Mtaala mpya wa elimu, walimu jiandaeni kurudi shule

Mtaala mpya wa elimu, walimu jiandaeni kurudi shule

Utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 na mitaala ya elimu toleo la 2023 utaanza kwa awamu mwakani, huku walimu watakaofundisha shule ya msingi wakipaswa kuwa na stashahada ya ualimu.

Akiwasilisha rasimu za sera na mitaala hiyo kwenye semina ya wabunge jijini hapo, Kamishna wa Elimu Tanzania, Dk. Lyabwene Mtahabwa, alisema katika mapendekezo ya rasimu hizo, walimu watakaofundisha elimu ya msingi itakuwa lazima wawe na stashahada ya ualimu baada ya kumaliza kidato cha sita.

Alisema kwa watakaofundisha elimu ya sekondari, ni lazima wawe na shahada ya ualimu, hivyo walimu waliopo kazini ambao hawatokuwa na sifa hawataondolewa kwenye ajira bali watapewa fursa ya kujiendeleza ili kufikia viwango.

Akitoa ufafanuzi kwa wabunge, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisema hakutokuwa na mtihani wa kumaliza elimu ya msingi badala yake kutakuwa na mtihani wa upimaji, ili kuendelea na elimu ya sekondari ngazi ya chini.

Chanzo: Nipashe
Elimu ya Tanzanua mbwembwe nyingi utekelezaji sifuri. Wanabadili mitaala lakini hakuna tija yoyote.
Unaanzisha mada za computer halafu shuleni hakuna umeme wala kompyuta zenyewe, huo si uhawayani.
Hakuna mahusiano yoyote kati ya diploma na elimu ya msingi, ni mbwemmbwe tu.
Elimu ya Tanzania inahitaji resource na rasilimali watu.
Mwalimu mmoja anafundisha masomo 4 na zaidi, hivi kuna tija hapo hata kama mwalimu ana digrii.
 
Sijui walitumia kigezo gani
Waliofeli shule ndo wakapewa kazi ya kuelekeza Awali na msingi
Hata secondary waliofanya vibaya form six bdio huenda kusoma diploma ya ualimu. Form six waliopata div 1,2,3 wengi huenda vyuo kusoma degree
 
Ualimu
Sekta ya Afya
Wapelekwe waliofaulu tu, waliofeli watafute vitu vingine vya kufanya
Hakuna field inayotaka vilaza kijana...
Vijana wakaze sana form four wapate vyeti vizuri ili wachague fani yoyote wanayoitaka bila kusumbuana...
Kama sijakosea bado C tatu ni sifa ya kusoma A level...sasa kweli vijana wanashindwa kujibana wapate izo C tatu tu aisee?sikuhizi material yako kila mahali hadi YouTube

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
 
Hakuna field inayotaka vilaza kijana...
Vijana wakaze sana form four wapate vyeti vizuri ili wachague fani yoyote wanayoitaka bila kusumbuana...
Kama sijakosea bado C tatu ni sifa ya kusoma A level...sasa kweli vijana wanashindwa kujibana wapate izo C tatu tu aisee?sikuhizi material yako kila mahali hadi YouTube

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
Hakuna wakati elimu ni rahisi kama zama hizi ambazo kila kitu kiko mtandaoni
Sio notice, maswali, majibu

Ila wanafunzi hawasomi
 
Hakuna wakati elimu ni rahisi kama zama hizi ambazo kila kitu kiko mtandaoni
Sio notice, maswali, majibu

Ila wanafunzi hawasomi
Kabisa,o level ndio hatua ya muhimu sana kwa elimu ya bongo ukishanyoosha pale basi unaweza kua yoyote unayetaka...kuna option ya college ama A level imradi tu cheti chako kiko bomba

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
 
Kabisa,o level ndio hatua ya muhimu sana kwa elimu ya bongo ukishanyoosha pale basi unaweza kua yoyote unayetaka...kuna option ya college ama A level imradi tu cheti chako kiko bomba

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
Kibongo bongo bado wanafunzi hawajitambui huko college wanaenda fanya umalaya tu, kuolewa wengi wao
 
Ni vyema ila serikali igharamie hayo masomo ya walimu.
Kila kitu kitaenda vizuri na si kuwapa ruhusa tu maana wengi wamepigika, hawana pesa, mikopo ya kumalizia mapagare imewasambaratisha
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hakuna field inayotaka vilaza kijana...
Vijana wakaze sana form four wapate vyeti vizuri ili wachague fani yoyote wanayoitaka bila kusumbuana...
Kama sijakosea bado C tatu ni sifa ya kusoma A level...sasa kweli vijana wanashindwa kujibana wapate izo C tatu tu aisee?sikuhizi material yako kila mahali hadi YouTube

Sent from my SM-A035F using JamiiForums mobile app
Betting, kamari, bangi, sigara,
Kujichubua, kudanga, wamuachie nani??
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jaribuni muone...

Walimu wa Diploma walio Sekondari ndio walimu tegemeo. Kuliko hizo degree fake.

Msijaribu kufanya kosa hili...
Diploma kufundisha sekondary sio sahihi hana tofauti na form six

Ndio.maana shule nyingi za sekondary za serikali zina matokeo mabaya sana

Private walikojaa walimu wenye digrii kuko vizuri.mno
 
Diploma kufundisha sekondary sio sahihi hana tofauti na form six

Ndio.maana shule nyingi za sekondary za serikali zina matokeo mabaya sana

Private walikojaa walimu wenye digrii kuko vizuri.mno
Unaongea usilolijua ww ..

Private schools never prefer graduates employee...

Nenda kesho private yeyote utakuta vijana form six...fresh kabisa wanapiga kazi..

Private shida yao content bas...
 
Back
Top Bottom