Msiba wa George Kahama wamkumbusha Mhariri wa Raia Mwema, Abdulwahid Sykes

Msiba wa George Kahama wamkumbusha Mhariri wa Raia Mwema, Abdulwahid Sykes

Alifutwa kwa kuwa hakuwa na adabu hivyo upuuzi wake wa kuleta udini ndio sababu kuu.... hata wewe utafutika kwasababu ya udini udini wako kwanza unachosha tu
Mlaleo,
Hapana haja ya kutukana.
Tunaweza tukafanya mnakasha wa ustaarabu watu wakatusoma na faida na tija vikapatikana.
Najua ni kwa kiasi gani wengi mfano wa wewe wanavyochomwa na historia hii ya TANU na uhuru wa Tanganyika kama nilivyoiandika.
Lakini huu ndiyo ukweli.
Ikiwa nachosha hujalazimishwa na mtu kunisoma ungeweza kunipita wima tu ukasoma hayo yasiyokuchosha.
Hii ni historia wala hakuna dini popote unajitisha pasi na sababu.
Ama kuwa nitafutika si rahisi.
Madhali nimeandika In Shaa Allah watakaokuja baada yetu watanisoma.
Wewe ndugu yangu ndiyo ushafutika hata kabla hujaandoka duniani.
Angalia mimi nikiingia kwenye uzi mnavyojazana kunisoma.
Nani leo ajae kukusoma wewe?
 
Mohamed Said historia ya marehemu George Kahama unaweza kutupatia?
Al Watan,
Historia ya George Kahama naifahamu vyema ila nachelea kuiweka hapa kwani ukweli inagusa kipindi kilicholeta mtafaruku mkubwa katika TANU baada ya Uchaguzi wa Kura Tatu 1958.

Nakushauri usome historia hii katika kitabu cha Abdul Sykes.
 
Mlaleo,
Hapana haja ya kutukana.
Tunaweza tukafanya mnakasha wa ustaarabu watu wakatusoma na faida na tija vikapatikana.
Najua ni kwa kiasi gani wengi mfano wa wewe wanavyochomwa na historia hii ya TANU na uhuru wa Tanganyika kama nilivyoiandika.
Lakini huu ndiyo ukweli.
Ikiwa nachosha hujalazimishwa na mtu kunisoma ungeweza kunipita wima tu ukasoma hayo yasiyokuchosha.
Hii ni historia wala hakuna dini popote unajitisha pasi na sababu.
Ama kuwa nitafutika si rahisi.
Madhali nimeandika In Shaa Allah watakaokuja baada yetu watanisoma.
Wewe ndugu yangu ndiyo ushafutika hata kabla hujaandoka duniani.
Angalia mimi nikiingia kwenye uzi mnavyojazana kunisoma.
Nani leo ajae kukusoma wewe?
Wewe wakati hao wazee wanakaa ulikuwepo? Historia yako uwe unasema inahusu Dini na Sio Tanganyika...
 
Mlaleo,
Mimi nimezaliwa 1952 hiki ndicho kipindi siasa za kuikomboa Tanganyika zilikuwa zinaelekea kileleni.

Baadhi ya wazalendo walikuwa na uhusiano na wazee wangu na wakija nyumbani kwetu na walinijua nikiwa mtoto mdogo na wakawa nami nikiwa kijana wakati natafiti na kuandika historia hii.

Ama hilo la kusema dini kitabu kinaitwa, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika."
Hiki ndicho nilichotafiti na kuandika na Library of Congress Washington DC imeweka kitabu hiki katika "category," ya Political History.

Lakini mimi sikulazimishi wewe uamini nilichoandika una uhuru wa kuamini historia rasmi uliyofundishwa shule na vyuoni kuwa aliyeasisi TANU ni Julius Nyerere na wala pale New Street hakuwako Schneider Abdillah Plantan wala Sheikh Hassan bin Ameir nk. nk. wala hapakuwapo Hamza Mwapachu wala Abdul Sykes wala viongozi na wanachama wa mwanzo wa TANU hawakutoka Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika nk. nk..

