Mstaafu mwenye umri wa miaka 53 amejiua kwa kujichoma moto baada ya mahakama kuamuru kuuza mali zote na kugawana na mkewe mara baada ya kupeana talaka

Mstaafu mwenye umri wa miaka 53 amejiua kwa kujichoma moto baada ya mahakama kuamuru kuuza mali zote na kugawana na mkewe mara baada ya kupeana talaka

Kataa ndoa ni chama ambacho kina kuwa taratibu na kuchukua kasi kwa kuwa pata watu taratibu.Binafsi naweza kuungana na ninyi soon baada ya kumaliza taratibu za kutoa Talaka
 
mnachuma wote juani kwa bidii na baadaae mpongezana kwa upendo na mapenzi mazito 🐒

halafu mkishindwana ati sasa moja anabadilika kua ni mmiliki wa mwingine kwenye suala la mali 🐒

hapana,
si sawa.
mmekutana mkaamua kuishi papoja, mmepambana pamoja kwa jasho, gawaneni sawa sawa, kwa haki na usawa kwa mujibu wa sheria, kila moja akaanze maisha mengine kwa amani 🐒

kujipiga kitanzi haina maana yeyote na wala haisaidii 🐒
Hapo aliyechuma ni mwanaume ila kisheria eti wamechuma wote,Akim hakua mjinga.
 
Lusaka, ZAMBIA

Mnamo saa 09:10asbh Machi 5, 2024, Kituo cha Polisi cha Muwanjuni kilipokea ripoti ya kusikitisha ya tukio la kujiua kutoka kwa Bw. Emmanuel Mutale, mwenye umri wa miaka 42, mkazi wa kijiji cha Selengwe katika eneo la Maili Kumi. Bw. Mutale aliripoti kuwa rafiki yake, Bw. Charles Ngoma, mwenye umri wa miaka 53, na mfanyakazi mstaafu wa ZESCO, akijaribu kujitoa uhai kwa kujichoma moto kwa kutumia petroli katika makazi yake. Tukio hilo lilitokea Machi 4, 2024, mwendo wa saa moja jioni katika eneo la Maili Kumi.

Tukio zima lilikuwa hivi; Mnamo Machi 4, 2024, mwendo wa saa 19:00hrs, Bw. Ngoma alimweleza Bw. Mutale kuhusu matokeo ya kesi yake ya ndoa inayoendelea katika mahakama ya eneo la Matero. Bw.Ngoma na mkewe Faustian Chanda walikuwa wametengana kwa muda wa mwezi mmoja, na kufuatia kikao cha mahakama Machi 4, 2024, mahakama ya eneo hilo iliamua kwamba watalakiane na kuuza mali zao wanazomiliki kwa pamoja, ikiwa ni pamoja na nyumba, pamoja na mapato. kugawanywa kati yao.

Akiwa amechanganyikiwa na hukumu ya mahakama, Bw. Ngoma, katika hali ya kukata tamaa, alinunua petroli kwenye kituo cha mafuta cha mtaani kwao. Alienda kunyunyiza mafuta ya petroli ndani ya nyumba yake na kwenye gari lake, Toyota Passo yenye namba za usajili BAX 1448. Aliwasha moto huo, moto uliiteketeza kwa haraka nyumba nzima. Pamoja na jitihada za kijasiri za baadhi ya majirani kumwokoa bwana Ngoma, alipata majeraha mabaya.

Bw. Ngoma alikimbizwa haraka katika Hospitali ya Matero Level One, ambako wahudumu wa afya walimhudumia. Kwa bahati mbaya, alikufa kwa majeraha takriban dakika 30 baada ya kuwasili.

Polisi wa kituo cha Polisi cha Muwanjuni, baada ya kupokea taarifa hiyo, walitembelea mara moja eneo la tukio. Faili la uchunguzi lmefunguliwa ili kuchunguza mazingira yanayozunguka tukio hili la kusikitisha.
Ametumia nguvu nyingi bila akili angeanza kubadili umiliki wa mali kinyemela angemwandika hata mdogo wake au mama yake
 
Back
Top Bottom