Mwambie wazi ataishia kwa walimu vichwa maji wasioelewa mwanzo wala mwisho na then mwisho atalizwa yeye badaya ya kupata msukule atapatikana yeye. Watu wana professional zao sio za kufundishwa na wakizitumia hata kama ni act inakuwa real
Mkubwa, ahsante sana kwa thread nyingine nzuri sana. Inawezekana kabisa huyo X anautumia udhaifu wako ili umtimizie shida zake mbali mbali, lakini kuna wengine wana mioyo iliyojaa huruma hivyo wanaweza kabisa kuwa wanasaidia katika matatizo mbali mbali ya huyo X kwa kutotaka tu kumuona X anaisha maisha ya dhiki au anapata matatizo ya aina yoyote ile. Pale wanapokuwa na uwezo wa kusaidia basi watasaidia kwa moyo mkunjufu kabisa bila kulalama kwa yeyote yule.
Tukumbuke pia kuna X wengine pamoja na kuwa mlishindana na hivyo uhusiano kufikia tamati lakini inakuwa vigumu sana kuwatoa mawazoni. Hivyo hawa kuna baadhi kwa kugfahamu hilo wanaweza kabisa kutumia hali hii katika kupata msaada wa kila hali na wakati mwingine kwa kudhani kwamba labda kibao kikageuka na kujaribu tena kuwa katika mahusiano.
Kwa maoni yangu inapofikia X kuanza kudanganya kwa mfano "mtoto anaumwa" halafu unaenda kumuona mtoto na kukuta haumwi bali huyo X kukwambia "nilitaka kukuona tu" basi huo ni mwenendo mbaya sana ambao unaweza kabisa kuongeza uhasama uliokuwepo na hata siku nyingine inapotokea mtoto anaumwa kweli basi muhusika asiende kwa kudhani kwamba labda ndio yale yale ya "nilitaka kukuona tu" kumbe kweli mtoto yuko hoi bin taaban.
X wengine hawana hata adabu na heshima pale wanapoambiwa na waliowahi kuwa nao katika mahusiano kwamba nimeoa/nimeolewa lakini hawaelewi kabisa hutaka kuendelea kuwa na mawasiliano ya karibu mno (ya simu, emails, IM, sms n.k.) na hata kuomba misaada mbali mbali ikiwemo ushauri kuhusiana na maisha. Hali kama hii ikiachwa iendelee inaweza kabisa kuvuruga ndoa ya kuhusika iwapo mwenzie atafahamu kuhusu haya mawasiliano ya siri yanayofanyika nyuma ya mgongo wake.
Hali hii ipo sana kinachotakiwa ni kuwa na msimamo wa hali ya juu lakini kama utaruhusu hali hii ya X kutumia udhaifu wako ili tu aendelee kuwemo katika maisha yako ya kila siku au "mawazoni mwako" basi unaweza kabisa kuja kujuta siku za usoni.
NB: Ile avatar nyingine ni aje Mkuu? 🙂
...kuna ile ya mtu anafanywa msukule then siku ya siku anakugeuzia kibao! ...si unaijua zile za mume na mke wanapanga kumtia adabu Ex-Spouse (msumbufu) halafu kinachompata anashindwa hata kwenda shitaki polisi?...
Mbu hii mada nimeikutia mbali naona uvivu kusoma ..nitwangie radio call unipe mhitatasari wake ndo nichakachue
...................Ndio hapo Kate shost maana nimebakia nashangaa kuambiwa nina nguvu na sijazitumia!! ndo nijikague nizijue nizitumie niache kulialia hapa ati. Mzima lakini babygal?mwanajamii one umenichekesha sana, hata mimi sijui wanafanyiwa nini mpaka wanakosa control
...aaahhh, sasa utaharibu. Be Yourself! ...ndio maana unapendeka na kuthaminiwa hivyo ulivyo.
..Curiosity killed the Cat,...lol...
[TD="class: btext, colspan: 2"]A wife of noble character who can find? She is worth far more than rubies. Methali 31: 10 - 31
[/TD]
....Leo nimewakumbuka kina Joyce Wo wo wo...hivi 'vikarikenya' ambavyo vilikuwa vinachezeshwa 'kwasa kwasa' mitaani wakubwa na watoto wanashangilia!...
Kuna haja ya kujitazama mara mbili mbili na kuhakikisha isije ikawa nawe maishani kuna mtu anakufanya kituko mitaani jamani...Tuwe makini sana katika maamuzi yetu maishani. Tumepewa akili, tuitumie kwenye maamuzi mazuri na tuwe na misimamo thabiti. Kiukweli hakuna wa kulaumiwa kwa maamuzi yetu ila sie wenyewe.
Aibu mtu mzima kufanywa.. 'kikarikenya,'' msukule,' 'ATM,'' Buzi' na katika na hayo...
Nawakilisha.
.................. Mwe Mbu mbona unatufundisha kwa ukali jamani?......kikarikenya tena?!
....Leo nimewakumbuka kina Joyce Wo wo wo...hivi 'vikarikenya' ambavyo vilikuwa vinachezeshwa 'kwasa kwasa' mitaani wakubwa na watoto wanashangilia!...