Pole sana haikuwa nia yangu kuumiza hisia za watu kwa kitabu hiki.
 
Wazee wako wa Gerezani walifanya kosa kubwa sana la kumuachia Kambarage chama na hayo unayoyalalamikia hapa ndiyo matokeo yake.

Hawakufanya kosa, walikuwa hawana uwezo zaidi ya Nyerere, na la pili pamoja na mapungufu yake Nyerere alijitahidi kuunganisha nchi bila kujali kabila, dini wala mila za watu.
 
Nimemsikiliza vizuri sana Mzee Mohamed Said hajasema mahali popote kuwa ni waislam tu waliopigania uhuru ila amesema majority walikua ni waislamu na huo ukweli kabisa ila kwaa watu kwa makusudi wamewafuta kwenye historia kama huyu mzee Ally Sykes..mimi nilimpinga kidogo Mzee Mohamed Said hapo mwanzo lakini baada ya kusikiliza hii video yake nimegundua anayosema ukweli mtupu ila kuna watu wamepindisha historia sijui kwa manufaa ya nani. Na ni ukweli usiopingika ni waislam ndio walikua mstari wa mbele kuipigania uhuru wa Tanganyika na wala huu sio udini ila FACTS.
Mauza...
Hapo chini ni mada nilitoa French Institute for Research in Africa,
Nairobi mwaka wa 2013:

TANZANIA: A NATION WITHOUT HEROES (ZMO) BERLIN
 
Hawakufanya kosa, walikuwa hawana uwezo zaidi ya Nyerere, na la pili pamoja na mapungufu yake Nyerere alijitahidi kuunganisha nchi bila kujali kabila, dini wala mila za watu.
Kituko,
Hili la dini na Nyerere ndipo lilipo tatizo.
Unaweza kumsoma Bergen (1981), Sivalon (1992) na Njozi (2002).

Ukipenda msome Said (1998).
Katika watafiti hawa utajifunza mengi kuhusu tatizo la dini Tanzania.

Kuhusu uwezo si kweli kuwa Nyerere alikuwa na uwezo kama watuMwaimu
wanavyotaka kuaminishwa.

Hakika uongozi wa Mwalimu katika TANU ulifanya makubwa lakini ili upate
picha kamili na nzima inabidi usome mchango wa wale walioongoza harakati
hizi toka 1929 African Association ilipoundwa.
 
Kituko,
Hili la dini na Nyerere ndipo lilipo tatizo.
Unaweza kumsoma Bergen (1981), Sivalon (1992) na Njozi (2002).

Ukipenda msome Said (1998).
Katika watafiti hawa utajifunza mengi kuhusu tatizo la dini Tanzania.

Hizo ni Hisia zako tu
 
Hizo ni Hisia zako tu
Kituko,
Hakika ni hisia zangu ikiwa utapenda kuziona hivyo kwani ightilafu
ni silka yetu binadamu.

Ila tofauti yangu na wewe ni kuwa mimi mwenzako nimetafiti na
kuandikia historia hii kwenye vitabu na kwenye paper kadhaa.

Ukitaka naweza nikakuorodheshea hapa.
 
Kituko,
Hakika ni hisia zangu ikiwa utapenda kuziona hivyo kwani ightilafu
ni silka yetu binadamu.

Ila tofauti yangu na yako ni kuwa mimi mwenzako nimetafiti na
kuandikia historia hii kwenye vitabu na kwenye paper kadhaa.

Ukitaka naweza nikakuorodheshea hapa.

Umefanya utafiti uliokuwa biased, yaani wewe ulishakuwa na hoja zako ukazitafutia sababu unazosema utafiti, we ni mbobezi sana kwa story za vijiweni na huwa napenda kukusoma na kufatilia hizo kwani hata mie zinanikumbusha mbali. Unapofika kwenye Swala la Dini ambalo halikukauki kinywani mwako ndipo ninapokutoa thamani
 
Umefanya utafiti uliokuwa biased, yaani wewe ulishakuwa na hoja zako ukazitafutia sababu unazosema utafiti, we ni mbobezi sana kwa story za vijiweni na huwa napenda kukusoma na kufatilia hizo kwani hata mie zinanikumbusha mbali. Unapofika kwenye Swala la Dini ambalo halikukauki kinywani mwako ndipo ninapokutoa thamani
Tuletee wewe historia yako yenye utafiti usiokuwa "biased" tutakusoma. Mbona tumemsoma Sivalon na Bergen, itakuwa wewe Kituko?

