Msichana wangu anasumbuliwa x wake

Msichana wangu anasumbuliwa x wake

Uyu demu kwa ninavyomjua uyo jamaa ni boy wake wa pili, na mapenzi yao yalikuwa private ila alipokuja kwangu akayaweka public, aliniambia ananipenda mimi ndio mana kila kitu kiko wazi. Na nilimuuliza isiwe ananitumia mimi kuwaumiza watu.
Kumbe wee jamaa una akili sasa unakwama wapi??? Au ndo bado unampendaa..
 
Ninawatoto 2 mama mbali mbali ila nilitaka nimuoe huyu just awalee watoto wangu kwa kuwa sikuwahi mpenda mwanamke kama nilivyompenda yy.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kama huyo Ex wake anajua hili bhasi hili jambo ndo analitumia kumjaza sumu manzii na vile unampenda noma sana
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kama huyo Ex wake anajua hili bhasi hili jambo ndo analitumia kumjaza sumu manzii na vile unampenda noma sana
Analijua na huwa anamwambia siwezimuoa, ila ndo nimempenda binti ,Kwakweli apa naona majogoo wawili tunatunishiana misuri
 
Ninampenzi wangu ambaye soon tunafunga ndoa,
Kuna x wake anamsumbua sana akitaka warudiane nifanyeje?
Mlelee tu jamaa. Huyo ni mmoja unayemjua, wale anaowakubali moyoni hawezi kukwambia. Happy marriage
 
Abadilishe line za simu kabisa ikiwezekana chukua namba zake we mpe namba mpya za kwako uziweke pending kwa muda, kila atakapopiga simu atakuna na wewe....


Kama haitoshi siku muite kupitia msichana wako halafu umuonye onyo kuu ukiwa na watu mbali mbali
Nilipoandika watu waoe mabikira nilitukanwa na wasioelewa, here we are!!
 
Analijua na huwa anamwambia siwezimuoa, ila ndo nimempenda binti ,Kwakweli apa naona majogoo wawili tunatunishiana misuri
Ofcoz na demu nae anabadilishwa mawazo maana jamaa anamjaza sumu sana.
 
Kabisa mkuu, hapo uyo kijana kuna nguvu anaipata na anaitumia kama weakness point kwa huyo dada yani hapo kazi ipo. Apige chini
Yes ni sahihi yaani inavyoonekana amekaa naye muda mrefu na akamzoea kwa hyo hata akimkatalia Hana wasiwasi naye anajua atatumia angles gani kumpata.
 
Mkuu usiamini hawa viumbe
Mkuu upo sahihi, hiyo ya profile picture sio suluhisho, mwanamke anaweza akawa ametoka kuku cheat akimaliza tu anakupost status alafu anaandika bonge la caption yani utasema leo kakumbuka nini kumbe ushazugwa. Umeongea kweli
 
Nina mdogo wangu alipata mchumba akijifanya ameachana na x, kumbe anawachanganya tu, skienda kwa huyu anamwambia flan ananisumbua na akienda kwa huyu kadhalika, kumbe anawapa presha wote ili mmoja ajitoe muhanga kumweka ndani mapema. Dogo alianua kukaa pembeni kwani waliishia kugombana na x kumbe mwanamke ni kicheche kama nini. Huyu aliyekuwa anamwita x ndiye aliyemwoa na wakaishi miaka mitano akawa anamfumania kila mara na sasa waneachana.
 
