Msumbiji yaanza kusafirisha Gesi kwenda Ulaya

Msumbiji yaanza kusafirisha Gesi kwenda Ulaya

Sasa wewe uliye smart kichwani,ina kuwaje unashangaa eti gesi itoke msumbiji hadi ulaya?!??wakati sasa kuna mpango wa ujenzi wa bomba la gesi toka NIGERIA hadi SPAIN lenye urefu wa km 4000!!!halafu mbona lipo lenye urefu wenye zaidi ya km 8000?!!sasa unashangaa nini la kutoka Msumbiji?!!
Msumbiji Hadi ulaya kilomita ngapi!?..unalipitisha wapi!?..alisikia lini Bomba la gesi linajengwa msumbiji Hadi ulaya!?
 
Msumbiji Hadi ulaya kilomita ngapi!?..unalipitisha wapi!?..alisikia lini Bomba la gesi linajengwa msumbiji Hadi ulaya!?
Wewe ulivyompinga jamaa ni kana kwamba haiwezekani gesi kusafirishwa kutoka msumbiji hadi ulaya kwa kutumia bomba,na sio kuwa amesikia lini,bomba linajengwa.Lina pita wapi kwani hizo meli zinazotoka Ulaya kuja kwenye bandari ya Beira zina pita wapi?hata ziwe 11,000km,kama wakiona ki uchumi linalipa wanajenga tu.
 
Wewe ulivyompinga jamaa ni kana kwamba haiwezekani gesi kusafirishwa kutoka msumbiji hadi ulaya kwa kutumia bomba,na sio kuwa amesikia lini,bomba linajengwa.Lina pita wapi kwani hizo meli zinazotoka Ulaya kuja kwenye bandari ya Beira zina pita wapi?hata ziwe 11,000km,kama wakiona ki uchumi linalipa wanajenga tu.
Haiwezekani gesi kusafirishwa toka msumbiji kwenda ulaya kwa Bomba,wapi juu wapi chini?
 
Inawezekana unachosema na nia sio kumlaumu JPM, point ni kwamba hatuna umeme huku tuna trillions za gas ambazo zingeweza kutuwashia umeme mpaka wa ziada for the next 100 years na zaidi, kingine tunatumia trillion sita kujenga umeme wa maji ambao unategemea mvua na kuharibu mazingira (sio lazima ukubaliane na mimi kwa hili), tuna kila kitu lakini bado tunaishi kwenye umaskini na migawo kila siku kwa ajiri ya maamuzi yetu wenyewe (serikali ya CCM lazima ilaumiwe ndio waliotufikisha hapa)
Na huo ndio ukweli mchungu !! Tatizo letu siku zote kama Nchi ni Uselfishness hatuangalii maslahi ya Nchi kwanza!! Bali ya kwetu ndio ya kwanza na ndio ya muhimu zaidi !!
 
Mmmmh! Ndio maana kule hapatulii kila siku visanga kama congo![emoji848] Mtwara yetu itapona kweli!?
 
Hivi kama wananchi wananunua gas kupikia vyakula vyao, kwanini TANESCO wasinunue gas na kununua turbines za kutosha kumaliza tatizo la umeme once and for all nchi nzima, gas ipo na turbines zipo zimejaa ukiweka order mjerumani au mchina atakuja kuzifunga in 3 month, tatizo ni nini? nafikiri kuna ujinga unaendelea na lazima uwe mjinga kuuelewa
Yaani! Ni hivi! Tukitafuta suluhisho la kumaliza tatizo una dhani wale wazee wa fojifoji nangai watakula wapi!!? Sio kwamba hawajui hizo suluhu
 
Wakati sisi mwaka 2015 tulimuingiza madarakani muhutu ambaye badala ya kuendeleza mazungumzo ya uwekezaji wa gesi alipoyakuta kwa mtangulizi wake aliamua kuachana kabisa na mambo ya gesi leo Msumbiji ambao walitukuta nyuma yetu kwenye masuala ya Gesi wameanza kusafirisha Gesi kuelekea ulaya wakikamata fursa iliyofunguka

Kama Tanzania hatujaamua kuacha Siasa kwenye Utendaji tutazidi kuwa wa mwisho kwenye maendeleo hadi mwisho wa dunia
View attachment 2415622
===
Msumbiji imeanza kusafirisha gesi asilia ya kimiminika kwa mara ya kwanza, katika hatua ambayo Rais wa nchi hiyo Filipe Nyusi ameitaja kuwa ya kihistoria.

