Msiba wa George Kahama wamkumbusha Mhariri wa Raia Mwema, Abdulwahid Sykes

Ndio bibi Tanga na Lindi ni Pwani.

Kaingiza hiyo mikoa mingine kufunika kombe tu mwana haramu apite..

Ingekua Wahindi ndio wa Kwanza kuja Pwani ya Afrika Mashariki wewe na Mzee Said mngekua mnashubalia Wahindu wawekwe kwenye Historia.
 
Kina Germanus Pacha nadhani wako wengi! Lakini hii huenda inatokana na hulka ya Viongozi wazamani hawakupenda makubwa. Nakumbuka mama mmoja aliyefariki karibuni hata alipopewa uongozi na Mwalimu Nyerere alisema mimi sikupigania Uhuru kwa ajili ya kupata uongozi bali nilipenda nchi iwe huru baaasi. Tusitoe sana lawama Ni jukumu letu basi sisi tutafute hiyohistoria tena sio kwa kuwa biased na kuihifadhi kwa ajili ya vizavi vijavyo hata kama wao hawakutegemea haya.
 
Kituko...
Historia hiyo yako ni mpya.
Nchi ya kwanza Afrika kupata uhuru ni Ghana 1957.

Ingekuwa tuko tayari kujitawala wala Afrika isingevamiwa
na mataifa ya nje kupitia Mkutano wa Berlin.

Lakini ikiwa wewe unapenda kuamini kuwa Tanganyika
ilikuwa nchi huru 1918 hapana neno.
 
Kituko...
Kama nilivyoliahidi jamvi naweka hapa link baada ya utangulizi huu
historia ya Dk. Vedasto Kyaruzi:

Katika miaka hii ya karibuni nimesoma makala kadhaa ambazo Dk.
Kyaruzi
akifanyiwa mahojiano na waandishi wa magazeti tofauti na
katika kila makala Dk. Kyaruzi hakuacha kuweka msisitizo kuwa yeye
ndiye aliyemuachia TAA Nyerere.

Hiki ni kitu ambacho mimi kama mtafiti na mwandishi wa historia
ya uhuru wa Tanganyika kilikuwa kikinitaabisha sana. Kilichokuwa
kikinipa shida ni kuwa nilikuwa nikifahamu kuwa Dk. Kyaruzi aliingia
katika uongozi wa TAA mwaka 1950 pamoja na Abdulwahid Sykes.

Nilikuwa najua kuwa waliomsaidia kuingia katika uongozi walikuwa
watu wa mjini akina Plantan na Sykes.

Vipi watu hawa hakuwa anawakumbuka?

Wakati Nyerere anachukua uongozi wa TAA mwaka 1953 Kyaruzi
hakuwa Dar es Salaam.

Hiki ni kitu kikinishughulisha sana.

Jambo hili likishighulisha sana fikra zangu kwa kujiuliza mbona Kyaruzi
anamruka Abdulwahid Sykes katika historia yao ya uongozi wa TAA
mwaka wa 1950 na kumwingiza Nyerere ilhali Nyerere wakati ule hakuwa
anafahamika na yeyote katika duru za siasa za Tanganyika?

Nikawa nashangaa nikijiuliza kwani Dk. Kyaruzi hajui kuwa Nyerere aliingia
katika uongozi wa TAA mwaka 1953?

Nilikuwa nikijifariji kwa kusema kuwa haya ndiyo matatizo ya historia ya
uhuru wa Tanganyika.

Lakini jambo linalonisikitisha sana ni kujua kuwa katika miaka ya 1970 Dk.
Kyaruzi
alipeleka mswada wa maisha yake kwa mchapaji mmoja wa vitabu
ili mswada wake uhaririwe na kuchapwa kitabu.

Mchapaji yule ambae lilikuwa shirika la umma lilikataa kuchapa kitabu kile.

Sijui kwa nini walikataa kuchapa kitabu kile ambacho kwa hali yeyote ile
ingelikuwa hazina kubwa kwa vizazi vijavyo na hii leo wakati wa umauti
wake tungelimjua bila wasiwasi Dk. Kyaruzi na mchango wake katika
uhuru wa Tanganyika na jinsi kama alivyosema mwenyewe vipi alimwachia
TAA Nyerere.

