyonyooka fresh. Sijaona dalili yoyote ya kuashiria kuja kujaa maji. Nakushauri ununue tu.
 
Jenga kama ni njia ya maji yape njia ya kutokea. Tafuta fundi mzuri na mzoefu atakupa ushauri na utajenga vizuri tu hapo.

Ingekuwa eneo liko karibu na bonde la mto au kijito au kweye mporomoko nisingekushauri ujenge ila slope ya hapo ni ya kawaida sana
 
Tembelea maeneo kama Makongo Juu, Goba, Madale, Salasala, Mivumoni, Kimara, Mbezi ya Kimara, Kibamba kupata maeneo yaliyo tambarare ni nadra, maeneo mengi sehemu hizo ni miinuko na slope kama hapo au zaidi na watu wamejenga nyumba za maana tu
 
Ahsante
 
Hapo mbona pako wazi kabisa kuwa ni center ya maji kwa eneo Hilo ila sikuvunji moyo lakini kuwa makini na mtu anaitwa "rafiki"
 
Kiwanja chako kipo chini ukilinganisha na kule kwa jirani zako, sasa angalia jinsi ya foundation ya jirani kule jinsi ilivoinuka halaf kuanzia hapo utapata jibu la swali lako
 
simpo mbn.
uliza hao majirani hapo watakupa mkanda mzima wa hapo fullstop,

sasa kama ww ni wale wa kufunga vioo na ki-ist chako itakula kwako mazima
 
nenda katembelee mkuu, wakati sahihi wa majibu ndo huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…