Gesi hiyo imetolewa katika kiwanda cha kando ya pwani kinachoendeshwa na kampuni ya nishati ya Italia Eni, lakini kampuni kubwa ya mafuta ya Uingereza BP ina haki ya kuinunua.

Gesi hiyo iliachwa katika meli ya mizigo ya Uingereza kuelekea Ulaya.

Usafirishaji huo unakuja wakati Ulaya ikitafuta vyanzo mbadala vya gesi, huku ikijaribu kupunguza utegemezi wake kwa Urusi.

Msumbiji inatarajia kuwa miongoni mwa wauzaji wakubwa wa gesi asilia duniani, kufuatia ugunduzi wake kaskazini mwa jimbo la Cabo Delgado mwaka 2010.

Lakini juhudi zake zimetatizwa na uasi wa makundi ya Kiislamu yenye msimamo mkali yaliyodumu kwa muda wa miaka mitano ambayo yameua zaidi ya watu 4,000 na kuwaacha mamia kwa maelfu bila makazi katika jimbo hilo.

Serikali inaamini kuwa ugunduzi wa gesi utainua uchumi, lakini Bw Nyusi alisema Msumbiji itaendelea kuzingatia "shughuli za jadi", kama vile kilimo, uvuvi, utalii, ili kupata maendeleo.
Gesi ya iliyopo Tanzania sio ya kwetu. Nionyesheni kisima cha TPDC
 
Dah...
Siamini kauli hii.
Hata zile Flyover na Viwanja vya ndege basi hata Reli vyote ni utapeli...?
Mimi sikumkubali magu hasa kwenye uonevu na double standards japo yapo mazuri aliyoyafanya.Upendeleo kwa baadhi ya mikoa ni kidonda ambacho hata baada ya yeye kutoweka kitatutesa sana kisiasa na kiutawala na hii ni invisible illness.
 
Mimi sikumkubali magu hasa kwenye uonevu na double standards japo yapo mazuri aliyoyafanya.Upendeleo kwa baadhi ya mikoa ni kidonda ambacho hata baada ya yeye kutoweka kitatutesa sana kisiasa na kiutawala na hii ni invisible illness.
Mbona hata Jakaya na Mkapa walijenga katika mikoa yao
 
Gesi ya iliyopo Tanzania sio ya kwetu. Nionyesheni kisima cha TPDC
Hata kama tumeshapigwa, hivi hata kununua gas hatuwezi kuwasha turbines zetu kumaliza tatizo la umeme? watu wawe na huruma hata kama ni upigaji sio kumaliza na kuua biashara za watu na kufanya maisha ya watu kuwa magumu, hata ile idea ya kuzamisha trillion sita kwenye hydro naona haikuwa idea nzuri maana bado tutategemea mvua tuu, mtu mweusi ni changamoto sana acha wazungu watupige tuu labda tutapata akili, cha ajabu hakuna hata mbunge mmoja anauliza kuhusu gas imeishia wapi na wananchi mpaka leo hatujui ukweli zaidi ya kusikia tumepigwa tuu
 