DK. VEDASTO KYARUZI DAKTARI MWANAHARAKATI WA TAA
 

Si nimekuuliza hayo maswali hapo juu, mbona huyajibu, yajibu kama nilipokuuliza
 
Al Watan,
Historia ya George Kahama naifahamu vyema ila nachelea kuiweka hapa kwani ukweli inagusa kipindi kilicholeta mtafaruku mkubwa katika TANU baada ya Uchaguzi wa Kura Tatu 1958.

Nakushauri usome historia hii katika kitabu cha Abdul Sykes.
Ahali yangu hicho kitabu kipo bookshops? Bookshop gani? Vingine kama hicho ni vipi? Nikombali na nyumbani lakini naweza kuwatuma wadogo zangu wanitafutie hapo Dar wanitumie.

Nielimike zaidi.Nawe utapata royalties pia.
 
Si nimekuuliza hayo maswali hapo juu, mbona huyajibu, yajibu kama nilipokuuliza
Kituko,
Huwa maswali mengine huyaacha yapite na kisa ni kuwa
mie siko katika mabishano na yeyote awaye yule.

Nikinyanyua kalamu basi huwa kusomesha.

Nimeeleza kwa kirefu dhana ya Mandate Territories katika
kitabu cha Abdul Sykes.
 
Kituko,
Huwa maswali mengine huyaacha yapite na kisa ni kuwa mie siko katika mabishano na yeyote awaye yule.

Nikinyanyua kalamu basi huwa kusomesha.

Asante kwa kunielewa nilichokuwa nakimaanisha
 
Ahali yangu hicho kitabu kipo bookshops? Bookshop gani? Vingine kama hicho ni vipi? Nikombali na nyumbani lakini naweza kuwatuma wadogo zangu wanitafutie hapo Dar wanitumie.

Nielimike zaidi.Nawe utapata royalties pia.
Al Watan,
Kitabu kipo Ibn Hazm Bookshop Msikiti wa Manyema
na Mtoro pia soma Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru cha
Dr. Harith Ghassany na ''Conflict and Harmony'' in
Zanzibar cha Ali Muhsin kuhusu historia ya Zanzibar
na Mapinduzi.
 
Al Watan kitabu kipo Ibn Hazm Bookshop Msikiti wa Manyema na Mtoro pia soma Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru cha Dr. Harith Ghassany na Conflict and Harmony cha Ali Muhsin kuhusu historia ya Zanzibar na Mapinduzi.
Cha Dr. Ghassany nilikisoma kilipotoka. Kimeanza complacent halafu kikawa na a very provocative point of view that does not get discussed often.

Hivo vingine viwili nitavitafuta.
 
Cha Dr. Ghassany nilikisoma kilipotoka. Kimeanza complacent halafu kikawa na a very provocative point of view that does not get discussed often.

Hivo vingine viwili nitavitafuta.
Al Watan,
Ahsante kingine ni ''Propaganda za Udini Tanzania,''
cha Prof. Ibrahim Noor Sharif.
 
Ndio bibi Tanga na Lindi ni Pwani.

Kaingiza hiyo mikoa mingine kufunika kombe tu mwana haramu apite..

Ingekua Wahindi ndio wa Kwanza kuja Pwani ya Afrika Mashariki wewe na Mzee Said mngekua mnashubalia Wahindu wawekwe kwenye Historia.

Kagasheki wa Pwani?
 
Nashukuru kwa unayo yazungumza.

kuna mzee aliye mtoa Nyerere makerere ama alisoma naye sijakumbuka vyema kwa jina nahisi Rwegasira...achana na balozi alofariki majuzi, huyu amefariki miaka kama 5 hivi...je ni akina kagasheki tu kwa Bukoba waliopigania uhuru?

secretary general to buhaya council akina rwamugila, zahoro hawakuwa na mchango?

