Msimu wa mvua unakaribia, chukua tahadhari ya Radi

Msimu wa mvua unakaribia, chukua tahadhari ya Radi

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
1644842882849.png


Hata hapa Dar es salaam, msimu wa mvua unakaribia.

Radi hapa Jijini si za kutisha , lakini tumesikia kwa mfano huko Rukwa radi imeaua karibu kila wiki.
Nyanda za Ziwa kuzunguka ziwa Victoria radi ni kitu cha kila mwaka na inaua watu wengi.

Watu wanafikiri ni uchawi lakini hewa huwa ina msuguano kutokana na mawingu yenyewe hivyo kutengeneza chembe za mawingu yanye charge hasi au chanya.
Ardhini kama kuna charge kubwa iliyo tofauti na wingu, basi umeme hutokea kuruka kama shoti ya umeme.
Hapo ndipo penye hatari maana umeme unaenda kwa kasi ya ajabu na hutafuta njia fupi zaidi.
Kama mtu amesimama ardhini na ana charge ya ardhi basi radi hukatishia kwake, na mtu huyo kuuwawa.

Tujitahidi kufanyayafuatayo kujikinga na radi:
  • Tafuta mahali salama, aidha uwe ndani ya gari au nyumba kubwa
  • Ondoka sehemu zozote za wazi kabisa na vilima(radi inaenda pale rahisi kabisa kufikia ardhi)
  • Kama huna mahali pa kukimbilia heri kukaa chini kabisa na kutosimama, huu kichwa mtu umeinamisha
  • Usikae chini ya mti mrefu na ulio peke yake(radi lazima itapiga sehemu iliyojitokeza juu)
  • Ukiwa kwenye maji nenda nchi kavu, na kuondoka ufukweni haraka iwezekanavyo
Na tukumbuke radi ukisha isikia basi umepona.
Itakapokupiga huwezi kuisikia maana mwanga na umeme wa radi unaenda kwa kasi ya ajabu.
Sauti inaenda kwa kasi ndogo zaidi.

Hizi ni tips ndogo kuokoa maisha yako, pindipo mvua za radi zinayemlea eneo lako.
 
Na kama unaishi gorofani?

Naogopa radi ule kwanga sipendi kuuona.
 
Vipi matumizi ya simu wakati radi inapiga mkuu? Unaweza kudhurika ?
 
hii kitu watu huwa wanachukulia kawaida ...lkn ni kitu hatari sana...sio salama kabisa kutumia simu wakati wa mvua kwa mikoa yenye radi....mm huwa nazima kabisa simu mvua ikianza...
Mkuu hebu fafanua uhatari uliopo Kati ya radi na simu,ili tuwe makini zaidi.
 
Back
Top Bottom