Mkuu trust me ukiona wewe ndio unawaza sana kuhusu usumbufu anaopata wife to be wako kutoka kwa X wake amini KWAMBA mpenzi ulie nae au wife to be wako BADO ana vichembe chembe vya mahaba niuwe kwa huyo X wake..na ukitaka kuamini Jitie kumuacha uone "lazima atarudiana na X wake"

Usiteseke akili yako Fanya hiviiiiii...Ukiwa na Wife to be wako Mwambie ampigie Huyo X wake then aweke LOUD SPEAKER aongeee nae amchane LIVE kua hamtaki..Jamaa upande wapili ataanza kulalamika (SIKILIZA YALE MALALAMIKO) unaweza kukutana na malalamiko yanasema

"kweli Julieth unaniacha unaenda kuolewa wakati tulikubaliana utamuacha huyo jamaa uwe na mimi" "Kweli unaniacha wakati ulinambia hautoisha huu mwezi wa 8 utakua ushamtafutia sababu jamaa umerudi kwangu"

Ukikutana na malalamiko toka kwa jamaa ya namna hiyo then sikiliza huyo mkeo atavyojiuma uma...Ukiona hivyo ujue Ulikua unaliwa taiming ugeukie kibla utiwe kisu shingoni...

Usimruhusu mke wako aongee na X bila wewe kuwepo (kama mkeo hajielewi) MPENZI ANAEJIELEWA HAWEZI KUSUMBULIWA NA x MAANA TAYARI UWEZO WA KUJUA CHA KUFANYA ANAO BILA HATA WEWE KUJUA..ila ukiona unasumbuka hivi Brooooooooo take care Unaenda ingiza chatu ndani ya nyumba.
 
Mkuu hata mimi kuna ex wangu anaolewa nimemsumbua hadi kakubali kuingia mkataba nisiwe namsumbua tena...

Makubaliano ya mkataba wetu.

Kwa mwaka tutakutana mara nne kufanya tendo yani kila baada ya miezi minne,
Atanisave kaka,
Tutakua tunachat mara moja moja mchana kama kaka na dada mpka siku za tendo zikaribie,
Kama akipata mimba basi sihusiki ni ya mumewe.

Take care mkuu
Kuna mmoja kanifanyia hivi hivi, kaniahdi mtoto wake mdogo aliyenaye akikua basi tutapiga mechi kibao
 
Mkuu kunywa maziwa yamoto hapo ntalipa,aisee hii kitu nime proof uwezi amini ni ukweli kabisa.
Yaani Mimi wanawake nilikuja kuwadelete kichwani kwangu kutokana na event moja hivi ambayo niliifanya Mimi mwenyewe.
Miaka Kama minne hivi nyuma nikiwa na umri wa miaka 30 nilipataga mwanamke mtu mzima mwenye umri wa miaka Kama 45 hivi nikawa nadate naye.
Ni mtu ameolewa ana mme na watoto wake 3 na mme wake ni mtu mwenye uwezo wake anamiliki vikampuni kadhaa na ameajiri wafanyakazi kwa hyo kuhusu pesa kwao sio tatizo kabisa kuanzia yeye mpaka ndugu zake.
Lakini kipindi hicho alikuja Dar kwa Dada yake ambaye ni mzee mwenye umri Kama miaka 55-60.
Basi wakati nadate naye akawa ametokea kunikubali sana hadi akawa anasahau Kama ni mke wa mtu.
Cha ajabu akanitambulisha kwa huyo dada yake na dada yake akanihitaji niende kuwasalimia Basi nikaenda kweli kumuona dada yake nyumbani kwao naingia Hadi sebuleni na kutia kishoka kwenye masofa na badae natoka nao kwenda baa kunywa nao bia then usiku mkali nawasindikiza hadi kwao Kisha mm naondoka.Badae akawa ananishawishi nimpangie chumba ili tufanye mapenzi yetu kwa uhuru zaidi ila niliogopa nikakataa nikawa nampeleka kwenye mahotel one time Kisha namsindikiza kurudi kwao.Na Hadi ikawa wananialika kwenye masherehe ya ndugu na majirani zao na kweli nahudhuria.
Sasa wakati yote haya tunafanya Mimi kichwani najiuliza maswali mengi sana kwamba hawa watu wapo serious au wananitega!
Badae akarudi Arusha kwa mme wake lakini ikawa kila akija dar lazima anitafute na dada yake anasisitiza mwambie aje.
Basi kuanzia mwaka ule siwaamini kabisa hawa viumbe.
 
Back
Top Bottom