Hapo sasa.
 
Mzee Mohamed Said
Mimi huwa nasoma soma makala zako hapa na hata kama sehem nyingine huwa nakuwa natofautiana na mawazo yako, ki ujumla huwa nakukubali sana kwenyw tafiti zako.
Lakini leo naona umeenda kombo, at least bas unge tuletea historia ya Sir George, unge unganisha huko na watu unao wataka, then unayo taka wewe, lakin imekuwa ume mtumia tu Sir George kama daraja la ku mzungumzia Sykes (ambaye huwa tayar una mzungumzia mara nyingi). Ni kama na wewe una changia Sir George kusahaulika pia. I hope uta toa balance flan hivi nzuri.
 
Umefanya utafiti uliokuwa biased, yaani wewe ulishakuwa na hoja zako ukazitafutia sababu unazosema utafiti, we ni mbobezi sana kwa story za vijiweni na huwa napenda kukusoma na kufatilia hizo kwani hata mie zinanikumbusha mbali. Unapofika kwenye Swala la Dini ambalo halikukauki kinywani mwako ndipo ninapokutoa thamani
Kituko,
Mimi niko katika Cambridge Journal of African History.

Niko katika Dictionary of African Biography (DAB) na utanikuta
kwingi Oxford University Press.

Makala zangu zimechapwa na magazeti makubwa kama New
African na Africa Events na nikiandika na Africa Analysis na mara
moja nimechapwa na The Economist.

Miaka mingi sana imepita wakati nafanya haya.
Unataka kunambia hawa wanachapa stori za barzani?

Na hawa hawa wote wananitambua kama mtafiti na
mwandishi wa historia ya uhuru wa Tanganyika na siasa
za Tanzania.
 
Mzee Mohamed Said
Mimi huwa nasoma soma makala zako hapa na hata kama sehem nyingine huwa nakuwa natofautiana na mawazo yako, ki ujumla huwa nakukubali sana kwenyw tafiti zako.
Lakini leo naona umeenda kombo, at least bas unge tuletea historia ya Sir George, unge unganisha huko na watu unao wataka, then unayo taka wewe, lakin imekuwa ume mtumia tu Sir George kama daraja la ku mzungumzia Sykes (ambaye huwa tayar una mzungumzia mara nyingi). Ni kama na wewe una changia Sir George kusahaulika pia. I hope uta toa balance flan hivi nzuri.
Iceman,
George Kahama
mimi nimemweleza vizuri vipi aliingia TANU na katika
Baraza la Kutunga Sheria mwaka 1958 pamoja na Chifu Abdallah Said
Fundikira, Enesmo Eliufoo, Lawi Sijaona, Paul Bomani, John Keto,
John
Mwakangale na Lawi Sijaona.

Haya yapo katika kitabu cha Abdul Sykes.

Sijaweza kuwa na ujasiri wa kuandika taazia ya George Kahama kwa
namna hao hapo juu kuja TANU baadhi yao 1958 wakiwa wamechelewa
lakini Mwalimu Nyerere akawateua kuingia katika Baraza la Kutunga
Sheria 1958 kulivyozusha ugomvi ndani ya TANU kati ya Sheikh Takadir
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU na Julius Nyerere.

Hii ni historia hata Nyerere mwenyewe akiiogopa kuitaja.

Ndiyo maana hutosoma popote kisa cha Nyerere na Sheikh Suleiman
Takadir
.

Imetokea kuwa mimi ndiyo matafiti wa kwanza kumtaja Sheikh Suleiman
Takadir
katika historia ya TANU.

