Msajili wa Vyama vya Siasa: Nitavifuta CHADEMA na CUF

Msajili wa Vyama vya Siasa: Nitavifuta CHADEMA na CUF

assadsyria3

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2013
Posts
6,905
Reaction score
4,054
Msajili wa Vyama vya Siasa, amedai wote watakao kiuka kuvunja vikundi binafsi vya ulinzi vya vyama hivo atavifuta.

Amedai kama Katiba zao zinatambua jambo hilo walifanyie mabadiliko haraka.

Tamko hill limetolewa kwa ushirikiano wa IGP Mangu kwa niaba ya Jeshi la polisi na ofisi ya msajili.


My Take.

Niwazi kwa ubishi wa CHADEMA bila shaka kitafutwa katika medani za siasa.

=========================================


Dar es Salaam. Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi amevitaka vyama kurekebisha katiba zao kwenye kipengele kinachoruhusu kuanzishwa kwa vikosi vya ulinzi na usalama.

Vyama vyenye vikosi cha ulinzi na usalama ni Chadema chenye Red Brigade, CCM (Green Guard), CUF (Blue Guard) na sasa ACT-Wazalendo (ACT Amani).
Mutungi alisema uanzishwaji wa vikundi hivyo unakwenda kinyume na Katiba ya nchi inayolipa jeshi la polisi mamlaka ya kulinda usalama wa raia na mali zao.

Akizungumza baada ya mkutano wake na vyama hivyo jana, Jaji Mutungi alisema katiba za vyama vingi vilivyosajiliwa kabla hajaingia ofisini vilikuwa na kifungu kinachoruhusu kuanzishwa kwa vikosi vya ulinzi na usalama wa mali za chama au viongozi wao wawapo katika mikutano.

"Haturuhusu kifungu hicho kuwapo kwenye katiba za vyama vinavyosajiliwa sasa (hakugusia ACT - Wazalendo). Hatuvifundishi vyama vya siasa namna ya kuandaa katiba zao lakini tunasimamia kifungu hiki kwa vile kinapingana na sheria."

Jaji Mutungi alisisitiza kuwa vyama vya siasa nchini havina uelewa wa sheria ya vyama vya siasa ambayo ndiyo inayovisimamia, ndiyo maana vinashindwa kuendesha shughuli zao kwa mujibu wa sheria hiyo.

Kauli ya polisi
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Ernest Mangu alisema watapambana na vikundi vya ulinzi na usalama ndani ya vyama vya siasa wakati wa Uchaguzi Mkuu endapo vitaingilia majukumu ya jeshi la polisi.

Alisema uanzishwaji wa vikundi hivyo ni kinyume cha sheria inayolipa Jeshi la Polisi dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao.
Alisema vikundi hivi vilianzishwa kama chipukizi au halaiki lakini baadaye vilikuwa na kubadili malengo na kuanza kuingilia majukumu ya polisi na kuhatarisha amani.

Maoni ya wadau
Hata hivyo, kauli za Msajili na Mangu zilipokewa kwa hisia tofauti na viongozi wa vyama hivyo na baadhi vikiweka wazi kuwa havipo tayari kuachana na vikundi hivyo.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM – Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema vijana wa Green Guard hawaandaliwi kijeshi na kuwa tishio kama vyama vingine, bali kuwafanya wawe vijana bora, wakakamavu na kuwajengea uzalendo ndani ya nchi yao.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema chama chake hakipo tayari kuivunja Red Brigade huku akiilaumu CCM kuwa kikundi chake cha Green Guard kimepata mafunzo ya kijeshi kikifundishwa na askari tofauti na wao ambao wanafundishwa na raia.

Akihutubia mkutano wa hadhara mjini Nzega jana, Mbowe alisema suluhisho la tatizo hilo haliwezi kuwa sheria bali kuhakikisha haki inatendeka na inaonekana kutendeka kwa kila chama, akitolea mfano jinsi viongozi wa chama hicho walivyopigwa na Green guard bila polisi kuchukua hatua.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM – Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema vijana wa Green Guard hawaandaliwi kijeshi na kuwa tishio kama vyama vingine, bali kuwafanya wawe vijana bora, wakakamavu na kuwajengea uzalendo ndani ya nchi yao.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema chama chake hakipo tayari kuivunja Red Brigade huku akiilaumu CCM kuwa kikundi chake cha Green Guard kimepata mafunzo ya kijeshi kikifundishwa na askari tofauti na wao ambao wanafundishwa na raia.

