Msajili: Nafuatilia kwa karibu sana Uchaguzi wa Viongozi CHADEMA kuhakikisha haki inatendeka na Katiba kufuatwa

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Mutungi amesema anafuatilia kwa makini sana uchaguzi wa viongozi wa CHADEMA kuhakikisha katiba inafuatwa na haki inatendeka kwa wagombea wote.

Msajili amesema endapo katiba itakiukwa kwa makusudi basi uongozi utakaochaguliwa utakuwa ni batili na hatautambua.

Chanzo: Gazeti la Jiji

Maendeleo hayana vyama!
 
ha ha ha, dunia ina mambo ishi ushuhudie mengi
 

Tena ili afuatilie vizuri anatakiwa akahesabu kura. Akiona yeye mwenyewe hataweza amuombe Magufuli wakahesabu wote.
 
Huyu msajili vipi??

Aingilie kwanza uchaguzi wa serikali za mitaa, ambao hata mtu aliye kipofu ameona namna ulivyokuwa siyo wa haki na huru
 
Kwanini wanaccm wanahangaika sana na uenyekiti wa Mbowe kuliko uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu!
Lakini inaonesha maelekezo aliyopewa ni kutowatambua viongozi watakaochaguliwa endapo waccm hawatashinda.
Msajili ni mwanaccm?!
 
Huyu msajili vipi??

Aingilie kwanza uchaguzi wa serikali za mitaa, ambao hata mtu aliye kipofu ameona namna ulivyokuwa siyo wa haki na huru
Uchaguzi wa serikali za mitaa unasimamiwa na Tamisemi bwashee!
 
Yaani wametafuta kila mbinu ya kiufuta Chadema wanashindwa......

Ndiyo hasira zote hizi za msajili wa vyama vya siasa!

Hivi hajauona uchaguzi wa serikali za mitaa namna ulivyogeuzwa UCHAFUZI, ndiyo amekuja kuushupalia uchaguzi huru na wa haki wa Chadema??

Hakika sasa ameamua kuweka wazi kuwa yeye anatumika na Jiwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…