Msafara wa Raisi (Presidential Motorcade) kukosea njia! Hii imekaaje kiusalama?

Ni hatari kwa kweli ukiachana na mawasiliano basi hata ramani wameshindwa Kuwa nayo pia hivi Mishangingi kama ile inakosa TV pale mbele inayoonyesha Ramani!!!....
Sisi baaado sana

'HOW MUCH IS TOO MUCH?'
Inaitwa GPS mkuu..umenena vema!
 
Trafiki nao hawakuwepo kuonyesha njia msafara unakotakiwa kwenda?!
 
apo kweli uzembe umefanyika lakini kiusalama sidhani kama kuna shida kwani rais wetu tumeshudia akiwa kwenye msafara anaweza akasimamisha msafara ghafla na kuwasalimia au kusikiliza kero za wananchi wa eneo flani ikiwa ata ratiba ya kusimama kwa eneo hilo haikuwepo, au wananchi wenyewe wanasimamisha msafara wa rais ghafla na rais anasimama kusikiliza kero zao. ulinzi wake uko makini istoshe tz hatuna historia ya matukio mabaya kwa viongozi.
 
Si bora huu msafara ulio kosea njia kuliko ule wa Jk ambapo tairi ya gari yake ilichomoka
 
tupe maelezo mkuu ilikuaje baada ya kukosea na kuelekeza msafara kusiko sahihi?
sio kwamba walipotea njia, huwa wanawasiliana na watu wao wanaokuwa njiani bara bara yote msafara unapopita. Kama wameona kitu wakakitilia mashaka huwasiliana na gari ya mawasiliano na uwezekano wa kubadilisha route unakuwepo. inawezekana hawakuelewana kwa sekunde chache na ma observer wao wanaocheki mienendo ya huko mbele wanakoenda
 
Si bora huu msafara ulio kosea njia kuliko ule wa Jk ambapo tairi ya gari yake ilichomoka
Hii story niliisikia kwenye kijiwe flani cha kahawa kurasini mitaa ya diplomasia kule. Hii ilikuwaje?

Muhusika wa usafiri hanaga records za matengenezo ya magari Yale Au? Na gereji ya hayo magari ni wapi?
 
Hii story niliisikia kwenye kijiwe flani cha kahawa kurasini mitaa ya diplomasia kule. Hii ilikuwaje?

Muhusika wa usafiri hanaga records za matengenezo ya magari Yale Au? Na gereji ya hayo magari ni wapi?
Mkuu, yule mheshimiwa kipindi chake cha pili aliandamwa na majanga sana. Hukusikia hata mkoani Mbeya kuna sehemu walimrushia mawe ikabidi abadilishiwe gari haraka sana? Hiyo ya kuchomoka tairi ilitokea Mwenge pale
 
Mkuu, yule mheshimiwa kipindi chake cha pili aliandamwa na majanga sana. Hukusikia hata mkoani Mbeya kuna sehemu walimrushia mawe ikabidi abadilishiwe gari haraka sana? Hiyo ya kuchomoka tairi ilitokea Mwenge pale
Dah noma kweli, najaribu kuwaza hapa Kama wipii aliekosea msafara alifukuzwa kazi sipati picha huyo anaehusika na kitengo cha usafiri wake kilimtokea nini..bila kusahau fundi mkuu wa magari Yale ilikuwaje! Maana speed ya ule msafara mmh..lazima wahusika wahakikishe ubora na usalama wa magari Kabla ya Safari.

Alitokaje Kama tairi ilichomoka kabisa?
 
nimekumbuka mwaka fulani msafara wa jk tarime, polisi alielekeza visivyo alikamatwa na usiku huohuo alijipiga risasi akafa
 
Trafiki mgeni bunduki ataitoka wapi? Acheni mzaha
Ndugu wale Traffic wanaosimama njia panda kuonyesha uelekeo wa msafara sio wageni, bali ni wenyeji wa eneo husika. Wewe labda unaongelea Rider (Pikipiki) ambaye anakuwa ametoka mkoani au wilayani, hivyo hutegemea maelekezo kutoka kwa askari/trraffic wanaokuwa njiani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…