Course Coordinator
JF-Expert Member
- Jul 27, 2019
- 1,742
- 3,224
Habari za Jumamosi
Haya mambo haya ndani ya wiki mbili hizi hatujazoea, kupishaha na magari sana sana coastal zenye waombolezaji kiasi hiki, barabarani unaweza kupishana na coastal zilizobeba miili ya wafu zaidi ya 9 kwa siku, hali hii sikuizoea kabisa.
Unaweza kujiuliza kuna ajali gani ilitokea hivi karibuni ikaua ndugu zetu, jamaa zetu, marafiki zetu kiasi hiki hizi maiti zinasombwa wapi ,je hii ni Brazil, au Italia ya 2020 tuliokuwa tunaisikia au ni kuna Boko Haramu siku hizi Tanzania inaua ndugu kwa kuvizia.
Ila ukiona waombolezaji wanaosindikiza miili ya wapendwa wao wote wamevaa barakoa ndo unashituka aaah kumbe kuna ugonjwa wa homa ya mapafu Tanzania (Pneumonia)...basi unaendelea na safari zako, unajiuliza tu kimya kimya sijui wanaenda wapi, sujui ni akina nani, msiba usije ukafika ukaambiwa ni flani kafa ila tu hukupati taarifa mapema.
Ndugu zanguni tujilindine,tusisubiri mamlaka husika ikuambie jilinde na uchukue tahadhari,wabunge wamesema hosptali zimejaa ukienda unaumwa Neumonia kuna mawili ama usubirie mgonjwa ampone au usubirie mgonjwa afe ndo upate Oxygen, unaambiwa hata kwa kuhonga rushwa hupati Oxygeni
Mtu atakayeugua na apate mashine ya oxygen ni wale VIP class no 1.
Mfano augue RC na Waziri augue pneumonia wewe unadhani nani atapata hiyo mashine ya Oxygen haraka ?.
Tuachane upuuzi wa kusema Pneumonia inaua wazee wa miaka 60 na watu wanene ,huo ni ujinga wa kutokuelewa afya.
Tuacheni ujinga wa kusema Pneumonia inaua sehemu ya baridi tu.
Tuacheni ujinga wa kusema Pneumonia tujifukize itaisha ,tunywe malimao tangawizi Sijui vitunguu.
Lini kichomi na homa ya mapafu iliisha kihivyo,dawa zote za asili hufanya kazi taratibu sana .
Unapomchukua mwanamke ujikinge na magonjwa ya zinaa kama UKIMWI serikaki iliwahi kukutuma ununue kondom ?
Ulipopata maradhi ya zinaa serikali ilikuuliza kwa nini hukutumia kondom sana sana si daktari atakushauri ujikinge na uwakinge wengine ?
Sasa kwenye hili la pneumonia si hao hao wataalam wa afya wametushauri tuvae barakoa na kufanya social distance.
Unapokufa familia yako itakulilia itagharamikia mazishi yako wachinje ng'ombe.
Wakifa wao serikali ndo inabeba misiba yao,peps na cocacola watapeleka soda na maji ya dasani,kilimanjaro na Azam atapeleka unga wa maandazi,Mtibwa na Kagera Sugar atapeleka sukari kwa ajili ya chai.
Tuchukue tahadhari ,jana nimetoka kumzika ndugu yangu Professa wa miaka 48 hasara kwa familia kisa pneumonia inauma.
Wao wanaumwa sisi tunaumwa ,hatuna BIMA wao wanazo,hatuna lishe wao wana mafungu,hatuna STK,SU,STL,SL,RAC,sisi tunategemea kukodisha coasta.
Bwana awasaidie wale wote wanaopigania UHAI wote mahospatalini na majumbani kwa ugonjwa wa Pneumonia na magonjwa mengine.
Tujilinde tujikinge ,tuwalinde tuwakinge.
Jumamosi iliyo Njema kwa wote.
Haya mambo haya ndani ya wiki mbili hizi hatujazoea, kupishaha na magari sana sana coastal zenye waombolezaji kiasi hiki, barabarani unaweza kupishana na coastal zilizobeba miili ya wafu zaidi ya 9 kwa siku, hali hii sikuizoea kabisa.
Unaweza kujiuliza kuna ajali gani ilitokea hivi karibuni ikaua ndugu zetu, jamaa zetu, marafiki zetu kiasi hiki hizi maiti zinasombwa wapi ,je hii ni Brazil, au Italia ya 2020 tuliokuwa tunaisikia au ni kuna Boko Haramu siku hizi Tanzania inaua ndugu kwa kuvizia.
Ila ukiona waombolezaji wanaosindikiza miili ya wapendwa wao wote wamevaa barakoa ndo unashituka aaah kumbe kuna ugonjwa wa homa ya mapafu Tanzania (Pneumonia)...basi unaendelea na safari zako, unajiuliza tu kimya kimya sijui wanaenda wapi, sujui ni akina nani, msiba usije ukafika ukaambiwa ni flani kafa ila tu hukupati taarifa mapema.
Ndugu zanguni tujilindine,tusisubiri mamlaka husika ikuambie jilinde na uchukue tahadhari,wabunge wamesema hosptali zimejaa ukienda unaumwa Neumonia kuna mawili ama usubirie mgonjwa ampone au usubirie mgonjwa afe ndo upate Oxygen, unaambiwa hata kwa kuhonga rushwa hupati Oxygeni
Mtu atakayeugua na apate mashine ya oxygen ni wale VIP class no 1.
Mfano augue RC na Waziri augue pneumonia wewe unadhani nani atapata hiyo mashine ya Oxygen haraka ?.
Tuachane upuuzi wa kusema Pneumonia inaua wazee wa miaka 60 na watu wanene ,huo ni ujinga wa kutokuelewa afya.
Tuacheni ujinga wa kusema Pneumonia inaua sehemu ya baridi tu.
Tuacheni ujinga wa kusema Pneumonia tujifukize itaisha ,tunywe malimao tangawizi Sijui vitunguu.
Lini kichomi na homa ya mapafu iliisha kihivyo,dawa zote za asili hufanya kazi taratibu sana .
Unapomchukua mwanamke ujikinge na magonjwa ya zinaa kama UKIMWI serikaki iliwahi kukutuma ununue kondom ?
Ulipopata maradhi ya zinaa serikali ilikuuliza kwa nini hukutumia kondom sana sana si daktari atakushauri ujikinge na uwakinge wengine ?
Sasa kwenye hili la pneumonia si hao hao wataalam wa afya wametushauri tuvae barakoa na kufanya social distance.
Unapokufa familia yako itakulilia itagharamikia mazishi yako wachinje ng'ombe.
Wakifa wao serikali ndo inabeba misiba yao,peps na cocacola watapeleka soda na maji ya dasani,kilimanjaro na Azam atapeleka unga wa maandazi,Mtibwa na Kagera Sugar atapeleka sukari kwa ajili ya chai.
Tuchukue tahadhari ,jana nimetoka kumzika ndugu yangu Professa wa miaka 48 hasara kwa familia kisa pneumonia inauma.
Wao wanaumwa sisi tunaumwa ,hatuna BIMA wao wanazo,hatuna lishe wao wana mafungu,hatuna STK,SU,STL,SL,RAC,sisi tunategemea kukodisha coasta.
Bwana awasaidie wale wote wanaopigania UHAI wote mahospatalini na majumbani kwa ugonjwa wa Pneumonia na magonjwa mengine.
Tujilinde tujikinge ,tuwalinde tuwakinge.
Jumamosi iliyo Njema kwa wote.