Msimu huu wa joto kali ni vizuri wizara ya afya ikahimiza wananchi kunywa maji mengi/matunda

Msimu huu wa joto kali ni vizuri wizara ya afya ikahimiza wananchi kunywa maji mengi/matunda

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Mikoa mingi hapa nchini kwa sasa inapitia katika kipindi cha jua kali na lenye joto kali kupindukia, si usiku si mchana joto ni kali.

Bado wananchi mfumo wao wa maisha ni ule ule kutokana na wengi kutokujua umuhimu wa kunywa maji mara kwa mara hususani kipindi kama hiki.

Kipindi kama hiki watoto wadogo wamekuwa wakilia hovyo huku wazazi wengine bila kudadisi ya kuwa wana kiu kali ya maji watoto wao.

Kuna mtoto wa jirani mwenye umri wa miaka Miwili amefariki baada ya kuumwa siku chache na kuambiwa na madaktari ya kuwa alikuwa na nimonia ya joto.

Kipindi kama hiki watu waelimishwe umuhimu wa kunywa maji mara kwa mara, kwa ajili ya kulinda afya zao.
 
Mwishowe utataka uhimizwe kuamka na mwenda kazini
Ni wachache wenye uelewa na hili kutokana asili /tamaduni yetu, wengi wanapenda kusikia serikali imesema nini,
Sio kila Mwananchi ni muelewa kwenye mambo yanayohusu afya zao
 
Ni wachache wenye uelewa na hili kutokana asili /tamaduni yetu, wengi wanapenda kusikia serikali imesema nini,
Sio kila Mwananchi ni muelewa kwenye mambo yanayohusu afya zao

Okay, pengine ni sawa
 
Honestly maji ninayokunywa kwa kipindi hiki ni kama ngamia haipungui Lita tatu Hadi nne kwa siku.

Sweating imezidi kiukweli kwa wanaozembea yani ukipigwa malaria kidogo utapata shida dawa zitakuendesha itabidi utandikwe dripu hata name ili ukae sawa na dawa.

Caution is better than cure
 
Ni wachache wenye uelewa na hili kutokana asili /tamaduni yetu, wengi wanapenda kusikia serikali imesema nini,
Sio kila Mwananchi ni muelewa kwenye mambo yanayohusu afya zao
Wengi wanapenda udaku 🤷 thread za kuelimisha huwa ni tatizo mpaka wapate tatizo, kuhusu maji especially watoto tuwape maji sana maana wao wanacheza zaidi n wanapoteza maji kwa wingi pia.

Mtoto akiwa hana maji mwilini na akiumwa kumpa dawa ni ishu sana na atatapika atapoteza maji zaidi waweza kumpoteza hivihivi.

Let's remind each other.
 
Jana Kuna mtoto wa jirani kapoteza maisha kwa mtindo kama huu
Mtoto akiwa hana maji mwilini na akiumwa kumpa dawa ni ishu sana na atatapika atapoteza maji zaidi waweza kumpoteza hivihivi.
 
Jana Kuna mtoto wa jirani kapoteza maisha kwa mtindo kama huu
Loh!!! Ni vema kuwapa maji au kuwatengenezea juisi ili iwahamasishe kuinywa kila wakati, Kuna matikiti yanatoa juisi nyingi tu wakiwekewa kwenye fridge wanywe tu.
 
Mimi nadhani kama ni tatizo la kutokunywa maji lilishanizoea, naweza kukaa wiki bila kuonja maji na maisha yanaenda tu. Nikiwa mdogo nilikuwa nikiskia kiu naenda kulala ili tu nisinywe maji nikiamka kiu imekata naendelea na kawaida.
 
Au waunde kamati/tume ya kuhamasisha watu wanywe maji,,
 
Mimi nadhani kama ni tatizo la kutokunywa maji lilishanizoea, naweza kukaa wiki bila kuonja maji na maisha yanaenda tu. Nikiwa mdogo nilikuwa nikiskia kiu naenda kulala ili tu nisinywe maji nikiamka kiu imekata naendelea na kawaida.
Kidney stones incoming,brace yourself.
 
Kidney stones incoming,brace yourself.
Daah yani najitahidi sana kunywa maji lakini nashindwa mkuu, kuna kipindi nimewahi kukaa mwezi mzima kwa maji Lita moja tu nadhani.
 
Mimi na maji dam dam...maisha bila maji kwangu hayaendi kabisa..sijui sababu ya huu ubonge nyanya..😀
 
Daah yani najitahidi sana kunywa maji lakini nashindwa mkuu, kuna kipindi nimewahi kukaa mwezi mzima kwa maji Lita moja tu nadhani.
Kwa joto hili kiu hakikutesi??..
 
Daah yani najitahidi sana kunywa maji lakini nashindwa mkuu, kuna kipindi nimewahi kukaa mwezi mzima kwa maji Lita moja tu nadhani.
Ni Kama kusema "unashindwa kula",maji ni LAZIMA hayana mbadala. Unazichosha Figo and with time utaona majibu yake.
 
Kwa joto hili kiu hakikutesi??..
Yani nikikaa ofisini tu bila kufanya kazi yoyote ya kutumia nguvu naweza kumaliza hata wiki mbili. Sana sana nikifanya mazoezi hapo nakunywa hata lita moja na nusu kwa siku. Na huu ni zaidi ya mwaka wa 10+ katika hii hali.
 
Back
Top Bottom