Akihutubia mkutano wa hadhara mjini Nzega jana, Mbowe alisema suluhisho la tatizo hilo haliwezi kuwa sheria bali kuhakikisha haki inatendeka na inaonekana kutendeka kwa kila chama, akitolea mfano jinsi viongozi wa chama hicho walivyopigwa na Green guard bila polisi kuchukua hatua.

Chanzo: Mwananchi
 
Kitengo kingine cha Maintarahamwe AKA MACCM kikitumika vizuri kuelekea kwenye kura ya maoni na uchaguzi Mkuu. Kati ya CHADEMA na Mainterahamwe sijui ni yupi alianza kuwa na vikundi binafsi vya ulinzi.
 
"KAMA katiba zao zinaruhusu wazifanyie marekebisho"...

Ina maana huyu msajili hajawahi kuzisoma hizo katiba. Sasa huwa anaenda ofisini kila siku asubuhi hadi jioni kufanya nini!
 
Aanze na ccm wafute chipukizi na wengine watafuata hiyo ni njia ya kuzuiya uhuru wa vyama kulinda wizi wa kura na kwanni hili limetangazwa muda mfupi tu kuelekea uchaguzi?tunamashaka sana na msajili na mangu wana ajenda ya siri ambayo ipo wazi kwamba wana njama za kuibeba ccm.
 
Kishapewa muongozo toka Lumumba Mkuu Tuko abwabwaje hadi kutoa povu kuhusu issue hii.

"KAMA katiba zao zinaruhusu wazifanyie marekebisho"...

Ina maana huyu msajili hajawahi kuzisoma hizo katiba. Sasa huwa anaenda ofisini kila siku asubuhi hadi jioni kufanya nini!
 
Last edited by a moderator:
GREEN GUARD ya MACCM vp??!! Wale si ndio wanafanya magwaride huku wakiwa na bunduki kabisa??!!

Green Guard wanatumiwa kwenye sherehe zao mbele ya raisi na mawaziri na jeshi la polisi likishangilia na tena wakiwemo watoto wadogo wanaopewa bunduki,CCM mnaita Chipukizi-chipukiziwa ujambazi au ufisadi,mbona mmekaa kimya??!!
 
msajili amedai wote watakao kiuka kuvunja vikundi binafsi vya ulinzi vya vyama hivo atavifuta. amedai km katiba zao zinatambua jambo hilo walifanyie mabadiliko haraka. tamko hill limetolewa kwaushirikiano wa igp Mangu kwa niaba ya jeshi la polisi na ofisi ya msajili.
my take
niwazi kwa ubishi wa chadema bila shaka kitafutwa katika medani za siasa

chanzo.RFA magazeti

Cdm kama ingekuwa ni mwanamume basi unge hatarisha ndoa yake
 
msajili amedai wote watakao kiuka kuvunja vikundi binafsi vya ulinzi vya vyama hivo atavifuta. amedai km katiba zao zinatambua jambo hilo walifanyie mabadiliko haraka. tamko hill limetolewa kwaushirikiano wa igp Mangu kwa niaba ya jeshi la polisi na ofisi ya msajili.
my take
niwazi kwa ubishi wa chadema bila shaka kitafutwa katika medani za siasa

chanzo.RFA magazeti

Mutungiphobia loading...........futa uone moto wake!
 
GREEN GUARD ya MACCM vp??!! Wale si ndio wanafanya magwaride huku wakiwa na bunduki kabisa??!!

Green Guard wanatumiwa kwenye sherehe zao mbele ya raisi na mawaziri na jeshi la polisi likishangilia na tena wakiwemo watoto wadogo wanaopewa bunduki,CCM mnaita Chipukizi-chipukiziwa ujambazi au ufisadi,mbona mmekaa kimya??!!

Mkuu huyo mutungi na mangu hawana ubavu wa kulazimisha cuf na cdm kufuta hivyo vikundi bila kuvifuta kwanza green guard hapo ndio patachimbika
 
"KAMA katiba zao zinaruhusu wazifanyie marekebisho"...

Ina maana huyu msajili hajawahi kuzisoma hizo katiba. Sasa huwa anaenda ofisini kila siku asubuhi hadi jioni kufanya nini!

