Mtafutaji nisiyechoka naomba mnishike mkono nipate ajira

Nimekosa hata cha kukujibu, but asante kwa ulichoandika. Ila muombe sana Mungu uwe na mwisho mwema kwa kila ulichojaliwa.
 
Nimekosa hata cha kukujibu, but asante kwa ulichoandika. Ila muombe sana Mungu uwe na mwisho mwema kwa kila ulichojaliwa.
Chukua ushauri weka hisia pembeni. Vijana hamtaki kuambiwa ukweli unataka udanganywe danganywe matokeo yake ndio hayo unaelimu kubwa huna uhakika imagine dereva dalaldala alieamka saa kumi usiku now anatafuta mtu amsaidie yeye akalale na huenda hesabu kashaisogeza ww upo jf kulialia na elimu yako ukipewa ukweli na maneno yatakayofanya uzinduke unaanza kuleta hisia za kidada. Na elimu yako bado unazidiwa na watu waliojiajiri kwa kazi za kawaida sana. Imagine mtu kashapiga supu nzito chapati 3 na anaendelea na kazi ww ukute hata hujaipa minyooo kifungua kinywa
 
Mnatukatisha wengn kuendelea na elimu ya juu aisee, yn kwa profile yko hiyo mkuu hauna ajira mpk Leo...dah? Mungu akuone ndugu yng akufungulie milango
Usikate tamaa alimu ina umuhimu wake lakini umuhimu mkubwa ni kutambua fursa na kifungua milango ya fahamu za maisha. Mbali na hapo hakuna faida ya kusoma kama utakua mtegemea vyeti. Cha msingi soma ukiwa unajaribu kuvumbua ujuzi au maarifa yaliyopo ndani yako
 
Asante mkuu, sorry kama kuna kitu nimekukwazwa. Mie nimekuja tu kuomba kama kuna mtu anaweza anishike mkono. Penye mapungufu tuvumiliane 🙏
 
Asante mkuu, sorry kama kuna kitu nimekukwazwa. Mie nimekuja tu kuomba kama kuna mtu anaweza anishike mkono. Penye mapungufu tuvumiliane 🙏
Huna mapungufu lakini usitake sana huruma za watu ndio maana nikakuambia tafuta mtaji hata kwa kazi za kibarua uwekeze kwenye kitu unachoweza fanya utatoboa sasa ww unaona kama nimekuambia vibaya wakati uhalisia ndio huo.
 
Huna mapungufu lakini usitake sana huruma za watu ndio maana nikakuambia tafuta mtaji hata kwa kazi za kibarua uwekeze kwenye kitu unachoweza fanya utatoboa sasa ww unaona kama nimekuambia vibaya wakati uhalisia ndio huo.
Lakini mkuu mimi nimeomba mtu aliye na nafasi anisaidie, ndio kutafuta kwenyewe maana huwezi jua riziki itapatikana wapi inaweza kuwa hata hapa JF. Sasa sijaelewa kutaka huruma unamanisha nini. Anyways nimepokea ulichoandika.
 
Mnatukatisha wengn kuendelea na elimu ya juu aisee, yn kwa profile yko hiyo mkuu hauna ajira mpk Leo...dah? Mungu akuone ndugu yng akufungulie milango
Maisha sio ajira wala shule
 
Wasio soma mukiwataja kwanamna hii ya kuwasema wasomi wanaopitia changamoto ina sound fun all time inakuwa kwa namna hii msomi aki face chllenge atatajwa asiyesoma ambaye angalau anapata ahueni SOUND FUN ila pale hao wasomi wakifanikiwa wakirudisha Energy hiohio nakusimanga wasiosoma utaanza kuona sentence nyingi zikimtaja MUNNGU, Mungu hivi, Mungu vile All Fun ina desappper

AY 5225 tia neno
 
Hakika
 

Nimejifunza kwamba miongoni mwa skills nzuri sana kuwa nayo maishani ni composure. Ni kawaida sana kwa mtu alienacho kuwaona wasionacho kwamba kuna sehemu wanakosea, ni kawaida yetu binadamu.

Nimesoma comments zote za huyo jamaa sio tu kwenye uzi huu, hata kwenye uzi wangu wa kuomba kazi. Nilichogundua kutoka kwake ni kuwa yeye ni aina ya watu wanaofikisha ukweli mchungu ambao wengi wetu hatupendi ama hatuko tayari kuusikia hasa ukizingatia mtu kama mtoa mada aliekaa darasani kwa takribani miaka 19 kuitafua hio master's aliyonayo.

Shida ipo sehemu moja tu, angesoma vizuri story ya mtoa mada angeona ni kwa jinsi gani amepambana na bado anaendelea kupambana bila kukata tamaa.

Angesoma vizuri angetambua kwamba sio rahisi kubadilisha imani ya mtu alietumia miaka yote hiyo na gharama kubwa katika kutafuta kitu na mambo yakaenda tofauti na alivyodhania na kumtaka atumie mbinu mbadala kwa dhihaka.

Angesoma vizuri angetambua kwamba mtoa mada kashasema alipata shida ya mgongo kwa kufanya vibarua hivi hivi ambavyo yeye anashauri kwa dhihaka mtoa mada avirejee.

Kuna wakati mwingine mtu unatakiwa kujifunza tu ku'skip kitu ambacho unaona kitakufanya utoe kauli za kuumiza binadamu wengine.

Brother mtoa mada ana master's degree ya PA, if all goes well, siku akabahatika kukamata ofisi ya serikali, kipi kimfanye awe mnyenyekevu kwa watu ambao walikua wakimdhihaki wakati hana hio nafasi?

Anyway, ngoja tu tuukubali ukweli mchungu kutoka kwa wanaodiriki kutubeza kwamba elimu haijatusaidia kitu na hatujishughulishi kwakua hatuna maarifa mbadala ya kuishi. Tutazivumilia dharau na masimango yote huku tukitumainia kesho yetu.

And if a day ever comes and the tables turn, I hope we will be humble enough not to take vengeance. Ninachojua ni kwamba inaweza isilete matokeo ya haraka, ila elimu haijawahi kukosa faida. Wacha muda uamue.
 
Eb saidieni watu kama mnasaidia acheni kuleta u much know kwenye maisha ya wa2 auna msaada pita pemben sio mnajaza migazeti utafikir watu ni wageni wa maisha nyny ndo mnafudnshamnaandika pumba
 
Kila mtu ashinde zake ugali ufike mezani uwe umesoma au haujasoma. Mbona wapo wasomi na wanafanya kazi za watu wasiosoma na zimewatoa kimaisha. It depends on how you choose to see it
 
Eb saidieni watu kama mnasaidia acheni kuleta u much know kwenye maisha ya wa2 auna msaada pita pemben sio mnajaza migazeti utafikir watu ni wageni wa maisha nyny ndo mnafudnshamnaandika pumba

Huku umeongea pumba kwakua umekurupuka hujasoma yaliyokua yanaendelea. Mtoa mada kaomba asaidiwe nafasi ya kazi halafu kaja mtu anamwambia mara arudi kufanya vibarua atafute mtaji wakati kashasema ana shida ya mgongo, mara kamwambia aache kutafuta huruma ya watu na mengineyo. Comment yang hapo juu imelenga kumpa moyo na kujipa moyo me mwenyewe pia kwakua napitia the same damn thing.

Acha makasiriko yasiyo na maana.
 
Kichwa yangu ipo lesi bab usiwaze
 
Alafu wewe unajua kazi za vibarua ni kama ku beba tofari, saidia fundi, na makazi magumu magumu huko viwandani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…