Msemaji Mkuu wa Serikali: Kumekuwa na upotoshaji kuhusu tozo, Wizara ya Fedha itatoa ufafanuzi tozo zilizopunguzwa

Msemaji Mkuu wa Serikali: Kumekuwa na upotoshaji kuhusu tozo, Wizara ya Fedha itatoa ufafanuzi tozo zilizopunguzwa

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
Kupitia ukurasa Rasmi wa mtandao wa Twitter, Msemaji Mkuu wa Serikali umetoa taarifa ifuatayo kuhusu upotoshaji unaoendelea kuhusiana na Tozo mbali mbali


TAARIFA

Kuna upotoshaji mkubwa kuhusu tozo za miamala ya kielektroniki iliyoanza katika mwaka huu wa fedha (2022/23). Serikali imepunguza kwa kiasi kikubwa tozo hizo. Wizara ya Fedha itatoa ufafanuzi kuhusu tozo hizi na namna zilivyoleta nafuu kwa wananchi. NAOMBA TUTULIE."


20220821_165440.jpg
 
Msemaji mkuu wa serikali ametoa tamko kupitia kwenye ukurasa wa Twitter akisema, namnukuu; "Kuna upotoshaji mkubwa kuhusu tozo za miamala ya kielektroniki iliyoanza katika mwaka huu wa fedha (2022/23). Serikali imepunguza kwa kiasi kikubwa tozo hizo. Wizara ya Fedha itatoa ufafanuzi kuhusu tozo hizi na namna zilivyoleta nafuu kwa wananchi. NAOMBA TUTULIE."
IMG_20220821_170655.jpg



-------------------

Msemaji Mkuu wa Serikali: Kuna upotoshaji mkubwa kuhusu Tozo

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema kuwa kumekuwepo na upotoshaji mkubwa kuhusu tozo za miamala ya kielektroniki(tozo katika miamala ya kibenki) iliyoanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2022/2023, ambapo ameeleza kuwa Serikali imepunguza kiasi kikubwa kwenye tozo hizo.

Ameeleza hayo leo Agosti 22, 2022 kupitia kurasa rasmi za Msemaji Mkuu wa Serikali kwenye mitandao ya kijamii, ambapo amesema kutokana na uwepo wa upotoshaji Wizara ya Fedha itatoa ufafanuzi kuhusu tozo hizo na namna zilivyoleta nafuu kwa wananchi.

"Kuna upotoshaji mkubwa kuhusu tozo za miamala ya kielektroniki iliyoanza katika mwaka huu wa fedha (2022/23). Serikali imepunguza kwa kiasi kikubwa tozo hizo. Wizara ya fedha itatoa ufafanuzi kuhusu tozo na namna zilivyoleta nafuu kwa wananchi. Naomba tutulie."- amesema Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa

Kumekuwepo na mijadala kwenye mtandao ya kijamii pamoja na kwenye vyombo vingine vya habari ikiwemo magazeti kuhusu tozo mpya kwenye miamala ya huduma za kibenki, huku baadhi ya wadau wakikosoa suala hilo na kudai kuwa linaongeza ugumu wa maisha kwa wananchi.

Itakumbukwa Serikali kupitia Waziri wa fedha, Dkt.Mwigullu Nchemba ilitangaza kupitia Gazeti la Serikali Na 478V kuanza kwa utekelezaji wa tozo ya miamala ya fedha kupitia benki.
 
FFS. Wenye hela zetu tunaona zinaibiwa halafu unatuambia kuna upotoshaji? Jinga kabisa.
 
Hii serikali imefeli,kwenye uongozi wa juu watu ni wale wale hakuna ubunifu,hakuna mawazo mbadala,akili zao zimechoka lakini madaraka wanayataka...nchi ngumu sana hii
 
Ni heri wakakaa kimya tu, hakuna ufafanuzi watakao toa utakao toa utakao kidhi haja , wao wamesha amua kutukomesha nasi tumekwisha kubali watakavyo wao, hatuna namna ila kusubiria wakati tu maana hakuna marefu yasio kua na ncha ni muda tu ndio unao subiriwa.
 
Kupitia ukurasa Rasmi wa mtandao wa Twitter, Msemaji Mkuu wa Serikali umetoa taarifa ifuatayo kuhusu upotoshaji unaoendelea kuhusiana na Tozo mbali mbali


"TAARIFA

Kuna upotoshaji mkubwa kuhusu tozo za miamala ya kielektroniki iliyoanza katika mwaka huu wa fedha (2022/23). Serikali imepunguza kwa kiasi kikubwa tozo hizo. Wizara ya Fedha itatoa ufafanuzi kuhusu tozo hizi na namna zilivyoleta nafuu kwa wananchi. NAOMBA TUTULIE."


View attachment 2330434
katika mambo ambayo magufuli alitukosea sana ni kumwinua huyu msigwa.
 
Jumba bovu hili lazima atapewa Kassim kama kawaida hahahaha! Akipewa Waziri mwenye dhamana domo lake lazima liteleze tu. Mimi naomba apewe Kinana au Shaka ndio wazungumzie tozo hizi!
 
Serikali ya walamba asali imeshindwa kupambana na matajiri huko imekuja kumkamua mlalahoi..hopeless kabisa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwa nini Serikali haikutoa ufafanuzi wa kina ili wananchi waelewe hapo mwanzo, gharama za tozo na mchango wake kwa maendeleo ya jamii na nchi kiujumla?

Wanaanzisha kitu kimya kimya bila ufafanuzi wa kutosha, na kisha baada ya malalamiko ya wananchi wanakuja kucheza mchezo wa lawama (playing the blame game), eti kuna upotoshaji?

Serikalini kuna watumishi wamejaa na wanapokea mishahara ya bure tu; Walipaswa kwa nafasi zao kuwasaidia watanzania, badala yake ofisi zao zimehamia mitandaoni kupost na kusifia ujinga.

Naunga mkono hoja za wananchi hapo juu.
 
Hawana hoja,Kwa mara ya kwanza naishuhudia serikali ikijaribu kuzima hoja ya wazi Kwa majibu mepesi kama vile wafanyavyo wasemaji wa Yanga na Simba Kwa mashabiki wao. Udhaifu ulioje huu
 
Back
Top Bottom