Msigwa amhoji Tundu Lissu kupinga Wamasai kuhamishwa Ngorongoro, Lissu akosa majibu

Mkuu wengine hujatutendea haki kwani umeweka hoja za msigwa na zako tu bila kushirikisha hoja za TL ambazo wengine hatuzijui au unajaribu kuwachonganisha kisiasa?
Nenda YouTube utazikuta clips kibao ziko huko.
 
Mimi kwenye suala la ngorongoro napishana na chadema. It's high time sasa tuache cheap politics. Masai lazima waondoke
 
Hao watu wanaosema wamasai wataondolewa ili wapewe wawekezaji wana ushahidi wowote au ni hisia tu?

Kwani wataondolewa kwa kuswagwa kama mifugo bila makumaliano ya kimkataba wenye makatazo. Mkataba useme Wanaondolewa Wamasai wasije watu wengine kufanya makao yao hapo walipohamishwa Wamasai.

Utakuta wengi wanao bisha kuondoka hapo Ngorongoro wana sehemu za kufanyia matambiko aka madhabahu za miungu baali. Wanajiuliza tukiondoka miungu yetu itabaki na nani?

Serekali iwape assurance wataruhusiwa mara moja kwa mwaka kwenda kwa ajili ya ziara ya kusalimia miungu wa koo zao na kufanya matambiko.
 
Mkuu umesoma Jografia ya shule ya msingi wewe? Unalijua jangwa la Kalahari? Ingia basi kwenye ramani ya Afrika uangalie!! Karibia mchi mzima ya Botswana imefunikwa na jangwa!
Karibu mkuu mimi nipo huku Kasane, Botswana 🇧🇼, acha upumbavu why tubishane kuhusu geography ya nchi?hapa cha kuongelea ni kuhusu economy ya nchi na jinsi gani wenzetu wamemudu kuthibiti ongezeko la watu na mbinu gani wanatumia kuruhusu binadamu na wild animals waishi pamoja, hapa Kasane kuna wild animals corridor ndani ya mji!,upuuzi tulioufanya sisi ni kutokua na mipango thabiti ya to keep on check population yetu, na hili lilisababishwa na president Nyerere kuwaogopa Roman catholic church
 
Tunachopinga ni kuamishwa kwa nguvu au kwa njia yoyote ile ya kilagai. Kama kuhama wahame kwa makubaliano na mioyo mweupe
 
Naunga mkono hoja yako.

Hii suala sio kubwa kama wahusika wa pande zote wangeshirikiana kwa uwazi na kirafiki, tatizo ni watu kuzoea ujanja ujanja.
 
Kwani hoja zao ni hizo?
Hoja zao zingekuwa hizo ingekuwa rahisi

Hawa watu wanakataa fact Kuwa hakuna uharibifu, na hapo ndio hata hizi negotiations nyingine zinashindikana
 
Kwani hoja zao ni hizo?
Hoja zao zingekuwa hizo ingekuwa rahisi

Hawa watu wanakataa fact Kuwa hakuna uharibifu, na hapo ndio hata hizi negotiations nyingine zinashindikana

Shetani anakuja kama malaika wa nuru. Magomeni na Mikocheni miaka ya 1950s kulikuwa na chui, fisi na simba. TANU ambayo ni sehemu ya CCM ya sasa ilikuwa na landirova moja tu.
 
Shetani anakuja kama malaika wa nuru. Magomeni na Mikocheni miaka ya 1950s kulikuwa na chui, fisi na simba. TANU ambayo ni sehemu ya CCM ya sasa ilikuwa na landirova moja tu.
Hoja yako hapa ni nini?
 
Hoja yako hapa ni nini?

Dsm ilikuwa ni mbuga kama Ngorongoro. Shughuli za kibinadamu zimeigeuza kuwa Jiji Makao makuu ya Kibiashara Tanzania. Kilicho ibadilisha DSM kitaibadilisha Ngorongoro hao Wamasai wasipo hama.

Kwanza Wamasai wa Ngorongoro wanayo bahati. Unahamishwa unapewa nyumba ya viumba vitatu na ekari 5. Wawaulize Watanzania wengine madhila waliyo kuwa wanakutana nayo kutoka kwa askari wa Wanyapori kabla JPM hajaingia madarakani.
 
Kwani hoja zao ni hizo?
Hoja zao zingekuwa hizo ingekuwa rahisi

Hawa watu wanakataa fact Kuwa hakuna uharibifu, na hapo ndio hata hizi negotiations nyingine zinashindikana
Sio wafugaji tu wanaoalibu mazingila, hata maujenzi ya mahoteli makubwa mbugani nayo yanahalibu mazingira
 
Nenda YouTube utazikuta clips kibao ziko huko.

Simu nyingine hazina YTube ndio maana imeombwa kujuzwa, lakini kama ni lazima Wamasai kuhama basi nao wamasai wapate dhamana ya kitu kidogo kinachotokana na wanyama kwa maisha yao yote ili mwarabu asije kupenya kama alivyozoea.... serikali ibaki na ardhi kama zile nyumba zaa magomeni walivyouziwa wanyonge
 
Suala hili la kutaka kupunguza idadi ya Maasai wanaoishi hapo halikwepeki. Ni ukweli uliokuwa dhahiri ya kwamba wanaishi hapo kwa fadhila na huruma ya kisiasa tu, na wala siyo haki za kisheria. Kama ongezeko la idadi ya Maasai katika eneo hilo tengefu ambalo lipo kisheria, imedhihirika kuwa linatishia ustawi na maisha ya wanyama pori, basi haipaswi kupepesa macho wala kuuzunguka mbuyu, inawapasa waondolewe kwa utaratibu maalum.
 
T
Tundu Lissu kajichokea,huwezi kutunga sheria kusema wamasai tu ndio waishi Ngorongoro.Kwamba anaamini wamasai wako idadi Ile Ile na hawabadiliki tabia
 
Wewe ndiye unayetaka kuleta upumbavu! Utaulizaje kwamba Botswana ni jangwa wakati inajulikana kabisa kwamba Botswana iko ndani ya jangwa la Kalahari? Wacha hizo mwamba!!
 
Bado mnapush tu agenda baada ya kutembezewa hivo vibahasha vya kaki?
 
Taja Kijiji Basi Kwenu huko au msomi niwewe pekee Kijiji chote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…