TANZIA Msanii wa Bongo Flava, Haitham Kim afariki dunia

TANZIA Msanii wa Bongo Flava, Haitham Kim afariki dunia

Sijui nazeeka au vipi, huyu Dada nimemjuwa akiwa anaumwa anaombewa michango, sikuwahi kumsikia.

Kweli kuna marehemu maarufu na kuna wanaoishi na umaarufu mfano DJ Choka sijuwagi umaarufu wake ulitokana na nini, sionagi la maana alilokuwa anafanya.
Wajinga ni wengi sana ushasema mtu anaitwa DJ choka harafu hujui umaarufu umetokana na nini au ndo hujui DJ ni kitu gani?
 
Si nimesoma hapa kuhusu wito wa kumchangia huyo Msanii kutoka kwa baadhi ya Wasanii wenzake?

Kama sababu ya kifo chake ni Uraibu wa kuvuta Shisha kama walivyochangia baadhi ya watu hapa Jamvini

Kuna Haja, Vijana wenye huo mtindo wa maisha wakabadirika.

Kumekuwa na wimbi la Vijana wengi wenye umri kati ya miaka 18 - 35 kuvuta sana Shisha.

Kwa kweli kama hazitachukuliwa jitihada thabiti, miaka kadhaa mbele kutakuwa na vifo vingi vitakavyokuwa na Mahusiano na Shisha, Pombe kali n.k
Kuna mambo mengine binadamu tuna ya fanya mpaka unajiuliza kwann tuna ya fanya?
Haya maisha ni bora kuonekana mshamba, tujaribu kuishi natural hivi vitu ambavyo sio vya lazima hatuwezi kuvimaliza.
 
Matibabu ni zaidi ya Starehe mkuu, usiseme hivyo kabisa. Kumbuka kwenye Starehe unatumia wakati huo huo unaingiza. Unapopata maradhi huingizi kitu bali unatoa tu.
Hata wewe ukiumwa kufikia mwezi 1 tu maisha yako yanabadilika.

Tumemuona hapa Prof Jay, kama sio huruma ya Mama Samia ilikuwa anarudisha jezi mapema sana, alikosa pesa za matibabu ya uhakika na watu walichanga lkn mpka pale Rais alipotoa tangazo la kumgharamikia.

Ugonjwa sio starehe ndugu yangu. Usitukane watu wala kukashifu kisa amefariki na hakuwa na hela za matibabu, hadi anapatwa na umauti unajua alitumia kiasi gani kwa matibabu achilia mbali huduma zingine muhimu?

Tuache Dharau, sisi ni Binadamu tu. Pumzi yako isikufanye kuwaona waliotangulia mbele za haki kama wazembe.
[emoji123][emoji123]
 
Sijui nazeeka au vipi, huyu Dada nimemjuwa akiwa anaumwa anaombewa michango, sikuwahi kumsikia.

Kweli kuna marehemu maarufu na kuna wanaoishi na umaarufu mfano DJ Choka sijuwagi umaarufu wake ulitokana na nini, sionagi la maana alilokuwa anafanya.
Hahahahaha,kwa huyu hata mie ndio nimemsikia kafa , kwa Dj Choka huyu yeye alikuaga na blogu maarufu ya Djcho.blogspot na pia alikua dj wa baadhi ya wasanii na dj wa kualikwa ktk shows
 
Matibabu ni zaidi ya Starehe mkuu, usiseme hivyo kabisa. Kumbuka kwenye Starehe unatumia wakati huo huo unaingiza. Unapopata maradhi huingizi kitu bali unatoa tu.
Hata wewe ukiumwa kufikia mwezi 1 tu maisha yako yanabadilika.

Tumemuona hapa Prof Jay, kama sio huruma ya Mama Samia ilikuwa anarudisha jezi mapema sana, alikosa pesa za matibabu ya uhakika na watu walichanga lkn mpka pale Rais alipotoa tangazo la kumgharamikia.

Ugonjwa sio starehe ndugu yangu. Usitukane watu wala kukashifu kisa amefariki na hakuwa na hela za matibabu, hadi anapatwa na umauti unajua alitumia kiasi gani kwa matibabu achilia mbali huduma zingine muhimu?

Tuache Dharau, sisi ni Binadamu tu. Pumzi yako isikufanye kuwaona waliotangulia mbele za haki kama wazembe.
Bosi Ruge tu kipindi anaumwa hali ilikuwa tete mpaka familia ikaomba mchango.
 
Back
Top Bottom