Mtaani kwenu kuna Tahadhari dhidi ya CoronaViruses?

Mtaani kwenu kuna Tahadhari dhidi ya CoronaViruses?

Mtaa unaoishi halo ilivyo ipoje? Mtaani kwetu unaweza kujua hakuna ugonjwa huu kabisa. Karibia kila kitu kinaendelea kama hamna kitu, watu wanaishi maisha yao bila wasiwasi (mikusanyiko na vijiwe) kilichobadirika ni ndoo za maji mtaani ambazo hazitumiwi.

Watu wanaishi maisha yao na kata yetu yote sijasikia mtu kafa kwa Corono au kahisiwa. Ila ukiingia mitandaoni jinsi wanavyoeleza hali ni tofauti na uhalisia. Unaweza kudhani watu wanakufa sana au wako hoi sana mitaani.
Je hali ya mtaani kwenu ipo vipi.?
Kusema ukweli kabisa kutoka moyoni, sijawahi kuona msiba mtaani kwangu tena ni Mwananyamala uswazi kabsaaaa. Hata mimi naona mauzauza tu. Wanakufa viongozi. Nadhani serikali ingechunguza. Yaweza kuwa kuna kitu hakiko sawa mahali. Sabotage inaweza kuwa iko kazini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umepima ukakutwa negative?? Bro tunatembea na virusi kwa sababu ya uimara wa kinga za miili yetu.. ushauri wangu jitahidi sana kuwakinga wazee wako na watu wako wa karibu wenye afya dhaifu .. .corona ipo.na ni hatari kweli kweli.. ikipata upenyo tu huchomoki
 
Tanzania kila kitu hewa, Corona hewa, wafanyakazi hewa, wanafunzi hewa,

Corona imebakia jina Tu Tanzania, Huku kwetu kila ninayekutana naye, anaulizia tu, hivi wamefika wangapi? Sasa endapo kila mtu atakuwa anauliza wamefika wangapi, unagundua kabisa hii Corona haipo, kama ingelikuwepo, basi hata hao wanaouliza watu kufika wangapi wangekuwa nao wanaugulia!

Corona hewa
 
Tanzania kila kitu hewa, Corona hewa, wafanyakazi hewa, wanafunzi hewa,

Corona imebakia jina Tu Tanzania, Huku kwetu kila ninayekutana naye, anaulizia tu, hivi wamefika wangapi? Sasa endapo kila mtu atakuwa anauliza wamefika wangapi, unagundua kabisa hii Corona haipo, kama ingelikuwepo, basi hata hao wanaouliza watu kufika wangapi wangekuwa nao wanaugulia!

Corona hewa
Corona haipo,mwambieni basi yule mzee aliyejificha kule kijijini arudi huku town aendelee kuchapa kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom