Msimu ujao 2023/2024 Simba tunahitaji sajili hizi ili tuwe imara

Msimu ujao 2023/2024 Simba tunahitaji sajili hizi ili tuwe imara

Kama kweli Simba inahitaji kufanya vizuri kimataifa inatakiwa isajili wachezaji wanne/watano watakaoingia moja kwa kwa moja kwenye first eleven:-

1. Beki mmoja wa kati mwenye uwezo sawa au kumzidi Inonga ili Onyango abaki kucheza kwenye ligi ya ndani kwani ndio saizi yake kwa sasa. Iwapo Simba watakuwa na uwezo wa kuaachana naye waachane anaye kiungwana/ kistaarabu kwani ni mmojawapo wa wachezaji walioisaidida Simba kufika hapa ilipofika ndani ya misimu mitatu/minne iliyopita

2. Beki wa pembeni mweye uwezo wa kucheza kushoto na kulia kwa ufasaha ili kufanya "rotation" na Kapombe na mwenzake Mohamed Hussein kwani hawa jamaa hawapumziki kwa sababu hawana mbadala na hasa mechi muhimu zinapofuatana. Mara nyingine mpaka nawaonea huruma. Ikishidikana kupata beki mwenye uwezo wa kucheza pande zote mbili basi asajiliwe wa upande wa kushoto Gadiel aachwe kwa heshima na taadhima na apewe zawadi kwa kuonyesha nidhamu na uvumilivu kwa kipindi chote alichodumu Simba.

3. Kiungo mkabaji wa chini asili mwenye uwezo mzuri wa kupora mipira na kuilinda "back four"" na uwezo wa kuanzisha mashambulizi. Huyu awe na uwezo sawa au kuwazidi viungo wa zamani wa Simba Tadeo na Fragga.

4. Mshambuliaji wa kati mwenye nguvu na uwezo wa kukaa na mali kama alivyokua mshambuliaji wa zamani wa Simba Mugalu. Huyu atasaidia sana kwenye zile mechi ambazo timu inakwenda kujilinda na kushambulia kwa kushtukiza. Mfano mzuri mechi ya Waydad kule Morocco Simba ilikosa fowadi wa aina ya Mugalu kwani Baleke alifichwa na watu wawili na kwa kua hana nguvu sana alipotea kabisa. Ifahamike kuwa kwenye mechi kama ya Waydad inatakiwa mshambuliaji wa kati apokee mpira katikati ya mabeki wawili au watatu na aweze kuudhibiti mpira na kuwadhibiti mabeki wa timu pinzani kwa sekunde 30 mpaka dakika mmoja ili washambuliaji wenzake waliokuwa wanazuia wapande mbele haraka awape mpira waweze kushambulia kwa haraka.

5. Winga mmoja mwenye kasi anayeweza kucheza kushoto na kulia kwa usahihi na awe na uwezo wa kufunga magoli. Hapa bila kupepesa viongozi wa Simba wafanye kazi usiku na mchana wamrudishe Miquisone kwani kisingizio cha pesa hakipo tena kutokana na fedha watakazopewa na CAF kwa ajili ya Super League.

Naamini kabisa iwapo viongozi wa Simba watafanya "homework" yao vizuri na kuwapata wachezaji sahihi kwenye nafasi nilizotaja hapo juu hapo ndio itakuwa sahihi kwao kuzungumzia suala la nusu fainali, fainali au ubingwa wa Afrilka. Vinginevyo wakirudia makosa waliyoyafanya kwenye usajili uliopita ambapo wachezaji tena wa kimataifa Okwa na Akpani unawapeleka kwa mkopo ndani ya miezi sita ya usajili na huku Outtara anaozea benchi kwa kweli ni mzaha na kuhujumu uchumi wa Simba na pesa za mwekezaji.

Na kitendo cha kutamka tu kufika nusu fainali au kuchukua ubingwa wa Afrika bila ya kufanya usajili sahihi wa kufika huko ni mzaha wa hali ya juu kwa wanachama, mashabiki wa simba na watanzania kwa ujumla. Bara ala Afrika limejaa wachezaji wengi tena vijana wenye vipaji vikubwa suala kubwa tu Simba kuanza sasa usajili wasisubiri ligi ziishe wataambualia makapi.

Ni mtizamo tu.
Ulichokieleza kinaeleweka hata kwa mimi nisiejua mpira
 
1.Djuma Shaban
2.Yanick Bangala
3.Khalid Aucho
3.Bakari Nondo Mwamnyeto
4.Jesus Moloko
5.Musonda
6.TK Master
7.Kalala Mayele, Fiston
8.Bernad Morrison
9.Stephane Aziz Ki
 
Oya pale ni anguko, wanashuka kiwango kila kukicha...msimu ujao lzm tusajili zaidi ya yanga ili tuwe bora zaidi
Simba ya Mgunda ni tofauti kabisa na Simba ya Robertinho.

Anayecheza vizuri kwenye Simba ya Robertinho ni Inonga tu. Ina maana ukimwambia Robertinho tufumie kikosi, atakwambia anawataka Kibu, Ntibazonkiza na Nyoni.

Wachezaji wengi wameshuka viwango kwa aina ya mpira wa Robertinho. Ama Robertinho si kocha sahihi au anauwezo wa kawaida sana.
 
MO nae awe tayari kutoa hela.
Yanga huwa wanajilipua ndio maana wana wachezaji wazuri.
MO ana kaubahiri fulani, anapenda cheap players.
Huwezi kumwacha Adebayo unaenda kumsajiri Okwa, halafu unataka kushindana na Mamelodi.
Nimepata za ndani kabisa, hakuna mchezaji anayekuja Simba bila idhini ya MO.

Nawapongeza sana wachezaji wa Simba wanajituma sana ingawa viwango vyao ni vya chini.
Tunashindana na wachezaji wanaosajiriwa kwa mabilioni ya pesa na mishahala ya mamilioni. Yaani mchezaji wa mshahara wa milioni kumi anacheza na mchezaji analipwa zaidi ya milioni mia kwa mwezi.

Kuna wachezaji wazuri hapa kati Kariba ya Adebayo, hawaitaji pesa ndefu sana na wanakiwango kizuri sana cha kushindania kombe la Afrika.

Lingine Simba iache kuchukua vichezaji vidogo vidogo kwa ndoto za kufanana na Luiz miquessoni.

Simba inahitaji wachezaji wenye Bodi kubwa pia. Tuachane na kuchukua vichezaji kama vitoto vya shule vikina Banda, Sackho, Okwa, nk.
 
5.8B? Kua serious please
1683366135527.png
 
Yanga huwa wanajilipua ndio maana wana wachezaji wazuri.
MO ana kaubahiri fulani, anapenda cheap players.
Huwezi kumwacha Adebayo unaenda kumsajiri Okwa, halafu unataka kushindana na Mamelodi.
Nimepata za ndani kabisa, hakuna mchezaji anayekuja Simba bila idhini ya MO.

Nawapongeza sana wachezaji wa Simba wanajituma sana ingawa viwango vyao ni vya chini.
Tunashindana na wachezaji wanaosajiriwa kwa mabilioni ya pesa na mishahala ya mamilioni. Yaani mchezaji wa mshahara wa milioni kumi anacheza na mchezaji analipwa zaidi ya milioni mia kwa mwezi.

Kuna wachezaji wazuri hapa kati Kariba ya Adebayo, hawaitaji pesa ndefu sana na wanakiwango kizuri sana cha kushindania kombe la Afrika.

Lingine Simba iache kuchukua vichezaji vidogo vidogo kwa ndoto za kufanana na Luiz miquessoni.

Simba inahitaji wachezaji wenye Bodi kubwa pia. Tuachane na kuchukua vichezaji kama vitoto vya shule vikina Banda, Sackho, Okwa, nk.
Una dharau sana ww. Eti vichezaji kama vitoto vya shule.
 
Hizo sifa za wachezaji ulizozitaja, zimejaa pale Utopoloni, tukawabomoe Uto kama tulivyofanya miaka ya nyuma kwa kuwanyang'anya wachezaji wao muhimu akina Ajibu na Gadiel na kuintercept wachezaji ambao tunafununu wanataka kusajiliwa Uto kama tulivyofanya kwa Miquisone.
Itakua ike yanga ya dk Mshindo Msola.
Hii yanga ya watoto wa mjini usitegemee hilo kutokea. Huoni sakata la Feisali mlivyokwaa kisiki.

Interception mmefanyiwa nyie usajili wa Aziz Ki. Na bado mtaendelea kufanyiwa.
 
Back
Top Bottom