Aisee!Noma sana. Nilikuwaga na crush kwa huyu manzi enzi hiyo bado niko chalii hivi. Lord Eyes hii dhambi inakuhusu arif.
I
Labda jela.dawa pekee ni kukaa sehemu ambayo atakuwa hapati madawa, iwe jela au popote pale
Kijijini kwetu ni Masaki na sina ndugu wa kumlilia wote mambo yao ni mazuri.
Kawa teja ni matokeo.M ntaanza NA maombi...kwavideo niloona tunakazi mbelekubwa kumkomboa kubwasana lakini tusikate yatamaa..wenye instagram mnaweza search globapublishers AMA obbytheng mtamwona anavyochopolewa NA poliisi usiku mawindoni
Mkuu akati anaendelea na tiba mwananyamala anawahamasisha kina TID, chid, alipokuwa akitoka pale anarud kwenye kijiwe chake, mwisho wa siku alipasua kioo cha docta wake.Nadhani huelewi maana halisi ya 'addiction'. Mtu ambaye yupo addicted hayo mawazo kama yako inakuwa magumu kuyapata. Anaweza akawa ana nia lakini nia pekee itafeli. Hawa watu wanahitaji msaada ili watoke kwenye mtego wa addiction. Wanahitaji uangalizi wa hali ya juu, mwenyewe hawezi.
Na njia kuu ya kuwasaidia watu kama Ray C na mateja wengine ni kupambana na wafanyabiashara wakubwa wa madawa ya kulevya pamoja na wasambazaji wao.
Mleteni kwangu ni mlee ataacha tu na alivyonona... uwiiiMsanii wa muziki Rehema Chalamila aka Ray C usiku wa jana alikamatwa na jeshi la polisi maeneo ya Kinondoni Manyanya almaarufu ‘Kinondoni kwa Mpemba’ jijini Dar es salaam baada ya kupiga makelele barabarani akidai anataka kutekwa.
Ray C akiwa kwenye gari la polisi
=================
More:
Hali ya kiafya ya mwanamuziki mkongwe Rehema Chalamila ‘Ray C, imeonesha kuwa tata kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni matumizi ya madawa ya kulevya jambo lililoleta sintofahamu baada ya video inayozunguka mitandaoni ikionyesha akichukuliwa na Polisi huku akisema kuwa wanamteka.
Habari zinadai kuwa mama yake mzazi amekuwa akikesha kumtafuta mrembo huyo kutokana na kuzama kwenye vijiwe vya mateja wa madawa hayo na kushindwa kuonekana nyumbani kwani kwa siku kadhaa na watu kujitokeza kumsaidia bila mafanikio.
Sambamba na hilo siku za hivi karibuni mwanamuziki Jay Dee, alionekana kuwa naye karibu na kudai kuwa Ray C, anahitaji marafiki wazuri na watu wavumilivu kuweza kumsaidia kwani kumlaumu pekee hakuwezi kumjenga bali ni kumzidi kumharibu kisaikolojia.
Mmoja wa wasanii wa Bongo Movie, Esha Buheti, kupitia mtandao wa kijamii ameweza kueleza jinsi gani alivyoguswa baada ya kumuoa Ray C akiwa chini ya ulinzi wa polisi akiwa hajitambui na kuongea maneno yasiyoeleweka na kudai kuwa awali alijua mrembo huyo anasingiziwa tuu.
Ameandika “Nashindwa hata niongee nini jamani, Ray C leo Kinondoni umenitoa machozi, jamani tufanye kitu tumsaidie Ray C, I mean it jamani siku zote nlikuwa najua anaonewa ila nilichokishuhudia leo nimeumia kutoka moyoni amedhalilika mwanamke mwenzetu, jamani tufanyeje?”