Hayo ndio maajabu ya msajiri. Katiba zote anazipitisha yeye sasa anauliza nini? This means anajua kwamba katiba zao zina accomodate kitu hicho ndio maana anasema wafanye marekebisho.
Hivi yeye kama msajiri si anajua process za kurekebisha katiba? Anataka warekebishe kisirisiri? Je atawapa gharama za kuitisha vikao vya kurekebisha katiba?

Kama katiba zao zina accomodate kitu ambacho kina kwenda kimyume na katiba ya nchi na yeye ndiye alizipitisha nani wa kuwajibika zaidi yake?
 
Msajiki Mutungi na Mkuu WA Polisi Mangu, vipi chama kikiunda kikosi cha mbwa katika kujilinda? Nauliza hivi kutokana na kukaa kwenu kimya kuhusu kuanzishwa kwa kikosi cha ulinzi cha mafisi na CCM. Je hamuoni hatari kwa watu kushambuliwa na manyang'au kwenye mikutano ya kampeni.

CCM ilianzisha kikosi cha kigaidi cha Green Guard mkakaa kimya, wakaanzisha kikosi cha mafisadi na wezi mkakaa kimya, wakaanzisha kikosi cha mafisi mkakaa kimya...je tuwaeleweje? Kwa nini polisi wameshindwa kuithibiti CCM?
 
Ha!Ha!Ha!Ha!, naona ccm wameamua kuibuka na njia mpya ya kutoa maagizo kwa mtungi,afute cdm na cuf aone moto utakavo waka.
 
msajili amedai wote watakao kiuka kuvunja vikundi binafsi vya ulinzi vya vyama hivo atavifuta. amedai km katiba zao zinatambua jambo hilo walifanyie mabadiliko haraka. tamko hill limetolewa kwaushirikiano wa igp Mangu kwa niaba ya jeshi la polisi na ofisi ya msajili.
my take
niwazi kwa ubishi wa chadema bila shaka kitafutwa katika medani za siasa

chanzo.RFA magazeti

Mkuu huu ni uongo usiokua na maana!Hizo habari si za kweli ni kujaribu kupotosha kauli sahihi aliyoitamka msajili.Fuatili kwa makini na uisome habari hiyo uone jinsi ambavyo vyombo vyetu vya habari vinatumika, Waandishi wamekua makanjanja kuhangaikia matumbo yao tu.Jana siku ya Alhamisi nilisikiliza mwenyewe kwa masikio yangu kauli aliyoitoa msajili kupitia redio ya VOA alichokisema,Alichokisema ni kwamba ni halali kikatiba kua na vikundi vya ulinzi katika vyama lakini visiwe na mwelekeo wa kuunda jeshi,akamalizia na kusema kua vyama vyenyewe vikae na kupitia katiba za vyama vyao na visivuke mipaka ya kikatiba.Sikusikia popote akisema kua atavifuta vyama tusipende kukuza mambo kumsingizia msajili.
 
hqdefault.jpg

Green Guard Zanzibar ni Imara zaidi ya Chuma.​
images
 
haiingii akilini kuwa hawajawahi kusoma katiba za hivi vyama vya siasa na sheria ya vyama vya siasa kiujumla,vipi kuhusu vijana chipukizi wa chama tawala or green guard,je nao watahusika au itakua double standards?
 
walinzi wao wenyewe na malipo ni yao wenyewe kinachowauma nini? Polisi ingebidi ivishukuru vyama kwa kuwa wabunifu na kuweka ulinzi kwy mikutano kusaidiana na polisi kudhibiti usalama wa watu na mali zao kwani kazi hiyo kutokana na uchache wa polisi hawana uwezo wa kudhibiti kila mikutano na tumeshasikia mara nyingine mikutano ikiairishwa kisa hakuna polisi kwahiyo vyama viendelee kutumia walinzi wao kujilinda ni dhana nzuri. kama mimi mtu mmoja na familia tuna walinzi wa kulinda nyumbani kwangu itakuwa mkutano mzima ambao unajaza mamia ya watu .

otherwise mkingangnia tutajua munataka wasiwe na walinzi ili ccm itume wahuni kufanya vurugu bila kudhibitiwa mmechelewa.
 
Back
Top Bottom