Mtaalamu wa Dawa na Tiba: Ninakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

Mtaalamu wa Dawa na Tiba: Ninakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

Dr, mtoto wangu anasumbuliwa na maumivu ya miguu, nyuma ya kisigino hadi kwenye vidole, kun wakati maumivu yanazidi hadi anachechemea kutembea, ametumia dawa za hospital (Prednisolone na calcimag) bila mafanikio. Msaada tafadhali, ni binti 13 yrs old

Naomba umpeleke kwa daktari wa watoto kufanya vipimo ili tatizo ijulikane. Vipimo vya calcium, vitamin D, Bone Density ni muhimu.
 
Mtaalamu nina mtoto Wangu ana miezI saba hivi ametoka malenge lenge sehemu za mapajani yaanI liki pasuka mmoja linaota lingine naomba msaada wako.
 
Dr. Nina kijana wangu wa miaka 14 ametokwa na malenge lenge yaani tuvipele sehemu za siri kwenye kichwa cha uume wake tatizo nn na atumie dawa gan
 
Naomba umpeleke kwa daktari wa watoto kufanya vipimo ili tatizo ijulikane. Vipimo vya calcium, vitamin D, Bone Density ni muhimu.

Nilishampeleka akapewa hizo dawa za calcium na vitamin D lakini hazina matokeo mazuri
 
Dr habari yako?nashukuru nilikueleza tatizo langu la kutipata choo kwa wakati, nashukuru ulishauri nitumie Lactlose oral kwa muda wa wk nimetumia nikapata choo kwa wakati lakini nisipotumia iyo dawa tatizo linarud pale pale?ushauri dct
 
Habari wakuu,

Nakaribisha maswali yoyote kuhusu magonjwa, dawa, tiba na afya kwa ujumla. Kama una maswali kuhusu ugonjwa wowote, vipi kuishi na magonjwa, kufanya mabadiliko kwenye maisha baada yakupata ugonjwa, matibabu, matumizi ya dawa, matumizi ya dawa pamoja na dawa nyingine au athari zake.

Karibuni sana.

View attachment 361607

Kama umejibiwa maswali na mtu mwingine na haijakufaa ni kosa lako.
Mimi nitajibu maswali zote mwenyewe kama Daktari.










Habari Dr
Nimetokewa na vipele vingi vidovidogo mikononi na miguuni tu. Vipele haviwashi wala haviumi. Nimeenda hospital wakanipima damu wakasema inawezekana ni allegy kutokana na vyakula ninavyotumia.Akanishauri nikapime kipimo cha allegy ambacho bado sijakifanya.Wakanipa dawa ya kupaka tu ambayo nilipaka lakini havijaisha. Msaada kama kuna dawa nyingine naweza kutumia kumaliza hili tatizo.
Ahsante
 
Dr. Nina kijana wangu wa miaka 14 ametokwa na malenge lenge yaani tuvipele sehemu za siri kwenye kichwa cha uume wake tatizo nn na atumie dawa gan

Tumia dawa hii: Sonaderm, pakaa kutwa mara mbili asubuhi na usiku kwa muda wa siku kumi alafu nipe mrejesho.
 
Dr habari yako?nashukuru nilikueleza tatizo langu la kutipata choo kwa wakati, nashukuru ulishauri nitumie Lactlose oral kwa muda wa wk nimetumia nikapata choo kwa wakati lakini nisipotumia iyo dawa tatizo linarud pale pale?ushauri dct

Nimefurahi kuona dawa imesaidia. Je unakula matunda na kunywa maji kwa wingi?
 
Habari Dr
Nimetokewa na vipele vingi vidovidogo mikononi na miguuni tu. Vipele haviwashi wala haviumi. Nimeenda hospital wakanipima damu wakasema inawezekana ni allegy kutokana na vyakula ninavyotumia.Akanishauri nikapime kipimo cha allegy ambacho bado sijakifanya.Wakanipa dawa ya kupaka tu ambayo nilipaka lakini havijaisha. Msaada kama kuna dawa nyingine naweza kutumia kumaliza hili tatizo.
Ahsante

Ndiyo kuna dawa nyingi ya allergy kwaajili ya vipele. Naomba uniambie dawa gani ulipewa?
 
Alaf pia ni kwa nini unaweza ukafanya tendo la ndoa na mwenye ukimwi lakini wewe usipate??

Hii inategema na kama huyo mtu anatumia dawa za HIV na Idadi ya virusi ndani ya mwili wake. Lakini ni kama unaweza kufanya tendo la ndoa na mwanamke na asipate mimba. Ni bahati tu tuseme. Lakini tunashauri kwamba mtu asifanye kitendo la ndoa kwasababu chance yakupata hizo virusi ni kubwa na ukishapata ndiyo hivyo itabidi umeze dawa kila siku maisha nzima pamoja na kuwa na tahadhari ili usikose dozi wala kupata maradhi mengine.
 
Dr nakuomba kwa maelekezo yako uliyonipa na mizunguko niliyozunguka kwa matabibu nashindwa ni dr yupi ndio bingwa wa matatizo ya uzazi kwa wanawake naomba kwa msaada wako niambie nimuone dr gani au hospital gani ambayo naamini kwangu sasa itakuwa ni fainal

Gynecologist. Unaweza kuja Hospitali ya Sanitas, Mikocheni.
 
Dkt pole sana na majukumu. Kuna katatizo kameanza sio muda mrefu. Nikiamka asubuhi na kufanya mazoezi ya jogging basi nawashwa sana kwenye mapaja baada ya mwendo wa dk kadhaa kiasi cha kushindwa kumaliza na nikisimama tu baada ya sekunde kadhaa hali inatulia. Nini yaweza kuwa shida.

Hii mwasho inatokea kwenye mapaja tu? na asubuhi wakati yakufanya jogging tu?
 
asante mtaalam maana hii ilinitokea baada ya kusex masaa miwil Bila kupata bao na sikupumzika na kuja kumaliza nakuja kuona shahawa zinadam Dam but nilianza kutumia hizo dawa sasa naona imeisha isha

Nimefurahi kuona dawa imekusaidia. Asante kwa mrejesho.
 
Back
Top Bottom