Mambo kama haya ndiyo yalinifanya nijizuie kuandika.
Hakuna apendae kusoma taazia iliyojaa mapambano.
 
Mzee wangu Mohamed Said basi jitahidi kuwa una balance mabandiko yako, Usindeshwe na UDINI. Nimeshangazwa kuwa Bukoba waweke picha za Ali Migeyo, Suedi Kagasheiki, Abdallah Rutabanzibwa nk. nk. Wakazi wa Bukoba hatuwatambui hao kabisa kihistoria wakati wa kupigania Uhuru. Labda walipigania Uislam.

Napenda sana kukusoma, lakini punguza udini.
Udini ni kuandika ukweli ulivyo!
Ulitaka aandikwe nani,au unaona nani ambae si muislamu ameachwa?mtaje.
 
Iceman,
George Kahama
mimi nimemweleza vizuri vipi aliingia TANU na katika
Baraza la Kutunga Sheria mwaka 1958 pamoja na Chifu Abdallah Said
Fundikira, Enesmo Eliufoo, Lawi Sijaona, Paul Bomani, John Keto,
John
Mwakangale na Lawi Sijaona.

Haya yapo katika kitabu cha Abdul Sykes.

Sijaweza kuwa na ujasiri wa kuandika taazia ya George Kahama kwa
namna hao hapo juu kuja TANU baadhi yao 1958 wakiwa wamechelewa
lakini Mwalimu Nyerere akawateua kuingia katika Baraza la Kutunga
Sheria 1958 kulivyozusha ugomvi ndani ya TANU kati ya Sheikh Takadir
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU na Julius Nyerere.

Hii ni historia hata Nyerere mwenyewe akiiogopa kuitaja.

Ndiyo maana hutosoma popote kisa cha Nyerere na Sheikh Suleiman
Takadir
.

Imetokea kuwa mimi ndiyo matafiti wa kwanza kumtaja Sheikh Suleiman
Takadir
katika historia ya TANU.

Mambo kama haya ndiyo yalinifanya nijizuie kuandika.
Hakuna apendae kusoma taazia iliyojaa mapambano.
Sawa
Nimekuelewa mzee
Basi na omba utu letee hilo timbwili la 1958, au kama ulosha andika hapa naomba
Unijuze uzi uli uitaje ili ni some pia
 
Mzee Mohamed Said
Mimi huwa nasoma soma makala zako hapa na hata kama sehem nyingine huwa nakuwa natofautiana na mawazo yako, ki ujumla huwa nakukubali sana kwenyw tafiti zako.
Lakini leo naona umeenda kombo, at least bas unge tuletea historia ya Sir George, unge unganisha huko na watu unao wataka, then unayo taka wewe, lakin imekuwa ume mtumia tu Sir George kama daraja la ku mzungumzia Sykes (ambaye huwa tayar una mzungumzia mara nyingi). Ni kama na wewe una changia Sir George kusahaulika pia. I hope uta toa balance flan hivi nzuri.

Hilo hawezi fanya kaka, huyo sio wa Deen yake, we mgeni na huyo mzee?, anaweza kukuandikia wasifu wa say Bonke Munaka lakini ukisoma ndani huwezi kuona chochote cha maana zaidi ha story za Sykes mwanzo mwisho, mpaka unajiuliza hiyo ndio wasifu wa Bonke?, aliandika wa Kyaruzi ulikuwa ni aibu tu
 
Hilo hawezi fanya kaka, huyo sio wa Deen yake, we mgeni na huyo mzee?, anaweza kukuandikia wasifu wa say Bonke Munaka lakini ukisoma ndani huwezi kuona chochote cha maana zaidi ha story za Sykes mwanzo mwisho, mpaka unajiuliza hiyo ndio wasifu wa Bonke?, aliandika wa Kyaruzi ulikuwa ni aibu tu
Nadhani mzee yeye kuna watu ambao kwao amebobea historia yao kuliko wengine.
May be pia tuna hitaji kumsoma yeye halafu tuchek na watu wa upande mwingine wana dhan ipi
 
Back
Top Bottom