Mtaji wa pamoja kwenye mradi wa kilimo- (joint capital)

Mtaji wa pamoja kwenye mradi wa kilimo- (joint capital)

Revolution

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2008
Posts
960
Reaction score
927
Wandugu Habari za leo,

Ninapenda kutoa pendekezo hapa ambalo wadau watakaovutiwa nalo watatoa michango yao ya ku-modify zaidi wazo langu. Kutokana na hali ya maisha kuwa ngumu ni dhahiri sasa watu wengi wanafanya shughuli za maendeleo kwa pamoja. Kinachatakiwa hapa ni willingness, trust, commitment na creativeness.

Kifupi ninatafuta vijana kumi mpaka kumi na tano, lets say kuanzia miaka 20 hadi 45 ambao tunaweza kuweka mitaji ( mali, nguvu, muda na akili) yetu pamoja na kuanza kufanya miradi mikubwa ya kilimo cha umwagiliaji, biashara ya kununua, kuweka na kuuza, au biashara nyingine ambayo itaweza kusimamiwa na wajumbe na ikawa ni ya mafanikio makubwa (Ila binafsi ninapendelea zaidi kilimo- kwasababu kikifanywa kwa ufanisi na ueledi kinaweza kuwalipa wajumbe wote kwa kiwango cha juu).


Mimi nipo Dar es salaam hivyo ningefurahi ningepata wajumbe wataokuwa interested kutoka Dar ama la wajumbe wanaweza kutoka mikoani as long as kutakuwa na namna nzuri ya kukutana sehemu ya uzalishaji. mathalani, shambani.


Wazo langu ni kupata wajumbe hao kumi mpaka kumi na tano, kufungua kampuni brela kwa kuisajili, kuomba sehemu ya ardhi kubwa lets say kama ekari 3,000 na kuendelea katika serikali ngazi ya wilaya au taifa kama wawekezaji wa ndani. Lakini kabla ya hapo wajumbe tutakaopatikana tutaanza na kujichanga kwanza kwa mwaka mmoja au mmoja na nusu- ambapo kila mjumbe atatakiwa kuchangia kuanzia Tshs 10,000,000 na kuendelea kwa mwaka kutokana na hisa tutakazoziestablish.


Mnakaribishwa wanaume kwa wanawake, pia mawazo zaidi yanakaribishwa. Naomba wachangiaji walio serious wachangie kama kuna mapungufu yaboreshwe.

WanaJF wanaotaka hii kitu na wanaopenda maendeleo waniPM ili tuanze mchakato wa kutafutana.

NB: Matapeli hawatakuwa na nafasi katika hili.

Nawasilisha.
 
It is good idea.

Ila kwenye initial capital ya Tshs 10Mil kwa member ndio mtihani. Ingeweza kushuka atleast 5mil.

Nilishawahi kufikiri kuanzisha kitu kama hiki but at lower level, targeting graduates wanaotoka vyuo na kuanza kuhangaika na kazi.

Challenge ikawa mitaji itakua midogo compare to number of members then less return.
 
Sijakwelewaa unasema M10 au ulikoseaa ni M1..Kama ni M10 Hiyo kali...sizani kama mtu awe na 10M halafu asiwe ameziwekezaaa....sehemu...
Hiko ni kiasi kikubwaaaaa sanaaa....
 
Ni wazo jema sana, nilishawahi kufanya na baadhi ya wadau, changamoto iko ktk utekelezaji, mpaka leo kashamba ketu kapo na banda la mfanyakazi tulijenga na lipo.

Kazi imekuwa kutoa mshiko ili kazi iendelee,mimi nikushauri uanze kidogo kidogo kwa maana ya idadi ya wadau na mtaji.
 
Good Idea, Na kama alivyo sema Malila, commitment ndo mtihani mkubwa kabisa kuliko wote, hapa unawerza pata hadi watu 500 sasa ukija kwenye real commitment utakuta watu wawili tu.

Ushauri ni kwamba,

-Anza wewe ambaye tiyari uko commited hata ukianza na hekari moja ni sawa, na utakapo kuwa usha anza unaweza pata watu mbele ya safari, Mara nyingi watu wanaogopa kuingiza mtraji kwenye kitu ambacho hakijaanza, so jitahidi nwewe songa mbele na wazo lako na ulicho nacho kama una 10 milioni inatosha sana kwa wewe kuanza safari, then baadae unaweza hata waita watu shambani na kuwaonyesha kazi yako hapo utapata watu na unaweza wapandishia dau.
 
Last edited by a moderator:
Na swala la kutafuta partiner wa Biashara ni gumu kama ilivyo kutafuta mke/mme wa kuoa na zani hata zaidi ya hapo, inahitajika kusomana kwa muda mrefu sana, kujuana, kuna mtu ukimwambia kuanzisha kampuni anakuwa anawaza pesa tu anajua hapa ni pesa ila safari inapo anza na kufikia hata watu kushinda njaa unaweza usimuone, mara nyingi investment kama hizo matokeo huchukua muda mrefu sana sio sawa na biashara ya toyo unanunua leo kesho unataka pesa, so unihitajika uvimilivu wa kipekee kabisa.
 
