Msaada-Watoto wetu(ndugu)wametiana mimba

Du chances hapo wote wa nusu ya genes za mama zao, si sawa na baba mmoja mama mmoja. Anyway yameshatokese. Kimila mnatakiwa kuchinja mnyama kwenye kaburi la babu ili kuua undugu ili waweze kuoana.
Ili iweje sasa so kila wakitiana mimba wachinje?
 
Du chances hapo wote wa nusu ya genes za mama zao, si sawa na baba mmoja mama mmoja. Anyway yameshatokese. Kimila mnatakiwa kuchinja mnyama kwenye kaburi la babu ili kuua undugu ili waweze kuoana.
kuua undugu??😳
 
Hao sio ndugu. Ndugu ni wale waliozaliwa baba na mama mmoja. Hao ni cousins tena jamii za kiislam huwa wanaoana kabisa. Wa ba mdogo,wa shangazi wanaoana bila tatizo.
yeah ila kwenye genetics kuna chances za kuwa na matatizo, tabia hizo wanazo sana familia ya Rothschild kama umefatilia utaona kuna watoto (baadhi) walizaliwa hivyo sababu ya kuoana ndugu
 
ila kutoa mimba sio kosa la jinai?
 
ila kutoa mimba sio kosa la jinai?


Kutoa mimba kwa sababu za kimsingi imeruhusiwa, mfano kama mimba itasababisha mama kupoteza maisha hapo sio kosa kuitoa au kama mimba itaonekana kupitia vyombo kama ultra sound nk, inayomapungufu (abnormality) hapo inaruhusiwa kuitoa, kuna mapungufu na madhara mengi yanayoweza kuletwa kwa mama kupata ujauzito-- madhara kwa mama au kwa mtoto akiwa tumboni.

Shida kubwa iliyopo kwenye jamii (stereotype) ni kwamba wana generalize kuwa kutoa mimba ni dhambi ya uuaji, wanasahau kwamba mimba inapokuwa tumboni inakuwa ni sehemu ya mwili wa mama na haina maisha yake pekee (an independent life). Kuua ni hali ya kutoa uhai wa nafsi inayojitegemea yenyewe nje ya uhai wa kitu kingine. (Out of host life).

Kifupi kutoa mimba kwa sababu za msingi imeruhusiwa-- na kutoa mimba inaweza ikawa ni kosa lakini sio kosa la mauaji kama ilivyozoeleka katika jamii.
 
Kwan walikua wanaishi nyumba moja!!
 
Du chances hapo wote wa nusu ya genes za mama zao, si sawa na baba mmoja mama mmoja. Anyway yameshatokese. Kimila mnatakiwa kuchinja mnyama kwenye kaburi la babu ili kuua undugu ili waweze kuoana.
Hii mila ni ya kabila gani best?
 
tunaongelea hili lililotokea hapa, watoe mimba kisa ni ndugu wamekutana kimwili?? ni sababu ya kuua kiumbe aliyeko tumboni? kahatarisha maisha ya nani mpaka wamtoe? wangefundishwa kuzuia tamaa ama kujikinga na mipira yangetokea? na kama walifundishwa na hawakutii hayo mtoto hayamhusu! acha wazae maisha mengine yaendelee
 


Lakini unaelewa ninachosema??,

Hao ni ndugu wa damu wamekutana na kupeana mimba, je unajua ni madhara gani yanayoweza kupatikana kwa ndugu wa DAMU kupata mtoto??, jifunze kwanza hilo ndipo uje na utetezi kwa hoja yako.

Kutoa mimba siyo kuua, tafuta maana ya kuua halafu uje kutetea hoja yako.
 
hilo swala la ndugu na matatizo yake tunayajua ila wapo wengi wamezaliwa kwa mama mdogo na baba mkubwa (mashariki ya kati ni kawaida ili mali isiende mbali) ila sio sababu ya kutoa, wamejiingiza kwenye vitendo vya uzalishaji wa binadamu sheria ya nature inachukua mkondo wake (kupatikana mtoto) basi ndo hivyo - kingine unaposema kuua ni mpaka kitu kiwe nje kwenye macho yako unayoyaona? mtoto aliyeko tumboni nae ni kiumbe hai, ni MTU YULE (Murder is the unlawful killing of another human without justification or valid excuse, especially the unlawful killing of another human being with malice aforethought.) - kosoa
 
Hao kwa mila ya kiislam, km ni mtoto wa baba mkubwa na baba mdogo wanayo haki ya kuonana
 


Mimba inapotolewa kwa sababu yoyote ile kitendo hicho sio mauaji, kumbuka mimba siyo mtoto, mtoto ni yule aliyezaliwa ambapo ukimtoa uhai mara baada ya kumzaa au hapo baadaye hapo ndipo kitendo cha uuaji kitakuwa kimefanyika, lakini mimba (zygote) ambayo bado inategemea supply ya chakula na hewa kutoka kwa mama hiyo mimba inakuwa ni sehemu ya mwili wa mama na hapo anakuwa na hiyari ya kuitoa au laa.

