Msanii Aliyeimba Bongo bahati mbaya hakukosea, Ulaya kuzuri Sana

Error 404

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2022
Posts
2,151
Reaction score
3,493
Hivi ni kipi kinawazuia hawa waliojiita ni wakimbizi wa Kisiasa wasirudi Tanzania ?

Naona wanaona kama waliishi Bongo kwa Bahati mbaya tu ila kwa uzuri wa huko Ulaya ni bora waendelee kuishi huko .

Ni wakati muafaka kwa Tundu Lissu na Lema watupe sababu ya kueleweka kwanini hawarudi
 
Dunia ni kijiji
 
Kuishi na watu civilized pana raha yake sema tu tamaa na kiherehere cha wapigania UHURU ndio imetufikisha hapa pa hovyo.
 
Bongo hii ngumu sana! Wajinga wengi wamepewa nafasi hawana sifa nazo na kuna wengi wana maarifa na hawapewi nafasi! Mimi nadhani Lissu na Lema hata wakitokomea huko mazima bado ni sawa tu!
 
Bongo hii ngumu sana! Wajinga wengi wamepewa nafasi hawana sifa nazo na kuna wengi wana maarifa na hawapewi nafasi! Mimi nadhani Lissu na Lema hata wakitokomea huko mazima bado ni sawa tu!
Na hivi salio limesoma wataishi kwa raha sana
 
Kichwa cha habari kingine habari nyingine...kweli ww ni error
 
Ulaya ni ulaya tu,uwezi kulinganisha na bongo,
Kuna wale Islamic fundamentalist,wenye imani kali,huwa wanahubili ukristo ni mbaya sana,lakini wakati huo wanaishi USA,UK,Austaria,natherand,nchi za kikristo,hawathubutu kwenda kuishi kwa waislam wenzao,Saudia,Qatar,misri,
Ulaya imejengwa,mifumo inafanya kazi,ukipiga kazi,inakulipa,hakuna janja janja.
Bongo hapa,huduma za jamii shida,huwezi kuchukua maji ya Bomba ukanywa!utaugua typhoid mpaka ukome,
 
Sababu umeshatoa kwamba ulaya pazuri sana bongo bahati mbaya. Sasa unataka sababu gani Tena?
 
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kuishi na watu civilized pana raha yake sema tu tamaa na kiherehere cha wapigania UHURU ndio imetufikisha hapa pa hovyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…