Ntafurahi ukinijibu, binafsi nipo hapa kujifunza
 
Nimenunua Vitabu vyako vya hiyo historia ntajitaidi nivisome
 
Dr. Akanyonyi,
Watu wengi wamechangia katika jitihada za kupigania uhuru
wa Tanganyika lakini bahati mbaya michango yao haitambuliwi.

Endapo nisingeliandika kitabu hcho cha Abdul Sykes historia
kubwa ingepotea.

Binafsi sina taarifa za Rwamugila au Zahoro katika TANU.

Kwa kuwa wewe unayo hayo majina jaribu kufanya utafiti tuwajue
watu hawa.
 
Economist hili tunalolijua,au zamani kulikuwa na lingine tofauti- na hasa hiyo nakala uliyoandika ilikuwa inahusu nini??
 
Mohamed Said , keshaweka habari za Kyaruzi nenda kasome utaona ni paragraph mbili tu ndio zenye Kyaruzi, kwingine kote ni Sykes tu, mi sio mgeni na nyie Dada Faiza

Kituko,
Hebu msome hapo chini Dr. Vedasto Kyaruzi kama nilivyomueleza katika kitabu kizima cha Abdul Sykes bila kutia niliyoweka katika ''footnotes'':
  1. Lakini pamoja na yote hayo, wazee hawakutaka kuachilia madaraka. Jambo hili lilizusha mvutano baina ya wazee na wanasiasa vijana waliosomeshwa na himaya ya Waingereza. Vijana hawa walikuwa akina Abdulwahid na Ally Sykes, Tewa Said Tewa, Stephen Mhando, Dossa Aziz, James Mkande, na wale madaktari watano - Joseph Mutahangarwa, Luciano Tsere, Michael Lugazia, Vedasto Kyaruzi na wengineo. Haya yalikuwa ni mapambano baina ya kizazi kipya na kile cha kale.
  2. Mwezi Machi mwaka 1950, katika Ukumbi wa Arnatouglo, kijana wa Kihaya, Dr Vedasto Kyaruzi alichaguliwa kuwa rais na Abdulwahid Sykes katibu wake. [1]Walipokichukua uongozi, TAA ilikuwa na shilingi themanini na saba pekee katika Barclays Bank. Huu ndiyo ulikuwa mwisho wa wazee, kuongoza TAA. Vilevile mwanzo wa uzalendo nchini Tanganyika.
  3. Baadhi ya wanasiasa wakongwe wengine washirika wa marehemu baba yake kama Schneider, Mashado Plantan na Clement Mtamila walimuunga mkono yeye na Kyaruzi katika kuipa TAA uhai mpya.
  4. Jambo la kwanza alilofanya Abdulwahid mara tu baada ya kuingia madarakani ni kuunda TAA Political Subcommittee (Kamati Ndogo ya Siasa ya TAA) [1] iliyomjumuisha yeye mwenyewe, Sheikh Hassan bin Amir kama mufti wa Tanganyika na Zanzibar; Dr Kyaruzi, Mwapachu, Said Chaurembo aliyekuwa liwali wa mahakama ya Kariakoo; John Rupia na Stephen Mhando. Kazi ya kamati hii ilikuwa ni kushughulika na masuala yote ya siasa katika Tanganyika.
  5. Makao Makuu ya TAA mjini Dar es Salaam chini ya Dr Kyaruzi na Abdulwahid ikiungwa mkono na kamati ya siasa sasa ilikuwa ikiamka kutoka kwenye usingizi mzito.
  6. Sheikh Hassan bin Amir, Abdulwahid Sykes, Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, John Rupia, Stephen Mhando na Said Chaurembo.[1] Katika taarifa yake ya mwaka ya 1950 Abdulwahid aliandika: ''Kwa ajili ya maslahi ya Waafrika na kulinda maslahi ya chama hiki na yale ya jumuiya ya Waafrika kwa ujumla, chama kimeweka wakili atakayeshauri juu ya mambo ya sheria. Wakili huyo ni Bwana E. E. Seaton wa Moshi. Mara kwa mara amekiandikia chama hiki juu ya masuala mbali mbali ya siasa, na kwa kiasi kikubwa ushauri wake umesaidia wakati chama hiki kilipokuwa kikitayarisha mapendekezo juu ya katiba.''