Kuna haja ya kujitazama mara mbili mbili na kuhakikisha isije ikawa nawe maishani kuna mtu anakufanya kituko mitaani jamani...Tuwe makini sana katika maamuzi yetu maishani. Tumepewa akili, tuitumie kwenye maamuzi mazuri na tuwe na misimamo thabiti. Kiukweli hakuna wa kulaumiwa kwa maamuzi yetu ila sie wenyewe.
Aibu mtu mzima kufanywa.. 'kikarikenya,'' msukule,' 'ATM,'' Buzi' na katika na hayo...
Nawakilisha.
hapo mie ndipo panaponitia matatizoni kila wakati, na x ndio ametumia kama kigezo, anafanya kwa kusudi la kuharibu/kunipotezea amani, ni ngumu sana kila cku kumweleza mwenza wako kwamb ni salamu tu, cjui nn na nn na akakuelewa, kweli inakera sana...Mbu nae cjui ametokea wapi na hii thread leo.
Ni salamu tu my foot! Why should you entertain him? Kwanza alitakiwa hata namba yako ya simu asiwe nayo kabisa. Once you close one chapter, you better close it once and for all. Kuendekeza simu za ''salamu tu'' toka kwa ex wako ni kumuumiza hisia za mwenzi wako uliye nae kipindi hicho. Hebu fikiria na yeye akianza kupokea simu toka kwa ex wake za ''salamu tu'' mara kwa mara, wewe utajisikiaje?
Kwanza hata ile tabia ya uko na mtu kwenye mahusiano halafu awe anapenda kuongelea uhusiano wake uliopita kwa kumtaja ex wake mara kwa mara, au wakati mwingine kukulinganisha wewe na ex wake pia inaboa sana! Kifupi, tunatakiwa kuheshimu hisia za wenzi wetu.
Masaki upo umepotea sana
Umeongea la maana ila yahitaji moyo sana kuweza kuacha haya mambo maana unakumbuka mengi uliyofanya nae wakati mkiwa pamoja ndio haikuwork out ila bado huwezi kusahau
Nipo Rocky! Let the bygones be baygones! Kama kapata ajali si ampigie simu huyo aliye nae sasa hivi? Na kama mama anaumwa, si aende kumsalimia akiwa akiwa na huyo mpenzi wake wa sasa? Sasa kama na wewe uko kwenye mahusioano mengine, au ndoa kabisa, utakuwa na mama wakwe wangapi? Maana huyo mkeo naye ana mama yake, na kwa familia zetu za Kiafrika, hata mama zake wakubwa na wadogo wote watakuwa mama tu kwako!
Kuna vitu ukiviendekeza vinaweza kukufanya ukaishi maisha ya mashaka na kusononeka wakati wote ilihali huyo aliyesababisha hayo yote anaishi kwa amani, raha mustarehe!
Masaki nakubaliana na wewe kabisa unaweza haya mambo yakakufanya ukawa kichaa.
Ukisoma thread kuanzia juu kuna tatizo somehwere ambalo ukishajiingiza humo ni nadra sana kutoka na kujitambua kuwa umeshakuwa msukule. Kama unakubali kupokea simu zake unakubali kujibu sms zake na ukiitwa unaenda haraka hata kama tatizo uliloambiwa halipo na bado unaendekeza mawasiliano jua kuwa ushakuwa msukule bila kutarajia na kujiondoa pia ni kazi kubwa sana
Rocky, hilo tatizo nimelisoma hapo juu na linaweza kuwa ni tatizo kubwa sana kwa mhusika. Mimi niko upande wa mwenza wa huyo msukule wa mapenzi. Anatakiwa kuingia kati, kuwa mkali na kuhakikisha anamsaidia mwenzake kujinasua katika mtego huo! Otherwise, hata uchumi wa familia unaweza kuyumbishwa sana na huyo ex. Pesa itakuwa inapelekwa huko bila wewe kujua!
Mkuu hilo sikatai na familia inayumba sana kama mwenza wa jamaa asipokuwa makini
Ila mkuu elewa haya mambo yanafanyika kisiri sometime yaani mawasiliano kati ya Ex na mwanaume husika yanakuw aya siri sana na kama ni pesa zinatoka bila hata mwenza kuambiwa
Maana ingekuwa masuala ni kushauriana hilo lisingekuwa tatizo na ni wachache sana wanaowaambia wenza wao kuwa Ex wangu ananisumbua na hao ni wale ambao hawajawa misukule
Msukule wa kweli hatoi siri wala haongei na Ex wake mke wake akiwa anasikia mawasiliano yanamalizika huko huko na kama ni kukutana ni huko huko na msaada ni huko huko
Ndo maana tunasema yahitaji sana moyo kulimaliza hilo tatizo
Dahh,...hapo kuna ugumu sana.
Almuradi ni Win-Lose situation!
- Kuna wale ambao wakiwashirikisha wenza wao wapya, [wenza wapya] wanakuwa wakali hawataki kusikia kitu hicho. Na,
- kuna wale ambao 'wanahofia' wakiwaambia wenza wao wapya kinachoendelea, huenda wakakasirika na kuharibu zaidi!...
MBU najaribu kuwaza hapa, hivi ex ambae sikuzaaa nae kwa mfano anawezaje kunifanya msukule,