Wazo ni zuri sana....ila huo mtaji wa 10m ndo kimbembe...mi hata 5m kimbembe. Ila napenda sana hilo lifanyike

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Na swala la kutafuta partiner wa Biashara ni gumu kama ilivyo kutafuta mke/mme wa kuoa na zani hata zaidi ya hapo, inahitajika kusomana kwa muda mrefu sana, kujuana, kuna mtu ukimwambia kuanzisha kampuni anakuwa anawaza pesa tu anajua hapa ni pesa ila safari inapo anza na kufikia hata watu kushinda njaa unaweza usimuone, mara nyingi investment kama hizo matokeo huchukua muda mrefu sana sio sawa na biashara ya toyo unanunua leo kesho unataka pesa, so unihitajika uvimilivu wa kipekee kabisa.

Trick ya kuanza mwenyewe mdogo mdogo kwa mtaji mdogo ni nzuri, ila inachukua muda sana kufikia malengo, mimi nimeshafanya zote mbili, ya kuanza mdogo mdogo kivyangu imechukua miaka mitano mpaka nikaja kukubalika na jamii inayonizunguka, ya kuanza kama kundi nimeshindwa mara mbili ktk steji ya utekelezaji, na mara ya tatu tumeanza vizuri kwa kuchukua project niliyofanya peke yangu kwa miaka mitano.

Kwa hiyo utaona kwamba, pale panapoonyesha dalili za ushindi/matokeo chanya ndipo ambapo watu huingiza mtaji fasta, kama kuuza hisa za kampuni nzuri. Kuna wakati nilitembea kwa mguu 30km baada ya kukosa usafiri, lakini leo ni faraja. naungana na Chasha hapo juu, jitolee sana na ukaze moyo, ipo siku tutakufuata.
 
Ni wazo zuri sana.

Linahitaji kufanyiwa kazi kwa kina.

Count me in, ikiwa hicho kigezo cha umri utakiondoa. Kwanini mtubague wazee?

faiza,

Ukiona vijana wanakuzingua, njoo uungane na mimi tupige kazi Mkuranga kwetu karibu na Mpafu, pale si karibu na kwenu Boza?
 
Hata 40 no problem si share zangu zinaongezeka.kwi kwi kwi teh teh teh
sasa kama unacapital hiyo kwann usiwekeze faizafoxy?tena kama ni mimi ningefanya kilimo cha kitaalamu sana,angalaukwa shamba heka 8 lenye maji.
 
kaka wazo nzur sana bt wengi hawawezi kuchangia ml 10 .labda tujaribu kukusanya mawazo ya wengi natuone tunaanzajae labda 5ml.
 
pia na ushauri! iv sasa mazao yanavunwa nakuzwa kwa bei ndogo na baada ya miezi 3 bei itapanda! kuna sehemu ni sh30 gunia la debe 7. alafu unaenda kuuza kwa sh 35 kwj kilo moja! unaonaje wadau! tunaweza anza na hlo moja anakusanya mazao mwingne anasafirisha hata kupeleka kenya!
 
pia na ushauri! iv sasa mazao yanavunwa nakuzwa kwa bei ndogo na baada ya miezi 3 bei itapanda! kuna sehemu ni sh30 gunia la debe 7. alafu unaenda kuuza kwa sh 350 kwa kilo moja! unaonaje wadau! tunaweza anza na hlo moja anakusanya mazao mwingne anasafirisha hata kupeleka kenya!
 
Mkuu Revolution tunakuomba urudi kwenye uzi wako huku.
Kama unamaanisha ulichokiandika, basi natuanze sasa hivi. Binafsi ardhi ninayo ila ningekushauri tuanze mdogo mdogo kama wengi walivyopendekeza. Tuanze na ekari10 kwa kilimo cha umwagiliaji. Mimi shamba lililo karibu na chanzo cha maji ninalo na muda wa kujitolea kukaa shamba upo wa kutosha even over a year.
Nikomee hapa kwanza, utakapojibu post hii tutaendelea na mazungumzo hapahapa ili kila mdau apate wasaa wa kushiriki na kuchangia mawazo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Revolution tunakuomba urudi kwenye uzi wako huku.
Kama unamaanisha ulichokiandika, basi natuanze sasa hivi. Binafsi ardhi ninayo ila ningekushauri tuanze mdogo mdogo kama wengi walivyopendekeza. Tuanze na ekari10 kwa kilimo cha umwagiliaji. Mimi shamba lililo karibu na chanzo cha maji ninalo na muda wa kujitolea kukaa shamba upo wa kutosha even over a year.
Nikomee hapa kwanza, utakapojibu post hii tutaendelea na mazungumzo hapahapa ili kila mdau apate wasaa wa kushiriki na kuchangia mawazo.

Mkuu Kisima na wadau wengine ninashukuru kwa kuonyesha support kwenye wazo hili. Mawazo ya wadau wengi naona yamejikita kwenye capital kuwa ni kikwazo...kweli hata mimi nalijua hilo lakini nilipotoa hili.wazo niliona hicho ndicho kianzio kizuri ambacho kama group tunaweza kuanza vizuri hata hivyo niliplan hiyo capital tuichange kidogo kidogo even over a year. Najua kabisa kuwa na hii hela kwa mkupuo kwa wengi wetu ni mtihani, hata kwangu pia.
 
Last edited by a moderator:
Ni wazo zuri sana ila tatizo la biashara ya kikundi mkisha kuwa wengi management inakuwa ni tatizo,achilia mbali swala la commitment

Nafikiri bora muanze watu watano kwa mtaji hata wa 10M,kila mtu 2M kuliko kuanza watu 15 kwa mtaji wa 150M.Siki zote biashara nzuri ni ile iliyoanza kidogo ikakua na kuwa kubwa.
 
Back
Top Bottom