Akaendelea “Nilikua na Kabula, Kinondono kwa wapemba tumefuata chips mara tukasikia mtu anasema me Ray C nataka kuvua nguo, nikajua utani kushuka ni Ray C anasema nishikeni kuna watu wanataka kuniteka, alikuwa na nguvu sana watu kumshika akaanza kuongea vitu havieleweki, akaanza kutafuta kisu ajichome, watu walimzuia sana walishindwa akaanza kugaragara kwenye matope akipiga kelele,”
“Kiukweli nilijikuta nalia mara ikaja gari ya polisi ikambeba ila kwa tabu sana alikua akipiga kelele jamani nisaidieni msiniache kiukweli mpaka Ray C anaondoka na ile gari ya polisi sikujua anapelekwa wapi alikuwa kama mtu alopata kichaa, YARRAB TUNAMSAIDIAJE RAYC?”.
Mange nimekupenda gafla popotee ulipo umekuwawazi siokama wanafiki wengine humu wanasema apotezewe wakisikia Kafa wanakuja namakotiyaoo wakwanza kuweka shahada huku macho mekundu wamekulandumu wakituaminisha wanalia..tushauriane anasaidiwajeeNimeiona mahali hii:
Mange Amshukia RAY C Sakata la Matumizi ya Madawa ya Kulevya..Atoboa Siri ya Ray C Kuondolewa Kwenye Progarm ya Methadone | UDAKU SPECIAL BLOG
Mange Amshukia RAY C Sakata la Matumizi ya Madawa ya Kulevya..Atoboa Siri ya Ray C Kuondolewa Kwenye Progarm ya Methadone
Katika Jitihada za kumsaidia Ray C , Mange Kimambi Amefunguka Haya Hapa Chini:
"Confirmed news, Ray C ametolewa kwenye program ya kunywa dawa ya Methadone Mwananyamala Hospital. Alikuwa kila akipimwa mkojo anakutwa bado anatumia. Pale wanatoa dawa kwa masharti.Ray C anaweza kukaa wiki hajaenda kunywa dawa, ile dawa hakuna mgonjwa anaweza kukaa siku hata 1 hajanywa, Arosto yake ni hatareeeeee unaambiwa bora Arosto ya heroine kuliko Arosto ya methodone, so ukiona mgonjwa kapitisha hata siku moja hajafika kunywa dawa ujue tu anatumia Tena hata bila kumpima mkojo. Sasa Ray C alikuwa anakata wiki hajafika kwenye dawa . Ndo wakaona wamkatie mbali. Ambao bado mnamtetea Ray as if nyie ndo mnampenda sana nenda pale wanapopokea dawa kila siku Kama utamuona Ray C. Huyo boyfriend wake wa Sasa anaitwa Frank alikuwa rafiki wa Lord Eyes,ni muuzaji na mtumiaji, Kwahiyo hapo ni parefuuuu....
Anyways point sio kumwanika Au kumwandama huwa nawapinga mno global Kwa kuandika habari za uongo Kila siku Ila Kwa hili la kumwandama Ray C acha wamwandame wanamsaidia . Maana Ray C anafanya juu chini kuaminisha watu uongo ili aendelee kujimaliza.
hata Mimi sijui anasaidiwaje , Kama rehab keshapelekwa, Kama methadone keshakunywa sijui kilichobaki. Tusichukulie hii issue kijuu juu huyu msichana akiachwa Sasa hivi atawajoin kina Whitney Houston kiutani utani Hivi Hivi.... Embu tushauriane jinsi ya kumsaidia Maana Mimi sina idea aiseeee.... Alafu akifa tutajisikia vibaya mnoooo kuwa tulikaa pembeni tunaangalia. Sitaki kujua mama yake ana hali gani . Watoto wanajua kutesa wazazi jamani, I can't imagine mtoto wangu mmoja aje kuwa hivi jamani naweza kufa kwa kuumwa roho !
Challenge kubwa ya kuwasaidia addicts inabidi wawe tayari kubadilika. Inabidi wao wenyewe ndo waamue na sio mtu umforce. Yani Ray C inabidi aamue she wants to live"
Atakufa mkuuu...wakikosa yale masembe wanatetemeka km wanataka kufa hvKupambana na wafanya biashara wakubwa aise..
Halafu najiuliza hivi akichukuliwa akawekwa selo miaka mitatu akawa anakula menyu safi huku hakuna cha dawa wala nini hatapona??
teh teh tehMkuu akiwekwa selo na menyu safi atayapata tena hyo ni kumpotezea afe tu maana hakuna namna yeye kama nani abembelezwe hivyo?