Kuna mtu mmoja aliniambia kwamba huwezi kupiga hatua ya maendeleo bila kubadili dominant system(os) na akatoa mifano kadhaa.
1. Mfumo wa magari yanayotumia mafuta ni wa internal combustion. Na ndio dominant sokoni. Ukitaka kuubadilisha ghafla ni hatari.
2. Key board za computer nyingi zina mfumo(?) Wa qwerty na ndiyo dominant japo azerty nayo ipo. Kuibadilisha itaathiri chumi nyingi.
3. Tanzania mfumo wetu ni Politically dominated tena na chama kimoja na uliojichimbia. Hofu kama tukibadili ghafla nini kitatokea? So watu wanakuwa na wasiwasi na hivyo. Matokeo yake tumewekeza kwenye siasa kwa ajili ya kuendelea kulinda huu mfumo. So like the IC engine tunahitaji kuubadili lakini tunahofia matokeo ya kubadilika kwa mfumo. Twende nao taratibu au tufanye overhaul?
Ili ufanye overhaul lazima ujue una nyenzo gani. Unabadili nini kuweka nini. Kwa sasa naona kubadiri mfumo huu wa chama kimoja, kuna uwezekano mkubwa ni kabadiri tu majina!
Ona sasa watanzania wenyewe ni maskini wa kipato na akili. Namna pekee tuliyonayo ni kupata dikteta mzalendo(benevolent dictator) na kuipa tafsir yenye manufaa demokrasia tuitakayo.
Mf 1 Tunaweza kubadiri wapiga kura wapass test apige tu well_informed na knowledgeable( tuwaondoe wahongwa wali na kanga).
Mf 2 kuimarisha taasisi za checks and balance kuwepo na siasa shirikishi.
Mf 3 kuondoa ukomo wa utawala kama sifa ya demokrasia ili tusimpoteze anayetufaa.
 
Tunazingatia kabila na asili kwa sababu kuna makabila yamejaa ukatili na roho mbaya. Watanzania sio wakatili na hawana roho mbaya
Hao wahutu wa Katavi na Kigoma, ambao sasa wameenea Tanzania nzima ni watanzania wamapewa uraia! Huelewi? Na bado ni wahutu huwezi ukageneralize kabila lolote kwamba ni wakatili!
Kabila la wahutu lipo Tanzania. Kama wangekuwa na hulka ya ukatili kama unavyotaka kutuaminisha, Tanzania isiinge kubali kuwapa uraia na makazi maalumu kwa ajili ya kabila lao!
Nia yako kama ni kejeli, tumia maneno mengine - siyo kabila. Heshimu kabila la wahutu kama unavyo taka kabila lako liheshimiwe.
 
Ili ufanye overhaul lazima ujue una nyenzo gani. Unabadili nini kuweka nini. Kwa sasa naona kubadiri mfumo huu wa chama kimoja, kuna uwezekano mkubwa ni kabadiri tu majina!
Ona sasa watanzania wenyewe ni maskini wa kipato na akili. Namna pekee tuliyonayo ni kupata dikteta mzalendo(benevolent dictator) na kuipa tafsir yenye manufaa demokrasia tuitakayo.
Mf 1 Tunaweza kubadiri wapiga kura wapass test apige tu well_informed na knowledgeable( tuwaondoe wahongwa wali na kanga).
Mf 2 kuimarisha taasisi za checks and balance kuwepo na siasa shirikishi.
Mf 3 kuondoa ukomo wa utawala kama sifa ya demokrasia ili tusimpoteze anayetufaa.
Asante kwa ufafanuzi. Nisaidie masuala kadhaa hapa. 1. Wapiga kura kupass test inakuwaje hasa kwa kuzingatia mfumo wetu kura hazipigwi kwa maeneo(hatuna electoral college) na hizo test pia huoni kama zina ubaguzi?
2. Checks and balances zipo kwa mujibu wa katiba. Kama hazipo vizuri tunalazimika kufanya overhaul ya mfumo(katiba?).
3. Binadamu huwa hatutabiliki. Huyo benevolent dictator akitugeuka tukiwa tumeondoa ukomo tufanyeje(mapinduzi?). Nadhani best option tuwe na katiba ambayo ni jumuishi na ambayo haitakidhi maslahi binafsi ya mtu au kikundi bali kikundi au mtu akidhi mahitaji ya katiba.
 
Acha tuendelee kulala ile wizara ilibidi iwe na mtu makini km Mhongo
 
Magufuli hii nchi aliirudisha nyuma miaka 10, sio kwenye utawala bora wa sheria tu bali pia maendeleo
Magufuli alikua na malengo mazuri mikataba mingi ya wazungu tuliyoingia humu haitufaidishi ni ujanja ujanja yeye alikua anarekebisha sana
 
Back
Top Bottom