  7. Kufuatia mwamko huu wa chama, serikali ilishtuka na ikaanza kuingia hofu, ikaamua kumpa uhamisho Dr Kyaruzi, rais wa TAA, kutoka Dar es Salaam kwenda Hospitali ya Gereza la Kingolwira karibu na Morogoro. Serikali ya kikoloni iliamini kwa kufanya hivyo itaweza kupunguza kasi ya TAA katika uwanja wa siasa.
  8. Serikali ilidhani kwa kumtoa Dr Kyaruzi Dar es Salaam, jambo hilo lingedhoofisha uongozi wa TAA pale makao makuu. Lakini Dr Kyaruzi hakuzuiliwa na huo uhamisho. Kila mwisho wa juma alisafiri Dar es Salaam kushauriana na Abdulwahid. Serikali ilipotambua kuwa uhamisho huo haukuathiri chochote katika mchango wa Dr Kyaruzi kwenye uongozi wa TAA, alihamishwa tena kutoka Kingolwira hadi Nzega mbali kabisa na Dar es Salaam. Hapo ikawa Dr Kyaruzi amepatikana.
  9. Baada ya Dr Kyaruzi kuhamishiwa Nzega nafasi ya rais ikawa wazi. Abdulwahid akakaimu nafasi hiyo sasa akiwa katibu na kaimu rais wa TAA.
  10. Watu wengine mashuhuri walioshauriwa na kuombwa kuunga mkono chama hiki walikuwa: Dr Joseph Mutahangarwa, Chifu Abdeli Shangali wa Machame, Chifu Mkuu Thomas Marealle wa Marangu, Chifu Adam Sapi Mkwawa, Chifu Haruna Msabila Lugusha, Dr William Mwanjisi, Abdulkarim Karimjee, Dr Vedasto Kyaruzi, Liwali Juma Mwindadi, H.K. Viran, Stephen Mhando, Ally Sykes na Dossa Aziz.
  11. Hili linaweza kueleweka ikifikirika kuwa ilikuwa ni miaka mitatu tu huko nyuma wakati Abdulwahid na Dr Kyaru
  12. zi walikifufua baada ya kupoteza mwelekeo baada ya Vita Kuu ya Pili. Iliamuliwa kuwa wazee Waislam wa mjini Dar es Salaam waombwe kumuunga mkono Nyerere.
  13. Kuanzia mwaka wa 1950 wakati Abdulwahid na Dr Kyaruzi walipochukua uongozi makao makuu walianza kutumia manungíuniko ya wananchi ili kujijengea uhalali wa kuwapo kama chama chenye kushughulikia maslahi ya watu wa Tanganyika.
  14. Ajenda ya kwanza kujadiliwa chini ya TANU tarehe 9 Julai ilikuwa lile suala la uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la Kutunga Sheria. Katika mwaka 1950 itakumbukwa kuwa TAA, chini ya uongozi wa Abdulwahid na Dr Kyaruzi iliwakilisha memorandum kwa Gavana Twining kueleza mapendekezo yake juu ya mabadiliko ya katiba.
  15. Ally angefanywa kama vile Dr Kyaruzi mwaka wa 1951, alipokuwa rais wa TAA. Aliondolewa Dar es Salaam na kutupwa kwanza Kiongolwira na baadaye Nzega.
  16. Kufuatia majibishano haya kati ya TAGSA na serikali, Dr Mwanjisi kama Dr Kyaruzi kabla yake, alihamishwa kutoka hospitali ya Sewa Haji mjini Dar es Salaam hadi Kingolwira Prison Hospital karibu na Morogoro. Kawawa alipewa uhamisho kwenda Bukoba na Ally Sykes kwenda Mtwara. Ilikuwa wazi kwa uongozi wa TAA pamoja na TAGSA kuwa Uingereza ilikuwa bado haiko tayari kuwasikiliza Waafrika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…