Nina miaka kama 17 au 20 hivi imepita sijalia na yawezekana labda ndiyo maana hivi sasa nina Uono hafifu. Ngoja nimchokoze Mtu anipige ili Nilie.
Mkuu, kulia kwa kipigo baada ya kumchokoza mtu ni kulia kusipofaa, hakuna manufaa hapo ila moyoni kunakuwa na majonzi na msiba tu katika hali hiyo huponi kisaikolojia bali unaongeza ugonjwa wa kisaikolojia na mbaya zaidi mtu huyo akupige hadi akujeruhi na akupe ulemavu wa maisha, halikadhalika kulia kwa huzuni au kupatwa na majanga huko sio kulia kwa manufaa, mimi "NIONAVYO" (na hapa nipo huru kukosolewa), kulia kwa furaha na kulia kwa kuonyesha shukrani kwa mtu baada ya, mfano, kupewa msaada na mtu huyo.
Mimi, kama nilivyosema, huwa nalia ninapokuwa naswali katika posture ya shujuda,ninapotaka kutoa shukrani wakati huo huwa navuta hisia kwamba nipo mbele ya Mungu ili nimpe shukrani kisha huwa najaribu kutafakari kwamba; bila ya Yeye (Mungu) jambo langu lisingefanikiwa na hakukuwa na mwingine angaliweza kunisaidia isipokuwa Yeye, ninapojenga hisia kwamba hakukuwa na Yeyote angaliweza kunisaidia katika shida niliyoiepuka nk, basi jambo hilo hutia "humility" ndani ya Moyo wangu hapo machozi hunitoka na huwa natamka maneno haya "Sifa zote njema zinakustahiki wewe Mungu", kwangu hicho huwa ni kitendo cha dakika 2-3 hivi.
Katika Mazingira ya kuomba msaada kwa kulia nayo yanafanana na mazingira ya kutoa shukrani isiookuwa katika kuomba msaada maneno ninayotamka huwa; "hakuna mwingine yeyote awezaye kunisaidia isipokuwa wewe mtukufu Mwenye nguvu".
Kumbuka Mungu anazo sifa nyingi sana na anao uwezo mkubwa sana na hapa sisemi kwamba hizo dua zangu ndizo perfect sana, laahasha, mimi bado ni mtu dhaifu na ninayo mapungufu kibao bali ninajaribu kuonyesha ni jinsi gani mtu mzima anavyo weza kulia "with a fruitful purpose"
Mwisho, Mungu ni Supreme being, yeye ndiye ametuumba sote na kila kitu hivyo tukiwa mbele yake huwa zaidi ya mtoto mdogo kwa mzazi wake, yaani ulinganisho wa Mzazi kwa mtoto haufanani na ulinganisho wa Mungu kwa mtu, kama mtoto anaweza kulia mbele ya mzazi wake akiomba pipi sasa vipi mtu mzima ashindwe kulia akitoa shukrani au akiomba msaada mbele ya the most supreme being, the creator ??. Nadhani huko ndiko kulia kwa manufaa na hapo moyo hufarijika kwa furaha na raha.