Mimi niliposema mimba ya hao wana ndugu itolewe nilikuwa na hoja hii (ambayo umeikubali) kwamba watu wa damu moja wakizaa basi madhara ya kiafya mara nyingi hutokea katika watoto wanaozaliwa, sasa it would be inhuman to procreate a congenitally defective offspring deliberately while for sure you knew it would be suffering its entire life, forget about your suffering, as parents, from its upbringing. -- spending time, money and resources in its catering, something you knew before giving birth.

Na ndiyo maana leo kuna ultrasound, MRI nk, vyombo vya uchunguzi na elimu ya tiba na katika genetics ni kubwa kuweza kujua madhara mbalimbali ya kiafya hata kabla mtoto hajazaliwa sasa tutaishije kama watu wa karne ya 15??.

Wataalamu wa wanyama veternary doctors wanapohamilisha (insemination) wanyama ili kupata uzao bora usiokuwa na kasoro huchukua mbegu kutoka dume mwingine kabisa na wala sio dume kutoka katika ukoo uleule na hii ni kuepusha madhara ya kigenetic na magonjwa ya kurithi, sasa why should it be exceptional to humans as they are technically like animals in the case??!!--sasa itakuaje sisi tuishi tu kwa kujamiana hovyo kuliko hata hao wanyama tunao wa treat decently !!😁😁
 
Hao kwa mila ya kiislam, km ni mtoto wa baba mkubwa na baba mdogo wanayo haki ya kuonana


Mila gani za kiislamu??, toa ushahidi watu wa damu moja wanaweza kuoana?? Usichangane kati ya UARABU na UISLAMU.
 
sehemu ya mwili wa mama...au anakuwa parasite kwa host ambaye ni mama???? halafu post umesoma vizuri kuwa mtoto wa baba mkuwa na baba mdogo au umesahau hiyo part??? we nahisi ni dokta wale wanaosafisha wasichana wetu vyuo vikuu mimba zao...kaazi kweli kweli!! haya watoe kakaaa mimba sio mtu ni mnyama wa dizaini ingine kabisa (ila navyojua zygote ni binadamu kama binadamu wengine regardless anaishi wapi iwe tumboni iwe kwenye chupa au awe hapa) ni sawa na yai la kuku ambalo limesharutubishwa - yule ni binadamu ambaye hajakamilika bado yuko kwenye stage ya kulekea kwenye ukamilifu, nilichotolea maoni wote hapa tunajua repercussion zake za kuwa wa damu moja kuna kuwa na probability ya genetics mutation ila sasa si wameshaji engage kwenye sexual activity inayotengeneza watoto waachwe wazae! wasiwatoe ila kwa mawazo hayo unaweza kula nyama ya katoto ambako bado hakajakamilika ila wakakatoa sio bure ... 😁😁😁😁😁😁
 


Unaelewa maana ya parasite??, mfano minyoo ndani ya tumbo ndiyo parasite lakini siyo "Zygote", zygote ni sehemu ya mwili wa mama kwa sababu mama naye amechangia to its makeup.

Kutoa mimba unaweza kama ukipenda kuita ni "crime" lakini si kosa la mauaji, kutoa mimba ni sawa na mtu kukata kidole chake chenye kansa au kisichokuwa na kansa.

Zygote ni mtu asiyekamilika na wala siyo "binadamu" asiyekamilika, kwa sababu maendeleo ya kukua kwake yanategemea mtu/binadamu mwingine ambayo anayo mamlaka kamili juu yake.

Mtoto anapozaliwa hapo anakuwa ni "independent person" na anazo haki zote kama mtu kamili na hapo ukimuua utakuwa na hatia ya kuua.

Kuhusu kula "zygote" hiyo ni canibalism, ni sawa na kula viungo vya mtu-- ni mwehu yule anayefikiria such a nasty stupid deed let alone committing the deed.

Kuoana ndugu watoto wa "Ami" ni mila za waarabu, katika historia koo na makabila ya waarabu waliishi kwa uhasama na vita kwa muda mrefu hivyo hata kuoleana kati ya makabila ilikuwa ni taabu au ilikuwa ni katika kulinda "ujasiri" na ufahari wa koo zao ndiyo maana wakaoleana wao kwa wao, sasa siwezi kuwakataza watu kuiga mila za aina hii ila ninachoweza kufanya ni kutoa tahadhari juu ya " diverse repercussions" zake na kwaambia kuwa mambo hayo ni mila za waarabu na kisayansi ni jambo hatari kwa wazaliwa (offsprings).
 
Kaini alimla nani mpaka kizazi kikaendelea kama sio ndugu yake? Kuzalishana ndugu inakataliwa ili kuzuia magonjwa ya kurithi yasiendelee kutafuna ukoo na pia ingekuwa halali kuoa ndugu yako tungelazimishana kuoa dada zetu ambao wapo wanazeekea nyumbani kwa sababu mbalimbali mfano(hana kishuzi,miguu kama miwa,ugly face n.k)
 
Hakuna shda hapo,mtoto atazaliwa yuko salama kabsa,tatzo ingekuwa baba mmoja na mama mmoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…